Friday 3 December 2021

MTOTO ACHOMWA KWA MKASI WA MOTO AKITUHUMIWA KUIBA 'FLASH' YA MOVIE SHINYANGA MJINI

...

Muonekano wa sehemu alizojeruhiwa mtoto huyo  kwa kuunguzwa na mkasi wa kukatia fensi uliochemshwa kwenye jiko la mkaa akituhumiwa kuiba ‘Flash’ ya mama na bibi yake.
Muonekano wa sehemu alizojeruhiwa mtoto huyo.
Muonekano wa sehemu alizojeruhiwa mtoto huyo.
Muonekano wa sehemu alizojeruhiwa mtoto huyo  kwa kuunguzwa na mkasi wa kukatia fensi uliochemshwa kwenye jiko la mkaa akituhumiwa kuiba ‘Flash’ ya mama na bibi yake.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 9 anayesoma darasa la tatu shule ya Msingi Bugoyi A Mjini Shinyanga amejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kuunguzwa na mkasi wa kukatia fensi uliochemshwa kwenye jiko la mkaa akituhumiwa kuiba ‘Flash’ ya mama na bibi yake.


Mashuhuda wa tukio wameiambia Malunde 1 blog kuwa mtoto huyo alifanyiwa ukatili huo Desemba 1,2021 majira ya saa 2 usiku katika mtaa wa Dome, Kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.

Wameeleza kuwa siku ya tukio jioni alipewa Flash na bibi yake aitwaye Adelida Leonard (50) na mama yake mzazi Beatrice Mwombeki (28) ili aende eneo jirani akaweke Movie (Filamu) kwenye ‘Flash’ lakini akiwa njiani alidondosha Flash hiyo na kurudi nyumbani kutoa taarifa juu ya kupotea kwa Flash hiyo.

“Baada ya mtoto huyo kurejea nyumbani na kuwaelezea bibi na mama yake kuwa Flash imepotea,walimwambia aende akaitafute lakini hakufanikiwa kuipata na akaogopa kurudi nyumbani na ilipofika usiku alirejea nyumbani ndipo akafanyiwa ukatili kwa kuchomwa na kipande cha mkasi wa kukatia maua/ fensi kilichochemshwa kwenye jiko la mkaa sehemu mbalimbali za mwili wake hasa mgongoni na mapajani na kumsababishia majeraha”, wamesema mashuhuda wakizungumza na Malunde 1 blog.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema chanzo cha tukio ni kumtuhumu mtoto huyo kuwa ameiba Flash na kwamba mbinu iliyotumika ni kuchemsha kipande cha mkasi wa kukatia fensi kwenye jiko la mkaa kisha kumuunguza sehemu mbalimbali za mwili wake.

Amesema watuhumiwa ambao ni Adelida Leonard (bibi) na Beatrice Mwombeki (mama mzazi) wamekamatwa na madhura amelazwa katika hospital ya rufaa mkoa wa Shinyanga.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger