Saturday 7 January 2017

Waziri Nchemba: Hatutamhukumu mtu kwa kazi anayoifanya, tutamhukumu kwa kosa analolifanya

...

Ikiwa imepita siku moja tangu waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba kusema kuwa watakaofanya unyama wa kuua au kuchinja watu au wanyama kwa mapanga na sime wataona chamoto, bado kauli hiyo imekaidiwa kwa baadhi ya watu wanaosadikika kuwa ni wa jamii ya kifugaji baada ya kumjeruhia kichwani kwa sime Rajabu Ayub (36) mkazi wa kijiji cha Mbigiri wilayani kilosa, akiwa shambani kwake na kumsababishia maumivu.

Polisi mkoani Morogoro mpaka sasa inawashikilia watu 24 kwa mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo. Waziri Mwigulu Nchemba ameagiza nguvu zaidi ya dola iongozwe katika maeneo hayo mpaka mhusika wa tukio hilo atakapopatikana.

Hili ni tukio la pili tangu Waziri Mwigulu awepo mkoani Morogoro la kwanza likiwa la Fabiano Bago mkazi wa kolelo wilaya ya Morogoro ambaye alijeruhiwa maeneo ya kichwani kwa sime na watu wa jamii ya kifugaji mara baada ya kumuona akiongea na simu wakidhani anawataarifu polisi na Fabian alifariki dunia kutokana na majeraha aliyopata
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger