Saturday 9 December 2023

SERIKALI ITAENDELEA KUTAMBUA, KUHESHIMU NA KUTHAMINI MCHANGO WA KANISA KATOLIKI

...


Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amesema kuwa serikali itaendelea kutambua, kuheshimu na kuthamini mchango wa Kanisa Katoliki.

Hayo yamesemwa leo tarehe 9 Desemba, 2023 wakati aliposhiriki hafla ya Kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Paul wa pili Parokia ya Lubaga Jimbo Kuu Katoriki Shinyanga hafla iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Dar es salaam Mwadhama Paolycarp Kardinali Pwngo.

RC Mndeme amesema kuwa, tunapoadhimisha miaka 62 ya Uhuru wa Tanganyika, nchi imeweza kupiga hatua kubwa sana katika kuwatumikia wananchi wake hasa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na matokeo yake yanaonekana chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

"Serikali itaendelea kutambua, kuheshimu na kuthamini mchango wa kanisa katoriki, na kwa kuzingatia kuwa nchi leo inaadhimisha miaka 62 ya Uhuru na maendeleo makubwa yanaoneka chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan", alisema RC Mndeme.

Kwa upande wake Mwadhama Kardinaly Pengo alisema kuwa, uzuri na upya wa kanisa hili halitakuwa na yoyote iwapo waumini wake hawataishi katika matendo ya upendo katika mioyo yao na maisha ya kumpendeza Mwenyezi Mungu na akawataka wananchi kuja kanisani hapa kwa ajili ya kuomba msamaha na ndiyo sehemu pekee ambayo unaweza kuomba msamaha kwa mungu.

Kando na hafla hii, pia RC Mndeme amewapa nafasi kufungua rasmi matumizi ya Kitabu cha Ibada ambacho kina mafundisho mbalimbali, sala, novena na nyimbo ambazo zitamuwezesha muumini kusali na kuelewa kwa urahisi zaidi kitabu hiki kitakuwa kinapatikana katika kanisa mbalimbali hapa Shinyanga.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger