Wednesday, 19 March 2025

CWT PWANI YASIFU UCHAGUZI WA VIONGOZI BAGAMOYO

...
Wageni waalikwa na kamati ya utendaji iliyochaguliwa
Mwenyekiti wa uchaguzi, mwalimu Leonard Gange
Katibu wa Chama cha walimu mkoa wa Pwani Mwalimu Suzan Shesha
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo , Shaibu Ndemanga (kulia) na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Bagamoyo, Hamisi Kimeza(kushoto)
Katibu wa CWT wilaya ya Bagamoyo, Mwalimu Joyce Maisa akisoma risala


NA. ELISANTE KINDULU, BAGAMOYO

CHAMA cha walimu mkoa wa Pwani kimesifu uchaguzi wa viongozi wa CWT Wilaya ya Bagamoyo uliofanyika mwanzoni mwa wiki hii katika ukumbi wa Stella Maris mjini hapa.

Sifa hizo zimetolewa na katibu wa CWT mkoa wa Pwani Bi. Suzan Shesha mara baada ya kumalizika kwa zoezi la upigaji kura.

"Niwashukuru kwa kufanya uchaguzi kwa utulivu mkubwa. Niwashukuru pia viongozi waliochaguliwa kwa kipindi cha 2025-2030. Na bila kuwasahau waliothubutu kugombea japo kura hazikutosha", alisema katibu huyo.

Nafasi ya mwenyekiti wa Chama cha walimu wilaya ya Bagamoyo na idadi ya kura kwenye mabano ni Hamisi Juma Kimeza (100), Alfred Peter Ringi(52), Bilali Mkeha (25), Nyamba Johanes(9) na Linus Aidan (7).

Kwa upande wa mweka hazina ,Mwalimu Siza Mnjokava (188) na Mwalimu Samwel Mbwasi (6).

Wanaounda kamati ya utendaji kwa kushirikiana na mwenyekiti na mweka hazina ni pamoja na Mwalilishi wa walimu vijana, David Phares(111) na Bakari Kibangu (79).

Mwakilishi shule za awali walikuwa Stella Mwihambi (93) na Asha Mohamed (88).

Wawakilishi wa shule za msingi zinatakiwa nafasi nne kwa walioongoza kwa kura. Matokeo ni kama ifuatavyo, Elisante Kindulu (51), Msafiri Innocent (38), Bahati Mohamed (32), Mohamed Kiparai (16), Hamisi Tuwaqal(15) na Ali Makame (1).

Nafasi mbili za wawakilishi wa shule za sekondari zilichukuliwa na Bernad Kapera na William Mrope.

Wagombea waliopigiwa kura za ndio na hapana na kushinda ni Anna Choaji(mwakilishi wa kitengo cha walimu wanawake), Phinus Tuarila(Mwakilishi wa walimu wenye ulemavu), Mzee Kihaku (Taasisi) na Beginus Mbiro (Vyuo).

Kwa upande wa kitengo cha walimu wanawake waliochaguliwa ni Veronica Kirumbi (Mwenyekiti), Anna Choaji(katibu), Theresia Kilimo(mweka hazina), Hawa Magulumali(mjumbe), Pili Mrope (mjumbe), Teddy Setebe (mjumbe) na Saida Msosa(mjumbe).

Wapiga kura katika mkutano huo ni mwalimu mmoja mmoja kutoka kila shule , chuo na ofisi ya elimu wilaya ambapo inafahamika kama tawi la chama mahala pa kazi.

Wilaya ya Bagamoyo ina jumla ya walimu 2189, Kati Yao wanachama wa CWT ni 2154 na matawi ya wawakilishi mahala pa lazi ni 195.

Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger