Tuesday 21 June 2016

Kesi ya Mauaji ya Mwanahabari, Daud Mwangosi Kuendelea Leo

...


Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, jana iliahirisha kesi ya mauaji ya mwanahabari, Daud Mwangosi inayomkabili askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Iringa (FFU), Pasificus Simon hadi leo. 
Kesi hiyo iliahirishwa baada ya upande wa Serikali kufunga ushahidi wake. Kesi hiyo iliyoanza kusikilizwa Februari 12, mwaka 2012, leo inaendelea kwa upande wa utetezi kuleta mashahidi wake mbele ya Jaji Paul Kihwelo anayeisikiliza.

Katika kesi hiyo ambayo haikuchukua muda mrefu mahakamani hapo jana, mawakili wa Serikali wakiongozwa na Sandy Hyra na Ladislaus Komanya walisema wamefunga ushahidi kwa mashahidi wanne wa awali.

Baada ya wakili wa utetezi, Rwezaura Kaijage kukubaliana na maombi ya upande wa Serikali kufunga ushahidi wao, Jaji Kihwelo aliiahirisha kesi hiyo hadi leo.

Awali, mtuhumiwa Simon alifikishwa mahakamani hapo akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ambao hawaruhusi apigwe picha na waandishi wa habari.

Mwangosi aliuawa kwa kupigwa bomu Septemba 2, 2012 katika Kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi alipokuwa akiwajibika kwa kazi za kihabari wakati wa ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger