Wednesday 1 May 2024

AMUUA MWENZAKE KWA KISU WAKICHEZA MUZIKI BAA

...


Mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam, Kadi Msela, ameuawa kwa madai ya kuchomwa kisu na rafiki yake aliyetajwa kwa jina moja la Amir, wakati wakicheza muziki baa.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amethibitisha tukio hilo lililotokea Aprili 20, mwaka huu.

Akizungumza na Nipashe Digital, Muliro amesema: “Ni kweli kuna tukio hilo la kijana Kadi kufariki dunia kwa madai ya kuchomwa kisu na rafiki yake Amir. Taarifa za awali zinaeleza kwamba wawili hao walikuwa marafiki na walitofautiana.”

Kamanda Muliro amesema kwa mujibu wa mashuhuda kijana huyo alichomwa kisu sehemu ya shingoni wakati wakicheza muziki katika baa moja iliyokuwa ikizinduliwa eneo la Tegeta.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger