Thursday 23 June 2016

Kauli ya Magufuli kuhusu kusitishwa kwa ajira

...

Rais Dr. John Magufuli amesema uamuzi wa serikali wa kusitisha ajira mpya na kupandisha vyeo kwa wafanyakazi wa sekta ya umma kwa miezi miwili umelenga kukamilisha zoezi la uhakiki wa wafanyakazi hewa ambao bado wanaligharimu taifa kwa wao kuendelea kupokea mishahara pasipo kufanya kazi.
Rais Dr.Magufuli amesema hayo wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini ya benki kuu ya Tanzania na kusema kuwa hawezi kuendelea kuvumilia kuona wafanyakazi hewa wakiwepo na kwamba kasi ya kuwabaini inaenda sambamba na kutakiwa kurejeshwa kwa mishahara ambayo wamelipwa ama wanaendelea kulipwa.
 
Kuhusu miaka hamsini ya benki kuu, Rais Magufuli amesema benki hiyo inapaswa kujiimarisha katika kuyasimamia maduka ya kubadilisha fedha za kigeni ambayo baadhi yake hutumika kusafirisha fedha nje ya nchi kinyume na taratibu na kutakatisha fedha haramu zikiwemo zile zinatokana na mauzo ya dawa za kulevya sambamba na benki hiyo na hazina kuboresha ukusanyaji kodi katika madini.
 
Naye Gavana wa benki kuu Prof Benno Ndulu pamoja na mwenyekiti wa jumuiya za mabenki nchini Dr.Charles Kimei ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa benki ya CRDB wamesema miaka hamsini ya uwepo wa benki hiyo kuu umekuwa mfano wa kuigwa duniani kutokana na kuisimamia vyema sekta ya fedha na kufanya huduma zitolewazo nchini kuigwa na. Mataifa mengine.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger