Saturday 2 February 2019

DIWANI WA CHADEMA AWEKWA NDANI KWA AMRI YA RC KISA DHARAU KAKUNJA NNE KWENYE KIKAO


 Diwani wa Susuni (Chadema), Abiud Solomon amesimulia jinsi alivyoondolewa kwenye kikao na mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima na kuwekwa ndani kwa saa saba kisha kuachiwa akielezwa kuwa ana dharau kwa kuwa alikunja nne kikaoni.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumamosi Februari 2, 2019 amesema Malima alitoa agizo hilo kwa polisi kumweka ndani kwa madai kuwa ameonyesha dharau kwenye kikao cha kumtambulisha mkuu mpya wa wilaya ya Tarime, Charles Kabeho.

Katika tukio hilo lililotokea jana Ijumaa Februari Mosi, 2019, Solomon amesema kabla ya kuondolewa alihojiwa kuhusu wadhifa wake, “lakini nilishangaa kusikia agizo la kuniweka ndani kisa nimekunja nne kwenye kikao cha mkuu wa mkoa.”

“Niliwekwa ndani kuanzia saa saa 9 alasiri hadi saa 3 usiku baada ya viongozi wangu wa chama kufanya taratibu za kuniwekea dhamana wakafanikiwa kunitoa lakini nikatakiwa kurudi siku ya Jumatatu Februari 4.”

Ameongeza, “Tulikuwa na kikao cha kumkaribisha mkuu wa wilaya mpya, nilipata nafasi ya kukaa eneo la waandishi wa habari ili kuwapisha wapite, nililazimika kubebanisha miguu yangu (kukunja nne) ili kutoa nafasi ya wao kupita na kufanya kazi yao vizuri, ila ikachukuliwa kwamba namdharau mkuu wa mkoa.”
Via Mwananchi

Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Share:

MTOTO MWINGINE AUAWA NJOMBE


Mtoto wa miaka 10, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili, amekutwa ameuawa kikatili na mwili wake kutelekezwa kichakani eneo la Lupembe, wilayani Njombe.

 Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Renata Mzinga, amesema kuwa maiti hiyo iliokotwa karibu na nyumbani kwao na mtoto huyo, baada ya majirani kuanza kumtafuta mara tu baada ya kupata taarifa kutoka kwa wazazi wake kuwa mtoto wao haonekani.

“Mtoto alipotea tangu saa 12, lakini wazazi wake walianza kumtafuta majira ya saa nne ndo wakakuta ametupwa karibu tu na nyumbani kwao, baada ya mtoto kwenda kucheza kwa jirani ilipofika saa moja hajarudi, walienda kutoa taarifa kwa majirani na polisi, sasa wakaanza kutafuta mpaka wakakuta hiyo maiti, haikupita siku nzima, ni masaa machache sana”, amesema Kamanda Mzinga.

Matukio hayo ya watoto kuuawa yamekuwa yakitokea mara kwa mara mkoani Njombe na taarifa zake kufikishwa Bungeni, jambo ambalo Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amesema kwamba jeshi la Polisi linafanyia kazi kuweza kuwabaini wauaji.
Chanzo-EATV
Share:

ALIYEONDOLEWA JELA KWA MSAMAHA WA RAIS AKAMATWA NA SARE ZA JWTZ

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia aliyekuwa mfungwa katika Gereza la Segerea na kuachiwa kwa msamaha wa Rais mwaka jana, Emmanuel Magoti (18), kwa tuhuma za kukutwa na sare za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini humo, Kamishna wa Polisi, Lazaro Mambosasa alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Januari 30, mwaka huu, saa 8 mchana eneo la Mbagala. Alisema Polisi ilimkamata kijana huyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba amekuwa akijihusisha na makosa ya uhalifu ndani ya kanda hiyo huku akiwa amevaa sare za JWTZ.

“Lengo la mtuhumiwa huyu ni kujificha baada ya kutenda makosa hayo ili lawama ziwaendee wanajeshi hao. Tulivyopata taarifa hizo tulianza ufuatiliaji mara moja na kwa bahati tulimkamata na tulimkuta akiwa na sare hizo ambazo ni suruali mbili, koti moja na fulana,” alisema. Alieleza kuwa makachero wa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na askari polisi wa JWTZ (MP) walifika katika nyumba ya mtuhumiwa huyo na kukuta sare hizo.

Alifafanua kuwa katika mahojiano na mtuhumiwa huyo alikiri kujihusisha na matukio ya uhalifu akishirikiana na wenzake wawili ambao walifanikiwa kutoroka na kwamba wanaendelea kuwafuatilia. “Mtuhumiwa huyu alikiri kwamba alikuwa mfungwa katika gereza la Segerea kwa kosa la wizi na kwamba aliachiwa kwa msamaha wa Rais mwaka 2018.

Msako mkali unaendelea kuwatafuta wenzake wawili wanaoshirikiana nao katika matukio hayo,” alieleza. Mambosasa alitoa onyo kwa wafungwa wanaotoka magerezani kwa rufaa, msamaha wa rais au kumaliza vifungo, kuacha kujihusisha na matendo hayo kwa sababu wanakuta hali shwari lakini wanachochea mitandao ya uhalifu.

Alisisitiza kuwa lengo la msamaha ni kumfanya mtu aliyejutia arudi kwa jamii kuungana nao kufanya shughuli za jamii na kwamba wanachotegemea ni mabadiliko ya tabia wanapofanya mafunzo jela ili aweze kupata maarifa waweze kuishi kama raia wema wanaofuata sheria. Kwa mujibu wa Mambosasa, wafungwa wanaotoka gerezani na kuanzisha makundi ya uhalifu watambue kwamba jeshi hilo liko macho kwani wataendelea kufuatilia ili kuwalinda raia wema dhidi ya wahalifu.
Share:

WANNE WAUAWA TENA NJOMBE

Na Amiri kilagalila Mtoto mwingine anayekadiliwa kuwa na umri kati ya miaka 7-10 aliyefahamika kwa jina la RECHAEL MALEKELA mkazi wa kijiji cha Matebwe wilayani Njombe amekutwa ameuawa kwa kuchomwa na vitu vyenye ncha kali mita chache kutoka nyumbani kwao. Akithibitisha tukio hilo mkuu wa wilaya ya Njombe RUTH MSAFIRI alisema kuwa ni kweli mtoto huyo amekutwa amefariki na walizipata taarifa hizo usiku wa kuamkia leo. “Mtoto huyo amechomwa chomwa na vitu vyenye ncha kali nadhani mtoto huyu alikuwa peke yake akitoka kwa mama yake na kuelekea kwa kaka yake…

Source

Share:

BABA MZAZI AWAPACHIKA MIMBA MABINTI ZAKE WAWILI

 Baba wa mabinti wawili mjini Eldoret nchini Kenya anasakwa na maafisa wa polisi baada ya kuwabaka na kuwapachika mimba watoto hao kwa wakati tofauti.

Baba huyo anasemekana kuanza kuwabaka wanawe mwaka wa 2014 mama yao alipoaga dunia.

 Mshukiwa alikuwa amerejea nyumbani kutoka gerezani baada ya kukamatwa kwa kumbaka binti wake kitinda mimba.

 Kulingana na taarifa za Citizen TV, jamaa huyo alipofika nyumbani kwake, alimbaka tena bintiye mkubwa ambaye kwa sasa amempachika pia mimba. 

 Msichana huyo aliwambia wanahabari kuwa dadake mdogo alijitoa uhai mwaka wa 2018 akiwa na ujauzito wa miezi saba. 
Msichana huyo ambaye pia ni mjamzito, alisema aliwasilisha malalamishi yake kwa wazee wa kijiji ila hakuna hatua ambayo imechukuliwa dhidi ya baba yao

 Aliamua kuranda katika mitaa ya mji wa Eldoret ila wasamaria wema wajitokeza na kumpa makazi.

Wasichana hao wamekuwa wakiteseka mikononi mwa baba yao ambaye anapaswa kuwalinda tangu mama yao alipofariki mwaka wa 2014.

Share:

MWALIMU MKUU ATUPWA JELA KWA WIZI WA FEDHA ZA SHULE

Mwalimu Mkuu shule ya sekondari Mikwambe, Paulo Lorry, amehukumiwa kifungo cha miaka sita na kutakiwa kulipa Sh milioni 16 katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke alizoiba kutoka akaunti ya shule.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Taasisiya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Temeke, Pilly Mwakasege, ilieleza kuwa mwamu Lorry amekutwa na hatia na kuhukukiwa kwenda jela.

Ilieleza kuwa mwalimu huyo alishtakiwa na makosa matatu ya matumizi mabaya ya ofisi kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Mshitakiwa alikuwa ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mikwambe Manispaa ya Temeke mwaka 2010 alipokea Sh milioni 28 kupitia akaunti ya shule namba CA 2011100236 kwa ajili ya ujenzi wa maabara shuleni hapo.

Share:

LUGOLA AWATAKA VIJANA KUTUNZA WAZEE WAO..HAKUNA ATAKAYESALIMIKA MAUAJI YA WAZEE

Waziri Mambo ya Ndani Kangi Lugola ametoa wito kwa vijana wote nchini kuachana na tabia ya mauaji ya vikongwe na Wazee Nchini na kutoa onyo kwamba hakuna muuaji hata mmoja atakaye salimika na kukwepa mkono wa sheria.

Amesema hayo jana jijini Dodoma katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao kazi kilichowakutanisha wazee makamanda wa jeshi la polisi na maofisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa kujadiliana kwa pamoja kuhusu mbinu mpya za kutokomeza mauaji hayo kwa kutumia Mkakati mpya wa miaka 5 wa Kutokomeza Mauji ya Wazee na Vikongwe Nchini.

Mkakati huo uliozinduliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Tanzania tarehe 29, January 2019 wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Ustawi wa Jamii Nchini uliofanyika Jijini Dodoma.

Aidha Waziri Lugola amewataka vijana kutambua kuwa kijana wa leo ni Mzee wa Kesho hivyo atambue kuwa machungu ya mauaji ya wazee wanayoyapata leo naye ayatarajie baadae kwa kuwa kila mtu atazeeka.

Kufuatia hali hiyo Waziri Lugola aliwataka Vijana kutunza wazee wao kwasasababu machozi ya wazee wanayolia kila siku kwa kwa kukosa matunzo ya watoto wao yanapelekea wazee wengi kuwa na macho mekundu yanayoplekea watu wenye imani potofu kuwapoteza maisha yao kwa imani za kishirikina.

Aliongea kuhusu Mkakati wa Kutokomeza Mauaji ya Wazee Waziri Nchini Lugola alisema lengo la mkakati huu ni kuhakikisha tunashirikiana ili ifikapo mwaka 2023 mauaji ya wazee yawe yamekomeshwa kabisa.

”Hatutakua na sababu yoyote ya kueleza tukishindwa kutekeleza wajibu huu muhimu wa kulinda uhai wa kundi hili tete. Naomba muongeze kasi ili tufikie lengo hili, tena ikiwezekana mapema zaidi kwani tutapimwa kwalo 2023’’. Aliongeza Mhe. Lugola.

Alitoa wito kwa vyombo vya dola hasa Jeshi la polisi kuendelea kufuatilia kwa ukaribu sababu na vichocheo vya mauaji haya ikiwa ni pamoja na kuwabaini wahusika wanaopanga na kutekeleza mauaji haya ili wafikishwe kwenye vyombo vya Sheria, na pale inapothibika wahusika wachukuliwe hatua kali ili tukomesha kabisa vitendo hivi vya kikatili. 

Wakati huo huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu aliwaambia wajumbe wa Mkutano kuwa mahuaji ya vikongwe yalianza tangu miaka ya 1960 na serikali imekuwa ikipambana nayo lakini yamekuwa yakiendelea.

Dkt. Jingu aliongeza kuwa jughudi za serikali kupitia Jeshi la Polisi zimefanikiwa kupunguza mauaji haya lakini hayajakwisha kwasababu bado kuna watu wengi wenye Imani potofu katika Jamii hivyo ni lazima mapambano dhidi yao yaendelee.

Alisema kuwa Mkakati wa Kutokomeza Mauaji dhidi ya Wazee unalenga kuwa na Taifa linaloazingatia haki na ustawi wa wazee kwa kupiga vita imani za kushirikina, ubaguzi, ukatili na mauaji.

Aidha Dkt. Jingu aliongeza kuwa tafiti zilizopo zinaonesha mauaji na ukatili dhidi ya Wazee yanachochewa na Imani za kishirikina pamoja na migogoro ya ardhi hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau imeandaa Mkakati wa Kutokomeza Mauaji ya Wazee Nchini kwa lengo la kutokomeza kabisa mauaji haya.
Share:

TPDC YAIMARISHA SEKTA YA ELIMU MKOANI MTWARA


Bi. Marie Msellemu, Meneja Mawasiliano wa TPDC akimkabidhi hundi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh. Bw. Gelasius Byakanwa kiasi cha Tsh,. 13, 258,042 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa Mkoani Mtwara.
Meneja Mawasiliano wa TPDC Bi. Marie Msellemu akikabidhi hundi kwa mratibu wa tasisi ya TAKUWA Bi. Hadija Malibecha 
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mtwara Ndg.Omari Kipanga akitoa ufafanuzi wa mahitaji ya elimu mkoani Mtwara.
 ***
Katika jitihada za kutekeleza dhana ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kutekeleza kwa vitendo dhana hii kwa kushiriki katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo Mkoani Mtwara. 

Katika tukio la hivi karibuni, TPDC imeweza kumkabidhi Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Mh. Bw. Gelasius Byakanwa hundi ya kiasi cha shilingi milioni kumi na tatu laki mbili hamsini elfu na arobaini na mbili ili kusaidia ujenzi wa darasa moja katika halmashauri ya wilaya ya Mtwara. 

Akiongea katika tukio hilo, Mh. Byakanwa alisema TPDC imefanya jambo kubwa na kuonyesha uzalendo kwa kurudisha kwa jamii, na aliishukuru TPDC kwa kuendelea kushiriki katika kutatua changamoto mbalimbali mkoani Mtwara, husani zile zinazoikumba sekta ya huduma za jamii ikiwemo elimu. 

Vile vile mkuu wa mkoa alitoa rai kwa wadau na wawekezaji waliopo mkoani Mtwara kuiga mfano wa TPDC katika kuwajali wananchi kwa kuchangia katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Akimkabidhi mfano wa hundi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Bi. Marie Msellemu ambaye ni Meneja Mawasiliano wa Shirika alisema..

 “TPDC ni mdau mkubwa wa Mkoa wa Mtwara, na kwa kupitia mfuko wa uwajibikaji kwa jamii (CSR), TPDC imekuwa ikiwashika mkono wananchi wa Mkoa wa Mtwara na mikoa ya jirani katika kuboresha huduma za jamii kama vile elimu, afya, maji na hivyo kiasi hiki cha fedha kitauwezesha mkoa kuendelea kufikia lengo la kuweka mazingira mazuri ya kusomea kwa watoto wetu”. 

Wakati huo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Ndg. Omari Kipanga alieleza kuwa..

 “Sisi kama halmashauri tumefarijika sana kwa msaada huu uliotolewa na TPDC, kwani fedha hizi zitaelekezwa moja kwa moja katika ujenzi wa madarasa katika halmashauri ya Wilaya yetu kama ilivyokusudiwa. Mchango huu uliotolewa na TPDC unakwenda kukamilisha kazi ya kuezeka madarasa manne katika shule ya msingi Mitambo pamoja na madarasa mawili katika shule ya sekondari ya Madimba’’. 

Mkurugenzi Kipanga aliendelea kusisitiza kwamba uhitaji bado ni mkubwa kuweza kukamilisha uhitaji wa madarasa kwa Mkoa wa Mtwara na kuwataka wadau wa elimu na wawekezaji mbalimbali waliopo mkoani Mtwara kuiga mfano wa TPDC katika kurudisha kwa jamii na kuimarisha elimu mkoani hapo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Ndg. Evod Mmanda naye aliungana na viongozi waliotangulia kwa kuishukuru na kuipongeza TPDC kwa kusaidia kuboresha huduma mbali mbali za kijamii mkoani Mtwara. 

Alieleza kuwa...

 “Si mara ya kwanza kwa TPDC kuchangia kwani mwaka jana tumepokea kiasi cha 21,151,500 za kumalizia ujenzi wa zahanati ya kijjiji cha Mngoji pamoja na kiasi cha 12,000,000 za ujenzi wa choo cha wanafunzi wenye uhitaji maalumu katika shule ya msingi Shangani”. 

Katika hatua nyingine TPDC ilikabidhi Taasisi ya Kusaidia Wanawake Mkoani Mtwara (TAKUWA) kiasi cha milioni tatu laki tisa na elfu sabini kwa ajili ya unununuzi wa vitendea kazi vya ofisi ili kurahisisha shuguli za kila siku za taasisi hiyo. 

Mratibu wa taasiis hiyo Bi. Hadija Malibecha alishukuru TPDC kwa msaada huo na alieleza kuwa “kabla ya upatikanaji wa vifaa hivyo tulikua tunafanya kazi katika mazingira magumu lakini sasa TPDC imetuboreshea mazingira ya kazi na kazi zinaenda vizuri”. TAKUWA inasaidia vikundi vya wanawake kwa ajili ya kuinua shughuli mbalimbali za kiuchumi na elimu. 

Jumla ya vikundi 12 vya wakinamama mkoani mtwara vinasimamiwa na taasisi hii katika kupewa mafunzo ya ujasiriamali kama kutengeneza sabuni, ufugaji wa nyuki na ufugaji wa wa mbuzi lengo ikiwa ni kuboresha maisha ya wanawake.
Share:

WASANII WA FILAMU NCHINI WATAKIWA KUZINGATIA WELEDI NA UFANISI KWENYE KAZI ZAO


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Monica Kinala akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu wa mkoa wa Tanga
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fissoo akizungumza katika mafunzo hayo
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Mathew Bicco akizungumza katika mafunzo hayo 
Mwezeshaji wa Mada ya Uandishi wa Miswada ya Filamu Dkt. Richard Ndunguru kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu mkoani Tanga.
Msanii nguli wa Filamu mkoani Tanga akizungumza wakati wa mafunzo hayo kulia ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Monica Kinala
Sehemu ya wasanii wa filamu mkoani Tanga wakifuatilia mafunzo hayo 
Sehemu ya wasanii wa filamu mkoani Tanga wakiwa kwenye mafunzo hayo
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Monica Kinala katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo kulia ni KATIBU Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fissoo kushoto ni nKATIBU Mkuu wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Mathew Bicco. 


Wasanii wa filamu hapa nchini wametakiwa kuhakikisha wanazingatia waledi na ufanisi mkubwa kwenye kazi zao ili ziweze kuwa chachu ya maendeleo kwa jamii zinazowazunguka kutokana na tasnia hiyo hivi sasa kuwa mkombozi kwenye jamii.

Hayo yalisemwa na Mwezeshaji wa Mwezeshaji wa Mada ya Uandishi wa Miswada ya Filamu Dkt. Richard Ndunguru kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu mkoani Tanga.

Alisema sanaa inaweza kuwa tija kubwa ya maendeleo kwa wasanii kwa kutengeneza ajira nyingi na kuweza kuwakomboa iwapo wataizingatia na kuithamini kwa kuonyesha walezi kwenye kazi zao.

“Ndugu zangu wasanii labda niwaambie kwamba mkiwa makini kwenye kazi zenu na kuzingatia weledi mkubwa mnaweza kufika mbali kimafanikio kutokana na namna tasnia ya filamu hapa nchini iliyokuwa”,alisema.

Aidha alisema pia wasanii lazima watambue kwamba hawawezi kutengeneza filamu nzuri kama hawatakuwa na muda wa kutazama wenzao wanafanya nini kwani kupitia wenzao wanaweza kujifunza na kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa”,alisema.

“Labda pia niwaambie kwamba waledi kwenye kazi ya sanaa ni kitu muhimu sana inaweza kukupa maendelea makubwa kwa kuhakikisha mnaipenda na kuithamini",alisema.

Naye Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Joyce Fissoo alisema sekta ya filamu ni ya kiuchumi kutoka Tanzania ni ya pili kwa idadi uzalishaji ukilinganisha na nchi ya Nigeria lakini ukija kwenye pato la taifa kidogo wanahitaji kuongeza nguvu.

Alisema bodi ya filamu imeweka mpango mahususi wa kuwajengea uwezo wadau wa filamu hapa nchini hususani kwenye maeneo ya kuboresha kazi zao ili ziwe kuwa na tija.

Aidha alisema hilo linatokana na baadhi ya wasanii hususani wanaochipukia kutokutambua namna ya kuweza kutengeneza kazi zao na kuweza kuzitangaza ili ziweze kuwa na manufaa makubwa kwao.

Share:

KAGAME ATEULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI - EAC

Rais wa Rwanda, Paul Kagame ameteuliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Rais Kagame amechukuwa nafasi ya Rais wa Uganda, Yoweri Museveni aliyemaliza muda wake.

Akizungumza Ijumaa Februari Mosi, 2019 jioni baada ya kutangazwa kwake katika mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya hiyo unaofanyika jijini Arusha nchini Tanzania, Kagame amesema ataitumikia vyema jumuiya hiyo.
Share:

Friday 1 February 2019

Video Mpya : CHIEF MAKER - BHOKE...NGOMA KALI UTATA WA BINTI WA KIKURYA


Msanii Chief Maker anakualika kutazama video yake mpya kuhusu Binti wa Kikurya inaitwa Bhoke..Bonge moja la ngoma mtu wangu..Itazame hapa chini
Share:

WAWILI WAFARIKI,WATANO HOI BAADA YA KUBUGIA DAWA ZA MITI SHAMBA


Watu wawili wamefariki dunia huku wengine watano wakilazwa hospitalini baada kunywa dawa za miti shamba mtaani Karen jijini Nairobi nchini Kenya. 

Watu hao saba wanasemekana kunywa dawa hizo walipokuwa wakifanya kazi ya ujenzi wa jengo eneo la Kazuri kule Marula Alhamisi Januari 31,2019.

 Waathiriwa walikimbiziwa hospitalini baada ya kulalamika kuhusu maumivu makali kwenye tumbo na kutapika. 

Kulingana na taarifa za polisi, mmoja wa waathiriwa aliaga dunia alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Karen na mwingine alifariki akiwa katika zahanati ya St. Odillas. 

Waathiriwa wanasemekana kalalama kuhusu maumivu makali kwenye tumbo na kutapika wakati walipofikishwa hospitalini. 

Manusura 5 walipelekwa katika hospitali ya St. Mary's ambapo wanapokea matibabu.

"Uchunguzi ulionyesha kuwa walikunywa dawa za miti shamba wakiwa kazini wakifanya ujenzi eneo la Kazuri, maafisa wa polisi walifika eneo la tukio na wakapata jagi iliyokuwa na matawi ya mmea wa Aloe Vera," taarifa ya polisi ilisoma.

Miili ya wawili hao ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhi wafu cha Umash huku maafisa wa polisi wakiendelea na uchunguzi kubaini aliyewapatia dawa hizo.

Via Tuko
Share:

MCHUNGAJI KKKT ATUHUMIWA KUFANYA MAPENZI NA MTOTO WA MCHUNGAJI MWENZAKE

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT Dayosisi ya Iringa kumuondoa na kutomfumbia macho aliyekuwa Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi hiyo mchungaji Yusto Kinyori kwa tuhuma za kufanya mapenzi na mtoto wa mchungaji mwenzake kwenye gari. Kasesela amesema hayo kwenye Mkutano Mkuu wa kumchagua Msaidizi wa Askofu wa kanisa hilo uliofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT usharika wa Ipogolo ambapo amesema kuwa anayo video clip ikionesha mchungaji huyo akifanya mapenzi kwenye gari na mtoto wa mchungaji mwenzake. Kasesela…

Source

Share:

Ministry of Education, Science and Technology: China Scholarships 2019

Ministry of Education, Science and Technology:: Scholarship tenable in people’s republic of china for the academic year 2019/2020

  1.  Call for Application

The General Public is hereby informed that, the Chinese Government has opened new scholarships for Undergraduate, scholars and Post-graduates to Tanzanians for the academic year 2019/2020. The online application and the corresponding application documents should be submitted to application receiving agency. For more information, please visit the following link: http://www.csc.edu.cn/studyinchina or http://www.compuschina.org

Eligibility:

To be eligible, applicants must:

  • Be a citizen of the United Republic of Tanzania;
  • Be in good health;
  • Be a high school graduate under the age of 25 when applying for Bachelor degrees programs;
  • Be a Bachelor’s degree holder under the age of 35 when applying for Master’s programs;
  • Be a Master’s degree holder under the age of 40 when applying for Doctoral programs;

2.0 Application Documents

a) Completely filled application form for Chinese Government Scholarship (in Chinese or English);

b) Certified copies of Certificate for Secondary Education Examination (CSEE), Advanced Certificate for Secondary Education Examination, Diploma, Bachelor`s Degree and Master`s Degree. Documents in languages other than Chinese or English must be attached with certified Chinese or English translations;

c) Academic transcripts: Transcripts in languages other than Chinese or English must be attached with certified Chinese or English translations;

d) A Study Plan or Research Proposal in Chinese or English. (A minimum of 200 words for undergraduates, and 800 words for postgraduates);

e) Recommendation letters: Applicants for graduate programs or senior scholar programs must submit two letters of recommendation in Chinese or English from professors or associate professors;

f) Certified copies of birth certificates

g) Applicants for music studies are requested to submit their own works and those applying for fine arts programs must submit their own works which include two sketches, two colour paintings and two other works;

h) Applicants with good Bachelor’s degree in Mechanical and/or Electronics Engineering can apply for Masters’ programme which are offered at Tianjin University of Technology and Education;

j) Applicants under the age of 18 should submit the valid documents of their legal guardians in China; and

i) Applicants planning to stay in China for more than 6 months must submit a photocopy of the Foreigner Physical Examination Form completed in English (the original copy should be kept by the applicant). The form designed by the Chinese quarantine authority can be downloaded from http://my.china-embassy.org/eng/whjy/P020190109380893894433.pdf The physical examinations must cover all the items listed in the Foreigner Physical Examination Form. Incomplete records or those without the signature of the attending physician, the official stamp of the hospital or a scaled photograph of the applicants are invalid. Please select the appropriate time to take physical examination as the result is valid for only 6 months.

3.0 Please submit the following documents where applicable

k) Pre-admission Letter from Chinese Government Scholarship universities; and

l) Language qualification certificate. E.g., HSK certificates, IELTS or TOFEL report.

Instruction for online application of the Chinese government scholarship information system

Step 1: Visit http://www.csc.edu.cn/laihua or www.capuschina.org and click “Scholarship Application Online for International Students”;

Step 2: Read “Tips for online application” carefully before clicking “NEXT” to the registration page;

Step 3: Log in with your user name and password. For new user, please click “Create an account” for registration;

Step 4: Fill in the correct Program Category and Agency Number. An Agency Number represents a specific application receiving agency and a correct choice of Program Category is necessary before filling in the Agency Number. Please make sure you fill it in correctly, otherwise you will not be able to continue your online application or your application will not be accepted. Your ‘Program Category’ is: Type A and Agency Number is: 8341. Once the correct ‘Agency Number’ is entered, the name of the agency will automatically emerge;

Step 5: Fill in the Online Application Form and Upload Supporting Documents truly, correctly and completely following the steps listed on the left of the page. Applicants are required to select a discipline before choosing their majors. Please refer to the Disciplines Index, which could be downloaded from help, if you have any doubt about the disciplines and majors;

Step 6: Check each part of your Application carefully before submitting it. Click Submit to submit your Application. The submitted documents will be the only reference for the applied universities to confirm the admission;

Step 7: You can make changes to your application by clicking Withdraw and Edit the Application on the top of the page. But make sure to submit it again by 4 clicking Submit after finishing all the changes. Otherwise, the retrieved application will become invalid and your new application will not be received either;

Step 8: You can download and print the completed Application Form by clicking Print the Application Form; and

Step 9: Send the printed paper application form and other supporting documents to the address below.

Note: Please use Firefox or Internet Explorer 11.0. Menu selection functions may not work in other browsers.

Kindly submit your application to the undersigned not later than 11th March, 2019.

Issued by:

Permanent Secretary,

Ministry of Education, Science and Technology,

College of Business and Law,

University of Dodoma,

P. O. Box. 10,

40479 DODOMA.

The post Ministry of Education, Science and Technology: China Scholarships 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

BILIONI 50.4 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO BUKOBA KWA MWAKA 2019/2020

Na Allawi Kaboyo Bukoba. Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya Bukoba mkoani Kagera, limepitisha bajeti ya zaidi ya shilling bilioni 50.4 kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2019-2020. Akisoma rasimu ya bajeti hiyo katika baraza la madiwani lililofanyika Januari 31 mwaka huu katika ukumbi wa halmashauri hiyo, afisa mipango wa halmashauri ya wilaya Bukoba JULIAN TARIMO ameeleza vipaumbele vilivyolengwa kuwa ni afya elimu maji na miundombinu pamoja na mambo mengine na kuwataka madiwani hao kuipitisha bajeti hiyo kwa kuwa inalenga maslahi…

Source

Share:

WATENDAJI WAPEWA ONYO KALI UGAWAJI VITAMBULISHO AWAMU YA PILI KAGERA

Na mwandishi wetu Kagera Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti amegawa vitambulisho 35,000 awamu ya pili kwa Wafanyabiashara Wadogo katika Mkoa wa Kagera na kuwaagiza Watendaji wa Serikali chini ya usimamizi wa Wakuu wa Wilaya kuendelea na zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo na kuhakikisha ifikapo Februari 28, 2019 vitambulisho vyote viwe vimegawiwa kwa Wafanyabiashara Wadogo. Katika zoezi fupi la kukabidhi vitambulisho hivyo 35,000 vya awamu ya pili kwa Wakuu wa Wilaya iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Februari 1, 2019 Mkuu wa…

Source

Share:

MWANANCHI YEYOTE ATAKAYEUWAWA NINAANZA KUSHUGHULIKA NA MWENYEKITI WA MTAA HUO-OLESENDEKA

Na Amiri kilagalila Mkuu wa mkoa wa Njombe CHRISTOPHER OLESENDEKA amewaagiza viongozi wa serikali za mitaa wakiwemo wenyeviti wa vijiji kuhakikisha wanashiriki katika zoezi la kutoa taarifa za wahusika wa mauaji mkoani Njombe huku akiapa kuanza kushughulika na viongozi hao wa vijiji endapo yatatokea mauaji yanayofanana na yaliyotokea mkoani humo. OLESENDEKA alitoa maagizo hayo hii leo katika viwanja vya polisi mjini makambako wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa mji huo kwa lengo la kuwaomba wananchi kuonyesha ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama katika kushiriki kuwafichua wanaohusika katika mauaji…

Source

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger