Friday 14 May 2021

SHEIKH MAKUSANYA : WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU TUWATII VIONGOZI WETU..UWE UNAWAPENDA AMA HUWAPENDI

...
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Makusanya akitoa hotuba kwenye Swala ya Eid El Fitri katika uwanja wa Sabasaba mjini Shinyanga
Waumini wa dini ya Kiislamu mkoani Shinyanga wakiwa kwenye Swala ya Eid
Waumini wa dini ya Kiislamu mkoani Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu na Sheikh wa Mkoa Ismail Makusanya watatu katikati
 **
Na Marco Maduhu, Shinyanga
Waumini wa dini ya Kiislamu hapa nchini, wametakiwa kuwatiii na kuwaheshimu viongozi wa kiserikali, akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.

Rai hiyo imetolewa leo Mei 14,2021 na Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Makusanya, wakati akitoa hotuba kwenye swala ya Eid El Fitr iliyofanyika katika viwanja vya sabasaba Mjini Shinyanga.

Alisema maagizo ya kutii viongozi yanatoka kwa Mwenyezi Mungu, hivyo ni vyema waumini hao wakafuata maagizo hayo, na kuwatiii viongozi wa nchi na kuwaheshimu, ili kujiongezea thawabu.

"Nawaomba waumini wa dini ya Kiislamu tuwatii viongozi wetu wa Serikali, uwe unawakubali ama kuwakataa, na hata kama huwapendi ama unawapenda, akiwamo Mkuu wetu wa Mkoa hapa Shinyanga Zainab Telack na kiongozi wetu wa nchi "Rais Samia",alisema Makusanya.

Pia aliwataka Waislamu kusheherekea Sikukuu ya Eid kwa kutoa sadaka wa yatima, wafungwa, wajane, pamoja na kufurahia na familia zao nyumbani na siyo kwenda kufanya mambo ya anasa.

Nao baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu akiwamo Twaha Habibu, alisema katika kusheherekea siku kuu hiyo ni vyema kila Muislamu akajiepusha na masuala ya anasa ikiwamo kunywa Pombe, ili kuepuka kuharibu mfungo wao kwa kuchuma dhambi.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger