Monday, 5 September 2022

JESHI LA POLISI LAMKAMATA MWANAMKE ALIYEMFANYIA UKATILI MTOTO WAKE

...


JESHI la Polisi nchini Uganda, linamshikilia Dorothy Nabulime (22) mkazi wa mji mdogo wa Busula, nje kidogo ya jiji la Kampala kwa tuhuma za kumpiga na kumfanyia ukatili mwanae wa kike mwenye umri wa miaka miwili.

Dorothy mama wa watoto watatu alirekodiwa video akimpiga mwanae huyo bila huruma na kumuangusha kwenye beseni alilokua anaogea.
Mwanae mkubwa ana miaka 5 ambaye alimzaa akiwa na miaka 17. Wa pili ana umri wa mitatu na wa mwisho ana miaka miwili ambaye ndiye aliyerekodiwa akimpiga. Dorothy ni “single mother” ambaye anadaiwa kupitia unyanyasaji wa kijinsia katika malezi yake, na anawalea watoto wote watatu peke yake kwa biashara ndogondogo.

Amefunguliwa kesi ya shambulio la kudhuru mwili (assault causing bodily harm) na unyanyasaji wa mtoto (child abuse) na anatarajiwa kupandishwa kizimbani kesho, jumatatu kujibu tuhuma zinazomkabili. Kwa sasa anashikiliwa kituo cha polisi Luwero, huko Busula na amefunguliwa kesi nambari SD/RF/06/03/09/2022.

Ikiwa atapatikana na hatia anaweza kufungwa kati ya miaka miwili hadi mitano Gerezani.!
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger