Sunday 31 December 2023

WAKAZI KAWE WALIA NA UKABAJI NYAKATI ZA JIONI

...

 

......................

Na Mwandishi Wetu

Wakazi wa mtaa wa Kawe Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam, wameliomba Jeshi la Polisi nchini kuongeza ulinzi hasa nyakati za jioni eneo la Tanganyika pekazi kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukabaji na unyanganyi kwa kutumia silaha husani za jadi unafanywa na vijana wanajitambulisha kama Ulinzi Shirikishi kabla ya kumuibia mhusika.

Wamedai kuwa ukikutana nao hujitambusha kama watu wa usalama na baada ya hapo hutekeleza uovu huo kwa kukutolea mapanga,Visu,Nondo, na kumuibia muhusika.

Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti, baadhi ya wakazi wa mtaa huo ambao wawili walikataa kutotajwa kwa majina, wamedai kuwa kumekuwepo kwa vitendo hivyo katika eneo hilo ambalo ni karibu zaidi na kituo Cha Polisi Kawe.

Wamedai hivi karibuni mmoja wa Askari wa Jeshi anadaiwa kukabwa akiwa na mpenzi wake katika eneo hilo jambo ambalo linaongeza wasiwasi miongoni mwao.

Williams Nashoni ni mmoja wa mkazi wa mtaa huo amesema kuwa kumekuwepo kwa vitendo hivyo kwa kiasi kubwa japo hivi karibuni vimepungua kutokana na baadhi ya walinzi wa mchungaji Mwamposa kuongeza walinzi hata hivyo akidai bado jitihada zinatakiwa kuongezwa kutokana na walinzi hao kutokuthi mahitaji .

Nashoni amesema kinachowaumiza ni vitendo hivyo kutokea eneo ambalo si mbali na kituo cha Polisi Kawe huku akiwaomba wahusika kujitathimini.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Acp, Mtatiro Kitinkwi amesema kuwa wamejipanga kuendeleza kudumisha ulinzi na usalama eneo nzima la mkoa wa kipolisi ikiwemo Kawe na Tanganyika Pekazi.

Amedai kuwa kuelekea Mwisho wa mwaka Kuna tukio la mkesha Tanganyika pekazi na wao kama Jeshi wamejipanga kuongeza ulinzi na usalama ili kuhakikisha hakuna vitendo viovu havijitokezi hata kwa bahati mbaya.

Amesema kuwa taarifa zote za uhalifu wanazipokea na watahakikisha wanazifanyia kazi ili kuhakikisha ulinzi na usalama kwa raia unaimarika zaidi.

Amewaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa zote za uhalifu katika mkoa huo ili kuwarahisishia kazi na kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger