Saturday 25 June 2016

Shamsa adaiwa kubanjuka na Chid Mapenzi

...

SHAMSA
DIVA anayeuza sura kwenye kiwanda cha filamu Bongo, Shamsa Ford anadaiwa kubanjuka kimalavidavi na mfanyabiashara maarufu jijini Dar anayefahamika kwa jina la Chid Mapenzi, kiasi kwamba wameshindwa kujizuia na kulianika penzi lao hadharani kwenye mitandao ya kijamii.
Madai hayo ya Shamsa kubanjuka na jamaa huyo yameibuka baada ya hivi karibuni kupitia Mtandao wa Kijamii wa Instagram, Chid kuposti picha inayomuonesha akiwa uwanja wa ndege amebeba begi na kuambatanisha ujumbe wa mapenzi akimuaga Shamsa ambaye baada ya muda mfupi alijibu pia akimtakia safari njema.
Gazeti hili lilipomtafuta Shamsa na kumbana alisema; “ Jamani yule ni mtu wangu tu wakaribu, tunataniana sana na hakuna lolote linaloendelea. Kwanza hivi karibuni nataka kufungua biashara yangu ya kuuza nguo na yeye atakuwa ananisaidia kuniletea kutoka nje kwa sababu ni mzoefu kwenye biashara hiyo.”
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger