Saturday 25 June 2016

Drake ashitakiwa kwa wizi wa mdundo

...

drakewimbledon2015billboard6501.jpgKIMENUKA! Rapa maarufu kutoka Marekani, Aubrey Graham ‘Drake’ ameingia matatani baada ya kukumbwa na tuhuma za wizi wa mdundo hata kushitakiwa na Prodyuza Noel Fisher ‘Detail’ ambaye ndiye aliyetengeneza Wimbo wa Beyonce uitwao Drunk In Love.
Akizungumzia tuhuma hizo za wizi, Detail alisema Drake alimuibia mdundo huo mwaka 2014 walipokuwa na makubaliano ya kufanya kazi pamoja lakini yakavunjika na kuanzia hapo amekuwa akimtaka rapa huyo asiutumie mdundo huo lakini yeye amekaidi.
“Nimemfikisha mahakamani Drake maana amekaidi makubaliano yetu baada ya kushindwa kufanya kazi pamoja. Kiukweli hakuwa mstaarabu na hili litakuwa fundisho kwa rapa wengine wenye tabia kama yake ambao wanafikiri mkono wa sheria hauwezi kuwagusa kwa vile tu wana majina makubwa,” alisema Detail.
Hata hivyo, Drake na Detail waliwahi kuwa na ugomvi mkubwa mwaka 2014 baada ya kushindwa kufanya kazi pamoja na kupigana huku chanzo haswa cha ugonvi wao kikiwa hakijawekwa wazi.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger