Friday 22 July 2016

SECOND SELECTION KIDATO CHA TANO 2016,KUTANGAZWA MDA WOWOTE

...

Waziri wa TAMISEMI amesema kwamba awamu ya pili inasubiri nafasi zitakazojitokeza kutokana na wanafunzi watakao acha kuripoti kwa kupelekwa na wazazi wao kwenye shule binafsi au vyuo binafsi na vya serikali.
Pia Mheshimiwa Simbachawene aliziagiza mamlaka zinazohusika na kuwapokea wanafunzi wapya wa kidato cha tano kuhakikisha kuwa miundombinu yote muhimu inakamilika ikiwemo mabweni, madarasa vyoo na Maabara, samani (vitanda, Meza na Viti huduma za Maji na Umeme zinatekelezwa na kukamilika kwa wakati.
Katika mwaka 2016 jumla ya shule mpya za kidato cha tano 50 zimeanzishwa kutokana na maombi ya mikoa kwenye maeneo yao ili kuendana na lengo la Serikali la kuongeza Shule za Kidato cha Tano na Sita.
Hivyo, Waziri Simbachawene amewataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa shule zote zina walimu na vitabu vya kujifunzia na kufundishia na pia kuhakikisha chakula kwa wanafunzi wa bweni kinaandalaiwa kabla wanafunzi wapya wa kidato cha tano hawajaripoti.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger