Sunday 31 December 2023

MWAKA 2024 PUNGUZA MAZOEA NA WATU ULINDE HESHIMA YAKO

...
 
Mwaka 2024 Punguza Mazowea na Watu Ulinde Heshima Yako!


Denis Mpagaze
_______________________

Usiruhusu watu wakuzoee sana, wakikuzoea watakuona wa kawaida, wakikuona wa kawaida watakudharau, wakikudharau, watakuharibia.

Siku zote anayekuharibia ni aliyekuzowea, anayekujua sana, anakuona wa kawaida sanaa, hakuogopi! Anakumudu!

Asipokuogopa hataona uzuri wako, akiukosa uzuri wako atashughulika na madhaifu yao, atayasambaza kwa watu wakuone mtu wa hovyo!

Akifanya hivyo umekwisha; wengi wameumia sana kwa sababu walikubali kuzoeleka, walikubali kuwa cheap.

Usiwe hivyo. Jitahidi kuwa adimu, siyo kila mtu anakuita ita kama mafungu ya nyanya na viazi sokoni na wewe unaitika na kwenda. Utaharibu!

Be adimuπŸ˜„πŸ˜„. Vitu vya thamani viko adimu. Havionekani kirahisi. Vimejificha! Vinavyoonekana kirahisi ni vile cheap!

Mungu ameendelea kutukuzwa na kuheshimika kwa sababu haonekani. Amejikalia zake Mbinguni. Hakuna anayejua hata sura yake. 

Angekuwa anatembea mitaani, tunakutana naye kila siku, anapanda na daladala kabisa tusingempa hiyo heshima. 

Alituletea Yesu tukamzowea, tukamuona wa kawaida, tukamdharau mpaka tukamuua. Binadamu ni wema wasipokuzowea. Ni hatari wakikuzowea.

Hata Mungu nakwambia siku akija hapa duniani tukamzowea kuna watu watafanya majaribio ya kumuua!πŸ˜„πŸ˜„ Hakuna kiumbe hatari kama binadamu. 

Kitu chochote kinachopatikana kwa nadra kinathamani kubwa. Madini yanapatikana kwa nadra sana na yapo ardhini.

Kaa mbali na nguru mbili. Ukikaa mbali heshima inakuja. Jitahidi kuwa mtu wa kutopatikana kirahisi.

Ikitokea mtu amekutana na wewe basi iwe ni kwa mambo ya msingi sana. Siyo unaitwa oi, umeishaitika na kuondokaπŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„.

Wazungu wanasema keep distance. Jitahidi kutopatikana popote wakati wote na kwa watu wote. 

Distance ndiyo inatengeneza hadhi ya mtu, usiwe mtu wa kujumuika na watu hovyo hovyo. Angalia kama kuna tija ya kujumuika. Kama ipo nenda, haipo acha! 

Ukiwa mbali na mtu ni rahisi kumpenda na kumfurahia na kuwa na kiu naye zaidi, hata dharau na machukizo hutaviona.

Mama yetu alipenda kusema mkitaka kupendana na kuheshimiana msiishi kwa ndugu zenu, na mkienda kutembea kaeni siku chache, ondokeni.

Ukiwa mtu wa kukeep distance watu watakwambia una nyodo, lakini  ndo ukweli. 

Katika kitabu cha Robert Green "The 48 Laws of Power" by Robert Greene, sheria ya 16 inasema use absence to increase respect and honour.

_"Too much circulation makes the price go down: The more you are seen and heard from, the more common you appear. Create value through scarcity._"

Hata bidhaa zikiwa nyingi sokoni zinashuka bei. Zikiadimika bei inapanda. Bora kujiweka mbali kidogo. Acha wakuone unaringa kikubwa wakuheshimu. 

Kuna watu mahusiano yenu yaishie kwenye salamu tu, mengine kuhusu wewe wasijue. 

Ikiwezekana wasijue unakoishi, wasijue familia yako, wasijue elimu yako, wasijue kazi yako, wasijue miradi yako, wasijue mkeo, wasijue mume wako.

Wakijua watakuzowea, wakikuzowea siku ukanunua hata gari watakununia na wakati gari lenyewe la mkopo, hawajui kama una maumivu ya kulipa mkopo.

Watakununia kisa umehamia kwenye nyumba yako, watakuchukia kisa umepanda cheo, ukizubaa wanakuua kabisa. Waulize wapanda vyeo mazonge wanayokutana nao!

Usiwaonyeshe watu ng'ombe anayekupa maziwa, watampa mifuko ya plastiki afe ukose maziwa, uteseke!πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„

Kutokuwa na mazoea mazoea na watu kunaeshimisha sana. Lazima ujiwekee mipaka. Mazoea husababisha kukoseana heshima.

Mtu akizoea biashara yako hatakulipa. Atakuwa mtu wa kukopa na kuchelewa kulipa. Wakati mwingine atataka umpe bure.

Hizi lugha za huyu ni mtu wangu hapana. Heshima kwanza.

Usipende kila mtu ajue unaishije hapa mjini ndo maana wahenga wakasema siri ya mtungi aijuae kata.

Mazoea ni mazuri kwa watu yanaleta ukaribu ila ni mabaya kuliko unavyoyafikiria. Hii ni ngumu kumeza ila ndo umeze tu.

Watu wakikuzoea sana wataanza kukuomba hela bila adabu. Wasipokuzowea hawakuombi. Wataishia kusema siwezi kumuomba yule baba kwa sababu sijamzoea. Good!

Watu wakikuzoea sana wataingia ndani kwako bila kupiga hodi na kwenda kula vitu kwenye friji. Hapo wanakusababishia mtikisiko wa bajeti hasa kama unatoka katika jamii zetu za kula kwa manati! 

Mazoea ni chanzo cha migogoro mingi. Waliozoeana ndiyo wagombanao. Mazoea ni fimbo ya maangamizi yako. Jaribu kuyakacha.

Kijana mmoja alikuwa mtaani na mama yake, rafiki yake akamwambi, oya bado hujaacha tabia yako ya kula wamama! Ayiii! Mazowea ni hovyo sana!

Ofa ya Sikukuu inaisha. Changamka. Ni vitabu 10 kwa Sh 20,000. Ni softcopy. Mpesa 0753665484.

Cheers
Mwl. Denis Mpagaze
Muhenga wa Karne ya 21!


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger