Sunday 15 January 2017

MWANAFUNZI MTANZANIA ALIYEKUWA AKISOMA NCHINI CHINA AFARIKI DUNIA NA KIFO CHAKE BADO KINA UTATA

...
tumepata taarifa za kuhuzunisha ambazo zinamhusu binti mtanzani aliyekuwa anasoma nchini China katika Chuo Kikuu cha Nanchang aliyekuwa akitambuliaka kwa jina la Safina John kuwa amefariki dunia. Marehemu alikutwa amefariki usiku wa kuamkia tarehe 13 Januari 2016 chumbani kwake.
Bado kuna utata mkubwa juu ya chanzo cha kifo cha marehemu kutokana na kuwa na taarifa tofauti zinazokinzana. Taarifa kutoka kwa watu wa karibu yake zinasema  marehemu alikuwa anaumwa kwa takribani wiki mbili zilizopita na alikuwa haonekani darasani wakati wakala wa marehemu huyo (Global Education Link) ametoa taarifa na kusema kifo ni cha ghafla. Bado uchunguzi wa chanzo chakifo hicho unaendelea. Taratibu zakusafirisha mwili wa marehemu zinafanyika.
Chuo alichokuwa akisoma marehemu
KUHUSU KUSAFIRISHA MWILI
Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TASAFIC (Umoja wa wanafunzi wanaosoma China)  ni kwamba, gharama za kusafirisha mwili  ni Dola 10000 ambayo ni sawa na 63,000RNM yaani takribani Tsh Millioni 20. Gharama hizi zinatakiwa kulipwa na familia ya marehemu  na siyo wakala wake “Agent”  japo wakala amesema atalipa halafu familia itazirudusha.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger