Sunday, 20 October 2019

RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKUU WA WILAYA NA MKURUGENZI WA HALMASHAURI

...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwe Rukia Muwango, pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya hiyo Bakari Mohamed Bakari, ambaye nafasi yake imechukuliwa na Hassan Abbas Rungwa.

Taarifa hiyo imetolewa Oktoba 19, 2019, na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, ambapo nafasi ya Mkuu wa Wilaya imechukuliwa na Hashim Abdallah Komba.

Uteuzi mwingine ambao umefanywa na Rais Magufuli leo ni wa Godfrey Mweli, ambaye amekuwa Naibu katibu mkuu TAMISEMI, akichukua nafasi ya Mathias Kabunduguru ambaye amekuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amemteua Mathias Kabunduguru, kuwa mtendaji mkuu wa Mahakama ya Tanzania, akichukua nafasi ya Hussein Katanga ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger