Wednesday 11 January 2017

MBWANA SAMATA KUENDELEA KUSHINDANIA NAMBA YAKE GENK

...
Siku 14 zimepita toka mshambuliaji wa KRC Genk Nikolaos Karelis ambaye alikuwa anashindania namba na mtanzania Mbwana Samatta atangazwe kuwa atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi 8 hadi 9 kufuatia jeraha la goti la kushoto alilolipata wakati wa mchezo dhidi ya KAA Gent dakika ya 51 December 27.

January 10 2017 KRC Genk imetangaza kukamilisha usajili wa mshambuliaji Jose Naranjo kutokea Celta Vigo ya Hispania, hiyo itakuwa ni changamoto mpya kwa Mbwana Samatta kuendelea kupambania namba ya kucheza na Naranjo katika kipindi ambacho Karelis atakuwa nje.

Jose Naranjo amejiunga na KRC Genk ya Ubelgiji akitokea Celta Vigo ya Hispania kwa mkataba wa miaka mitatu na nusu, Naranjo mwenye umri wa miaka 22 amewahi kuichezea Villarreal kwa mkopo mwaka 2014 akitokea Recreativo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger