Katika mchezo huo wa awali goli pekee la Simba lilifungwa na kiungo Mzambia, Clatous Chama akimaliza kazi nzuri iliyofanywa na Winga Luis Miquissone.
Sasa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) watakutana na FC Platinum ya Zimbabwe ambayo imetinga hatua hiyo baada ya kuwafunga Costa do Sol ya Msumbiji kwa ushindi wa jumla ya goli 4-1 baada ya kushinda 2-1 na kisha kushinda goli 2-0 katika mchezo wa marudianoa uliochezwa leo kwenye mji wa Bulawayo.
Katika mchezo huo, Simba itaanzia ugenini katika mchezo utakaochewa kati ya Desemba 22 au 23 katika uwanja wa National Sport na kisha watarudiana kati ya Januari 5 au sita katika uwanja wa Mkapa.
0 comments:
Post a Comment