Sunday 9 January 2022

BABU WA MIAKA 84 ADUNGWA CHANJO 11 ZA CORONA

...
Babu mmoja kutoka nchini India mwenye umri wa miaka 84, amekamatwa baada ya kudai kuwa amedungwa chanjo 11 ya virusi vya Corona.

Kwa mujibu wa ripoti ya gazeti la The New Indian Express, Brahmadeo Mandal mwenye umri wa miaka 84, mkazi wa jimbo la Bihar Mashariki alifanikiwa kupokea dozi hizo kwa kutumia vitambulisho tofauti na nambari za simu za jamaa zake.

Arubaini za mzee huyo zilifika alipokuwa amekwenda kwenye kituo cha afya akiwa anataka kupata dozi ya 12.

 Akielezea nia yake Mandal alisema serikali imefanya jambo la maana na ndio sababu yake ya kupata chanjo kupita kiasi.

Kulingana na mzee hiyo, kufikia mwishoni mwa mwaka 2021, alikuwa tayari ameshapokea jumla ya chanjo 11 na kuongeza kuwa anahisi vizuri.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger