Saturday 15 May 2021

NAMUNGO FC WAITUNISHIA MISULI YANGA SC ...MASHABIKI WAONDOKA KWA HASIRA BAO KUKATALIWA

...
Vigogo Yanga SC wamelazimishwa sare ya bila mabao na wenyeji Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.

Hata hivyo mashabiki wa Yanga waliondoka na hasira uwanjani kufuatia refa Hance Mabena wa Tanga kukataa bao lao lililofungwa na mshambuliaji Mburkinabe, Yacouba Sogne kwa kichwa akimalizia mpira wa kona kipindi cha pili.

Kwa sare hiyo, Yanga SC inafikisha pointi 58 baada ya kucheza mechi 28 na inabaki nafasi ya pili, sasa ikizidiwa pointi tatu na mabingwa watetezi, Simba SC ambao pia wa mechi tatu mkononi, wakati Namungo FC yenyewe inafikisha pointi 36 baada ya mechi 26 nayo pia inabaki nafasi ya 10.

Via Binzubeiry blog
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger