Ofisi ya Waziri Mkuu –
TAMISEMI inatangaza orodha ya Majina 3,733
ya watumishi wa Umma waliohamishwa katika Mamlaka za Serikali za mitaa
nchini,Aidha orodha ya watumishi 112
ambao hawakukidhi vigezo vya kuhama nayo imetangazwa.
KUBADILISHA SHULE NA TAHASUSI KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO 2014
Taarifa ya uchaguzi wa wanafunzi wa
kuingia kidato cha Tano katika Shule za Serikali na Vyuo vya Ufundi kwa
mwaka 2014 ilitangazwa kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI mwezi Juni,
2014. Wanafunzi waliochaguliwa awali walitakiwa kuripoti kuanzia tarehe
10 – 30/7/2014 .
Baada ya taarifa ya Uchaguzi wa wanafunzi
kutolewa, baadhi ya wanafunzi/wazazi/walezi wamewasilisha barua za
maombi ya kuwabadilishia wanafunzi waliochaguliwa shule na tahasusi au
mojawapo ya hivyo. Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI baada ya kupokea
imechambua maombi hayo na kubaini kuwa sababu zilizotolewa kwenye baadhi
ya maombi hayo zina tija na hivyo kulazimika kuridhia kuwabadilishia
shule, tahasusi au vyote kwa pamoja baadhi ya wanafunzi hao.
Wakati
jamii ikiwa bado haijasahau mateso aliyoyapata mtoto Nasra Mvungi na
kusababisha kifo chake, tukio lingine la aina hiyo limetokea katika
Kijiji cha Matongola, Tarafa ya Magole Wilaya ya Kilosa, baada ya
kubainika mtoto wa miaka sita akiwa amefichwa uvunguni mwa kitanda na
kufanyiwa vitendo vya kikatili na mama yake mzazi.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu (kulia) wakiongozana na Madona Pemba
(kushoto) , mtanzania aishie Uingereza kuelekea kwenye ukmbi wa mikutano
ili kuzungumza na watanzania waishio Reading.
STAA wa sinema za Kibongo, Miriam Mjolwa ‘Jini
Kabula’ amecharuka baada ya kukosolewa juu ya mavazi ya mitego, vimini,
anayovaa ndani ya mwezi wa Ramadhani.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY STAA
wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja ameibuka na kusema kuwa ushosti
wake na Miss Tanzania 2006/07, Wema Sepetu, uliorudishwa hivi karibuni
baada ya kuwekana sawa ni wa kinafiki huku akidai Wema ni kigeugeu.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY Mkuu wa Chuo cha Misitu Olmotonyi, Arusha anayo furaha
kuwataarifu wafuatao kuwa wamechaguliwa kujiunga na Chuo cha Misitu
Olmotonyi, Arusha kwa udhamini wa binafsi, Wakala wa Huduma za Misitu na
Mradi wa ECOPRC kwa mafunzo ya
Askari
Polisi wakimtoa nje daktari feki, Karume Habibu (22) kutoka kwenye
ofisi ya Mganga Mkuu wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ambako
alihojiwa kabla ya kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi.
Sekretarieti
ya Ajira katika Utumishi wa Umma inawatangazia Watanzania wenye sifa
na uwezo kujaza jumla ya nafasi wazi za kazi 1,324 ambazo ni kwa ajili
ya waajiri mbalimbali Nchini.
Katibu
wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Xavier Daudi amesema kuwa nafasi 1,334
zimeainishwa bayana kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ambayo ni
www.ajira.go.tz ili kuwawezesha wahitimu wote wenye sifa na uwezo
kutuma maombi kwa ajili ya kujaza nafasi hizo ajira Serikalini.
"Nadhani ni vizuri zaidi kwa kila
muhitimu anayetafuta kazi serikalini kufungua tovuti ya Sekretarieti ya
Ajira kuangalia nafasi za kazi zilizotangazwa na pale anapoiona kazi
inayoendana na sifa alizonazo kutuma maombi yake ili kuweza
kushindanishwa na wengine....maana ajira za Serikali hivi sasa ni za
ushindani hivyo inampasa kila anayetaka kupata kazi serikalini kujiandaa
vyema ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuajiriwa katika
Utumishi wa Umma" alisema Daudi.
Alifafanua
kuwa kwenye tovuti hiyo kuna matangazo mawili tofauti ya kazi ambapo
moja liko katika lugha ya Kingereza likiwa na jumla ya nafasi za kazi
447 na tangazo lingine lipo kwa lugha ya Kiswahili ambalo lina jumla ya
nafasi za kazi 877.
Aidha,
alizitataja baadhi ya nafasi hizo za kazi zilizoko katika tangazo la
kazi kwa lugha ya Kiswahili kuwa ni Mhandisi kilimo (agro–engineers),
Afisa kilimo (agro–officers) Mkufunzi kilimo (aquaculture), Afisa kilimo
msaidizi (agricultural field officers), Daktari wa mifugo (veterinary
officers), Daktari utafiti mifugo (veterinary research officer), Daktari
mifugo mkufunzi (veterinary tutor), Mkufunzi mifugo (animal science),
Afisa mifugo (live stock officer), Afisa utafiti mifugo (livestock
research officer), Afisa Utumishi (human resources officer), Afisa ardhi
msaidizi, Dereva (driver).
Basi la Amani Express likitokea Kigoma kuelekea Dar es salaam limepata
ajali usku wa kuamkia leo maeneo ya Salanda mkoani Tabora, ambapo mtoto
wa miaka mitatu amepoteza maisha na abiria kadhaa wamepata majeraha.
Mashuhuda wanahisi kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi. Pichani
abiria wakitafuta vitu vyao
Bodi
ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inawafahamisha waombaji wa
mikopo kwa mara ya kwanza na Umma kwa ujumla kwamba muda wa maombi ya
mikopo umeongezwa kwa mwezi mmoja kutoka Julai 1, 2014 hadi Julai 31,
2014.
Bodi ilianza rasmi kupokea maombi ya mikopo kwa njia ya mtandao kuanzia
Aprili 23, 2014 ambapo tarehe ya mwisho wa kupokea maombi hayo ilikuwa
Juni 30, 2014.
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imetoa muda wa nyongeza kwa
waombaji wa mikopo kukamilisha maombi ya mikopo katika kipindi cha siku
30, kupitia mtandao kwa anuani: http://olas.heslb.go.tz.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
NAIBU Waziri wa Maji, Mheshimiwa Amos Makalla amegeuka mbogo kufuatia
madai ya kukwepa kodi kupitia gari analodaiwa kulimiliki aina ya Toyota
Dyna lililokamatwa na maofisa
Mlezi wa chama cha wakulima wa pamba nchini na msemaji
wa wabunge wanaotoka katika mikoa inayolima zao la pamba nchini,mbunge wa Maswa
Magharibi kupitia Chadema mheshimiwa John Shibuda amewapigia filimbi wasukuma
kwa kuwataka kuamka na kueleza wazi wazi matatizo yanayowakabili badala ya
kukaa kimya na kusema hakuna tatizo(Nduhu Tabhu” wakati kuna tatizo
linawasumbua.
Rais Jakaya Kikwete amesema serikali imetenga kwa kila halmashauri ya
wilaya nchini kupatiwa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa
nyumba za walimu ili kuwapunguzia adha na usumbufu walimu wanapopangiwa
kwenda katika vituo vya kazi wanakosa mahali pa kuishi.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
AMA
kweli ng’ombe wa maskini hazai, kijana Peter Sitiwati (26), mkazi wa
Sinza ya Kwaremmy jijini Dar amejikuta akikatisha ndoto za utafutaji
maisha kufuatia kuoza mguu baada ya ajali mbaya ya gari. Akizungumza
na mwandishi wetu jijini Dar juzikati kwa sauti ya kukata tamaa, Peter
alisema alipata ajali ya gari mwaka 2013 maeneo ya Sinza-Mori, Dar na
kuumia vibaya mguu wa kulia.
kijana Peter Sitiwati akiwa na maumivu makali yaliyosababishwa na kuoza kwa mguu.
’’Baada ya kugongwa na gari niliangukia mtaroni nikachomwa na kijiti
kwenye mguu wa kulia.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY STAA wa filamu Bongo, Rose Ndauka amefunguka kuwa
kwa sasa yeye na msanii mwenzake, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ ambaye
aliwahi kukwaruzana naye wameshamaliza na kujikita katika kazi zaidi.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
JESHI
la Polisi Mkoa wa Arusha linamsaka kwa udi na uvumba, muuza nyama
jijini hapa, Lucas Lomayany Molel (37) mkazi wa Ilboru kwa madai ya
kumuua mkewe wa ndoa, Agnes Lucas (24) kwa kumcharanga na sime kwa kile
kinachoelezwa kuwa ni kutokana na wivu wa mapenzi.
Kipa wa Argentina Sergio Romero alikuwa Nyota wa mechi hiyo
Argentina imejukatia tikiti ya kufuzu kwa fainali yake ya kwanza tangu mwaka wa 1990 ambapo itachuana Ujerumani. Argentina ilikuwa imetoka sare tasa
baada ya muda wa kawaida na ule wa Ziada na hivyo kulazimu mechi hiyo
kuamulia kwa mikwaju ya penalti. Kipa wa Argentina Sergio Romero ndiye
aliyekuwa nyota katika mechi hiyo baada ya kuokoa mikwaju miwili na
kuipa Argentina Ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Uholanzi.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
“Namshangaa mama Kanumba… BABA
wa aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba,
Charles Kanumba ameibuka na kumtaka mama Kanumba, Flora Mtegoa kuacha
tabia ya kuombaomba michango mbalimbali.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY Na Mwandishi Wetu WAKATI jana, Julai 9, 2014 George Otieno Okumu
‘Tyson ametimiza siku 40 tangu kifo chake kilichotokea kwa ajali mbaya
ya gari mkoani Dodoma, mama mzazi wa marehemu, Gladys Okumu ameripotiwa
kuugua ghafla nchini Kenya anakoishi.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY Stori: Waandishi Wetu STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul
‘Diamond’ amefanya tukio la kihistoria kiasi cha kumliza mama yake
mzazi, Sanura Kassim ambaye alimwaga machozi kama mtoto mbele za watu.
Tukio la mama Diamond kumwaga machozi lilishuhudiwa na kamera za Amani,
juzi Jumatatu, mishale ya saa mbili usiku nyumbani kwake, Sinza jijini
Dar es Salaam ambako kulikuwa na ‘bethidei’ ya mama huyo.
MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO WA TAREHE 8 JULAI 2014
EXAMINATION RESULTS FOR RESEARCH ASSISTANTNCC
Usaili wa mahojiano utafanyika tarehe 9/7/2014 SAA MOJA KAMILI ASUBUHI. katika OFISI ZA NATIONAL CONSTRUCTION COUNCIL (NCC)
NB:
WASAILIWA WANATAKIWA KUZINGATIA MUDA NA SEHEMU ILIYOTAJWA KWA AJILI YA
USAILI NA KUJA NA VYETI HALISI (ORIGINAL CERTIFICATES). Na.EXAMINATION NUMBER SCORE REMARKS 1 PSRS RESE ASS NCC - 121 80 SELECTED 2 PSRS RESE ASS NCC - 118 73 SELECTED
3 PSRS RESE ASS NCC - 124 73 SELECTED 4 PSRS RESE ASS NCC - 128 66 SELECTED
WAHITIMU
39 wa kidato cha nne mwaka jana katika Shule ya Sekondari Karobe jijini
hapa wakiwa na wazazi wao, jana waliandamana hadi ofisi za Mkuu wa Mkoa
ili kujua hatma yao baada Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
kushindwa kuwapangia nafasi za kujiunga kidato cha tano licha ya kufanya
vizuri katika mitihani yao.
Kiongozi wa mbio za mwenge RACHEL KASSANDA, amefungua bweni la
wasichana la shule ya sekondari MSINDO na kuweka jiwe la Msingi katika
majengo ya vyumba vinne vya madarasa na Maabara moja katika shule ya
Sekondari RWINGA wilayani NAMTUMBO mkoani RUVUMA.
Vijana
wawili waliokuwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Chemchem wilayani
Mkalama katika Mkoa wa Singida, wamehukumiwa kifungo cha miaka sita kila
mmoja baada ya Mahakama kuwatia hatiani kwa kosa la mauaji ya mwalimu
wao.
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY Stori: Mwandishi wetu MWANAMUZIKI aliyefariki dunia, Amina Ngaluma maarufu
kama Japanese alifikisha siku 40 tokea azikwe Jumamosi iliyopita,
lakini katika kisomo kilichosomwa nyumbani kwao Kitunda, hakuna staa
yoyote wa muziki wa dansi aliyehudhuria.
Miroslav Josef Klose akishangilia baada ya kutupia bao la pili kwa Ujerumani usiku huu na kuvunja rekodi ya kupachika mabao.
Klose wakati akifunga bao lake la 16 katika michuano ya kombe la dunia.
Mkali wa mabao Miroslav Josef Klose.
MSHAMBULIAJI wa Ujerumani na timu ya Lazio ya Italia, Miroslav Josef
Klose, ameweka historia usiku huu baada ya kutupia bao lake la 16 na
kuwa mfungaji wa mabao mengi katika michuano ya Kombe la Dunia iliyoanza
mwaka 1930 ambayo kwa sasa inaendelea nchini Brazil.
Klose ameifungia Ujerumani bao la pili wakati ikitoa kichapo cha
mabao 7-1 dhidi ya Brazil katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia
2014.
Klose alifunga mabao matano katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka
2002 na 2006, akatupia manne huko Afrika Kusini mwaka 2010 na mpaka
sasa huko Brazil tayari amefunga mabao mawili moja dhidi ya timu yake na
Ghana wakati la pili dhidi ya Brazil leo.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 36 amempiku mshambuliaji wa Brazil, Ronaldo Luís Nazário de Lima aliyekuwa na mabao 15.
Wachezaji wengine waliowahi kufunga mabao zaidi ya 11 kwenye michuano
hiyo ni: Gerd Muller wa Ujerumani 14, Just Fontaine wa Ufaransa 13,
Pele wa Brazil 12, Jurgen Klinsmann wa Ujerumani 11 na Sandor Kocsis wa
Hungary 11.