Tuesday 19 December 2023

MWENYEKITI WA BODI YA EWURA AKAGUA MIUNDOMBINU YA MAMLAKA YA MAJI TUKUYU

...

Mhandisi Barnabas Konga ( kushoto) kutoka Mamlaka ya Maji Mbeya, akimweleza Mwenyekiti wa Bodi ya EWURA, Prof Mark Mwandosya( aliyeketi kulia) kuhusu maendeleo ya mradi wa maji Mbaka, wakati kiongozi huyo alipotembelea chanzo cha maji cha Mto Mbaka, 18 Desemba 2023. Mamlaka ya Maji Mbeya, ndiye msimamizi wa mradi huo.

.............

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA, Prof Mark Mwandosya, amefanya ziara ya kikazi katika Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira ya Mji wa Tukuyu ( Tukuyu WSSA), Jumatatu, 18 Desemba 2023 kwa lengo la kukagua miundombinu ya maji na kufuatilia utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji Mbaka, wenye thamani ya bilioni 4.5 uliopo Kitongoji cha Mbaka juu, Kijiji cha Isebe, Kata ya Itagata, Tukuyu, Rungwe.

Mradi huo, unatajiwa kuimarisha huduma ya maji kwa asilimia 95 na kuongeza upatikanaji wa maji katika mji wa Tukuyu, ambapo kwa sasa huduma inapatikana kwa saa 13 tu kwa siku.

EWURA husimamia utendaji wa mamlaka za maji nchini ili kuhakikisha huduma zake zinakidhi ubora, kanuni za afya, utunzaji wa mazingira na zinapatikana kwa uhakika na kwa gharama nafuu.


Mhandisi Barnabas Konga ( kushoto) kutoka Mamlaka ya Maji Mbeya, akimweleza Mwenyekiti wa Bodi ya EWURA, Prof Mark Mwandosya( aliyeketi kulia) kuhusu maendeleo ya mradi wa maji Mbaka, wakati kiongozi huyo alipotembelea chanzo cha maji cha Mto Mbaka, 18 Desemba 2023. Mamlaka ya Maji Mbeya, ndiye msimamizi wa mradi huo.


Mwenyekiti wa Bodi, Prof. Mark Mwandosya ( mwenye mkongojo) katika picha ya pamoja na watendaji wa EWURA, Mamlaka ya Maji Tukuyu na Mamlaka ya Maji Mbeya, katika chanzo cha maji Mbaka, wakati wa ziara ya kikazi ya kufuatilia na kutathmini utendaji wa Mamlaka ya Maji Tukuyu na maendeleo ya mradi wa maji Mbaka.


Mwenyekiti wa Bodi ya EWURA, Prof Mark Mwandosya akiwa amesimama mbele ya chanzo cha maji Mbaka, kinachotumika kuhudumia mradi wa maji Mbaka, uliopo chini ya Mamlaka ya maji ya mji wa Tukuyu, alipotembelea mradi huo, 18 Desemba 2023, kufuatilia utekelezaji wake.


Mweyekiti wa Bodi ya EWURA, Prof. Mark Mwandosya ( kushoto) akiwa na Mhandisi Mwandamizi wa Maji EWURA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Dickson Semkuyu ( katikati) na Mha. Barnabas Konga ( kushoto) kutoka Mamlaka ya Maji Mbeya , katika bonde la Mto Mbaka, ambapo ni chanzo cha maji cha Mradi wa Maji Mbaka, kijiji cha Isebe, kitongoji cha Mbaka Juu, Tukuyu, wakati wa ziara ya kikazi ya watendaji hao kufuatilia maendeleo ya mradi huo, 18 Desemba 2023.


Mwenyekiti wa Bodi ya EWURA, Prof Mark Mwandosya ( aliyeketi) akisisitiza jambo kwa watendaji EWURA, Mamlaka ya Maji Mbeya na Tukuyu, wakati wa ziara ya kikazi kijijini Isebe, kata ya Itagata, Mbaka Juu, 18 Desemba 2023; kilipo chanzo cha maji cha mto Mbaka kitakachohudumia mradi wa maji wa Mbaka, wenye thamani ya bilioni 4.5, unaotekelezwa na Serikali ya Awamu ya sita, ili kuimarisha huduma ya maji kufikia asiliamia 95, katika mji wa Tukuyu.


Chanzo cha Maji cha Mto Mbaka, nje ya kidogo ya mji wa Tukuyu, katika kitongoji cha Mbaka Juu, kijiji cha Ibese, kata ya Itagata, kitakachohudumia mradi wa maji Mbaka.


Chanzo cha Maji cha Mto Mbaka, kilichopo kitongoji cha Mbaka Juu, Kijiji cha Isebe, kata ya Itagata, nje kidogo ya mji wa Tukuyu. Chanzo hicho kitahudumia mradi wa maji wa Mbaka, unaotekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kuimarisha huduma ya maji katika mji wa Tukuyu na maeneo ya jurani.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger