Friday, 18 October 2019

BASI LA FREYS COACH LAUNGUA MOTO

...

Na Josephine Charles - Malunde 1 blog
Basi la Freys Coach lenye namba za usajili T119BDY Gari la Freys  Coachla linalofanya safari zake kutoka Shinyanga kwenda  Tanga limeungua moto katika  eneo la Mhizi Usanda Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga barabara ya Tabora - Shinyanga.


Tukio hilo limetokea leo Ijumaa Oktoba 18,2019 majira ya saa 12 na nusu baada ya kutoka Shinyanga Mjini kuelekea Tanga.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio wanasema basi hilo limeungua matairi mawili ya nyuma upande wa kulia na kwamba hakuna madhara yaliyojitokeza kwa abiria walishuka na kuanza zoezi la kuzima moto huo kwa maji na mchanga na muda mfupi Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilifika eneo la tukio na kufanikisha kuzima moto huo.

"Tumezima kwa maji na mchanga,zimamoto nao wamefika,gari limezima,hakuna uharibifu wala majeruhi,gari halijateketea,abiria tumefanya juhudi za kuzima,tunasubiri magari mengine kutoka Mwanza ili tuendelee na safari",wamesema abiria wakizungumza na Malunde 1 blog .

Muonekano wa basi la Freys Coach baada ya kuungua leo. Picha zote na Josephine Charles - Malunde 1 blog
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger