Monday 15 April 2024

UWT IBADAKULI WAFANYA KONGAMANO LA MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA MADARAKANI NA KUMPONGEZA KUFANYA KAZI KUBWA YA KUWALETEA MAENDELEO WATANZANIA

...

 


Na Marco Maduhu,SHINYANGA

UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga umefanya Kongamano la Miaka Mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan Madarakani, kwa kumpongeza kutokana na kazi kubwa ambayo ameifanya ya kuwaletea Maendeleo Watanzania.

Kongamano hilo limefanyika leo Aprili 13, 2024 katika Viwanja vya Shule ya Msingi Viwandani, ambalo lilitanguliwa na Maandamano,huku Mgeni Rasmi akiwa ni Katibu Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu, akimwakilisha Katibu wa CCM wa Mkoa huo Odilia Batimayo,Kongamano lililoandaliwa na Diwani wa Vitimaalum Tarafa ya Ibadakuli Mhe. Zuhura Waziri.
Ndulu akizungumza kwenye Kongamano hilo la UWT Tarafa ya Ibadakuli, amesema wanawake wanampongeza Rais Samia kwa kuwaheshimisha, kutokana na kazi kubwa ambayo ameifanya ya kuwatumikia Watanzania ndani ya Miaka Mitatu na kuwaletea Maendeleo.

Amesema Rais Samia aliichukua nchi kwenye kipindi kigumu cha kuondokewa na Hayati Rais John Magufuli, huku baadhi ya wananchi wakishindwa kumwamini kama ataweza kuongoza Nchi, lakini ndani ya miaka mitatu amewafuta machozi Watanzania na kuwaletea mapinduzi makubwa ya kimaendeleo, na kuonyesha kwamba wanawake wanaweza kushika nyazifa kubwa za uongozi.
“Ndani ya miaka mitatu Rais Samia ameleta mapinduzi makubwa ya kimaendeleo katika Sekta mbalimbali ikiwamo ya Afya, Elimu, Nishati na sasa hivi kuna Umeme kila kona hadi vijijini, Barabara zimejengwa, Maji yametapakaa kila mahali na kumtua ndoo kichwani Mwanamke,” amesema Ndulu.

Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Rehema Nhamanilo,amewataka wanawake kote nchini kwamba zawadi kubwa ambayo watampatia Rais Samia ni kumpigia kura nyingi za ushindi 2025, pamoja na kuwapigia kura wagombea wote wa CCM kuanzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu hadi uchaguzi Mkuu mwakani.
Naye Diwani wa Vitimaalum Tarafa ya Ibadakuli Zuhura Waziri, amesema ameandaa Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia kwa kushirikiana na viongozi wa UWT Kata ya Ibadakuli, kutokana na kazi kubwa ambayo wameifanya ya kuwaletea Maendeleo Watanzania ikiwamo Kata hiyo ya Ibadakuli.

Amesema hawana budi kumpongeza Mwanamke mwezao ambaye amekuwa chachu ya wanawake wengi kuaminiwa na kupata nafasi mbalimbali za uongozi na kufanya mambo makubwa, huku wakimwahidi kwamba katika Tarafa hiyo ya Ibadakuli wagombea wote wa CCM katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa watapata ushindi mkubwa, pamoja na uchaguzi Mkuu mwakani.
Aidha, amewataka pia wanawake wenye sifa za uongozi kwamba wajitokeze kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa Serikali mwaka huu,ili washike nyazifa hizo na kuingia kwenye vikao vya maamuzi pamoja na kuwaletea maendeleo wananchi.

Katika hatua nyingine Zuhura amewataka wanawake waendelee kupendana na pale wanapokwaruzana wasameheane, huku akiwakumbusha pia wasisahau malezi bora ya wototo wao wa jinsi zote wa kike na wakiume, pamoja na kuwapatia elimu kwa sawa.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu akizungumza kwenye Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia kufikisha miaka mitatu Madarakani na kuwaletea Maendeleo Watanzania.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu akiendelea kuzungumza kwenye Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia kufikisha miaka mitatu Madarakani na kuwaletea Maendeleo Watanzania.
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Rehema Nhamanilo akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Katibu wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Sharifa Mdee akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Ibadakuli Ester Komba akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kolandoto Zinila Kalwani akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Diwani wa Kitangili Mariamu Nyangaka akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Diwani wa Vitimaalum Tarafa ya Ibadakuli Zuhura Waziri akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu, akimpongeza Diwani wa Tarafa ya Ibadakuli Zuhura Waziri kutokana na kuandaa Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia pamoja na ujumbe Mzuri alioutoa.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano hilo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano hilo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Kongamano likiendelea.
Kongamano likiendelea.
Wanawake wakiendelea na Kongamano.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Awali Mgeni Rasmi Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu akiwasili kwenye Kongamano hilo.
Wanawake wakiwa katika Maandamano kuelekea kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia.
Wanawake wakiwa katika Maandamano kuelekea kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia.
Wanawake wakiwa katika Maandamano kuelekea kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger