Friday 7 August 2020

Vyama viwili vya upinzani nchini Uganda Vyagombania Rangi Nyekundu

...
Vyama viwili vya upinzani nchini Uganda vimeingia katika mzozo juu ya haki ya kutumia rangi nyekundu huku kila chama kikidai kuwa kina haki ya kuitumia rangi hiyo kama utambulisho wake.

Chama kikongwe cha UPC kinadai kuwa chama kipya cha NUP kinachoongozwa na msanii maarufu kama Bobi Wine kilikosea kuanza kutumia rangi ambayo imekuwa yao kwa miaka mingi.

Lakini NUP imekanusha madai hayo ikisema imetumia rangi hiyo ikiwa vuguvugu la 'People Power' na hakuna aliyejitokeza kupinga hadi pale waliposajiliwa kama chama.

Rais wa chama cha UPC Jime Akena ambaye ni mtoto wa mwasisi wa chama hicho Milton Obote anasema rangi nyekundu ni ya UPC tangu miaka 60.

Hata hivyo, Tume ya uchaguzi ndiyo itatoa maamuzi ya mwisho kati ya vyama hivyo viwili ni kipi kina haki ya kutumia rangi nyekundu katika nembo yao kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2021.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger