Wadau mbalimbali mkoani Kagera kwa kushirikiana na serikali pamoja na wananchi wametakiwa kulipa kipaumbeli swala la lishe bora mkoani hapa hili kupunguza na hatimaye kuondoa tatizo la lishe duni linalokabili makundi mbalimbali hususani watoto.
Hayo yameazimiwa katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (Rcc) mkoani Kagera kilicho fanyika katika ukumbi wa mikutano wa mkoa mnamo tarehe 21/10/2019 nakukutanisha wajumbe zaidi 50 wakiwemo wakuu wa wilaya zinazounda mkoa wa kagera,wenyeviti wa halmashauri ,wajumbe wakamati ya ulinzi na usalama pamoja nawadau mbalimbali kutoka katika mashirika ya serikali na yasiyo ya kiserikali chini ya mkuu wa mkoa kagera Brigedia Marco Gaguti
Ili kufikia azimio hilo wajumbe wa kikao hicho wameazimia kuwa kila mwananchi anaye ishi katika mazingira ya kilimo lazima alime kiasi cha hekali moja ya mazao ya chakula pamoja na hekali moja ya mazao ya biashara ili kufikia malengo nakuondoa udumavu
Aidha akizungumzia soko la kahawa katibu tawala wa mkoa wa kagera Faustine Kamzola katika kikao hicho amesema wananchi wamkoa wa Kagera wanatakiwa kuwa wa kwanza kutumia zao hilo mara baada yakuwa limeongezewa thamani ikiwa ni baada ya kutoka kiwandani nakusema kuwa nchi za Ethiopia,Uganda na nchi kama Brazil niwazalishaji wa Kahawa kwa kiwango kikubwa lakini pia ni watumiaji wakahawa kwa wingi ukilinganisha na mkoa wa Kagera na nchi kwa ujumla.
“Minadhani mkoa wa Kagera ili kukuza soko la biashara ya zao letu la kahawa lazima tuwe wakwanza kutumia mavuno yetu kwsababu hata nchi za Ethiopia Uganda na Brazil ambazo zimefanikiwa katika soko la kahawa wanatumia kiwango kikubwa tofauti nasisi kagera”
Baada ya kuwasilishwa kwa taarifa mbalimbali ndani ya kikao hicho mmoja wa wajumbe kutoka shirika la Kadetfu ambaye nimkurugenzi wa shirika hilo Dokta Peradius Mchuruza amewaomba wajumbe kuazimia kuundwa kwa tume ya watu maalumu (tasiki force) itakayochunguza maendeleo ya maazimio yaliyowekwa katika wiki ya uwekezaji mkoani Kagera
Katika upande wataaluma wajumbe wote wakikao wamepongeza ufaulu katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu baada ya kushika nafasi ya 4 kitaifa kutoka nafasi ya 5 mwaka 2018 mbali napongezi hizobado mkoa unaupungufu wa walimu mbali nakusema kuwa namaeneo mengine yana changamoto za ukosefu wa wataalamu
0 comments:
Post a Comment