Friday, 11 January 2019

ATOROKA KIFUNGO BAADA YA USHAHIDI KUMMBANA

Na Stephen Noel Mpwapwa -Dodoma. Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Julias Lwagila (51)aliyekuwa anakabiliwa na tuhuma za kulima zao la Bangi Heka tatu atoroka kifungo. Mtuhumiwa huyo hakuonekana mahakamani wakati wa kusomewa hukumu hiyo kitu kinachopelekea kuaminika kuwa ametoroka hukumu Hiyo baada ya kuona kesi inamwendea vibaya. Pamoja na kutokuwapo mahakamani lakini Mahakama ya Hakimu mkazi ya wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma imewahukumu watuhumiwa wengine kifungo cha miaka thelathini (30) bwana Julius Lwagila mkazi wa kijiji cha Wota, Kata Lwihomelo na wilaya ya Mpwapwa. Kesi hizo zilikuwa zinasikilizwa na…

Source

Share:

SERIKALI YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI NNE ZA KUBANGUA KOROSHO

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga jana (10 Januari 2019) ameshuhudia hafla ya utiaji saini mikataba ya ubanguaji korosho kati ya Bodi ya nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania na wenye viwanda vya ndani. Mkurugenzi wa Bodi ya nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania Dkt Hussein Mansoor ndiye ametia saini kwa niaba ya serikali na Kampuni nne zimesaini mikataba ya awali kuanza kazi hiyo ambazo ni kampuni ya Hawte Investment Co. Ltd, Micronix Mtwara, Korosho Afrika, na Micronix-Newala. Kampuni hizo zimeingia mikataba ya Jumla ya Tani 7500 ambapo kampuni ya Hawte Investment Co.…

Source

Share:

MWILI WA MTOTO ALIYEPOTEA WIKI MBILI ZILIZOPITA WAKUTWA KATIKA POLI NJOMBE

Na.Amiri kilagalila Mwili wa mtoto wa miaka 6 anayefahamika kwa jina la Godluck Mfugale aliyepotea wiki mbili zilizopita mkoani Njombe wakutwa katika poli lililopo karibu na shule ya secondary Njombe (NJOSS) ukiwa umeharibika. Akizungumza wakati wa Ibada ya kuuaga mwili huo iliyofanyika katika kanisa la KKKT mtaa wa Melinze mjini Njombe,mchungaji wa KKKT jimbo la Njombe Bernad Sagaya amesema kuwa mwili wa mtoto huyo ulipatika siku ya jana ukiwa umeharibika hali ambayo imewashtua wakazi wa mji wa Njombe kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya mauaji ya watoto. Aidha kiongozi huyo…

Source

Share:

MWILI WA MTOTO ALIYEPOTEA WIKI MBILI ZILIZOPITA WAKUTWA KATIKA PORI NJOMBE

Mwili wa mtoto wa miaka 6 anayefahamika kwa jina la Godluck Mfugale aliyepotea wiki mbili zilizopita mkoani Njombe wakutwa katika pori lililopo karibu na shule ya secondary Njombe (NJOSS) ukiwa umeharibika. Akizungumza wakati wa Ibada ya kuuaga mwili huo iliyofanyika katika kanisa la KKKT mtaa wa Melinze mjini Njombe,mchungaji wa KKKT jimbo la Njombe Bernad Sagaya amesema kuwa mwili wa mtoto huyo ulipatika siku ya jana ukiwa umeharibika hali ambayo imewashtua wakazi wa mji wa Njombe kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya mauaji ya watoto. Aidha kiongozi huyo wa kanisa…

Source

Share:

WAHANDISI WA MAJI WASIOKUWA NA SIFA WAKALIA KUTI KAVU.

Na mwandishi wetu-Bukoba Naibu waziri wa Maji na Mbunge wa Jimbo la Pangani Mh. Jumaa Aweso amewataka wahandisi wasiokuwa na sifa na Vigezo ndani ya wizara hiyo hususani wahandisi wababaishaji, kujitathimini mapema kwani msasa utapita kwa ajili yao. Aweso ametoa tamko hilo akiwa Mkoani Kagera katika ziara Mahususi iliyoanzia katika Ofisi za Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mjini Bukoba (BUWASA), kisha kutembelea kituo cha uzalishaji maji kilichopo Bunena, Bukoba Manispaa na baadae kukagua tanki la Maji lililopo Kashura na lile linalojengwa Ihungo ndani ya Manispaa ya Bukoba. Katika…

Source

Share:

WAHANDISI WA MAJI WASIOKUWA NA SIFA WAKALIA KUTI KAVU.

Na mwandishi wetu-Bukoba Naibu waziri wa Maji na Mbunge wa Jimbo la Pangani Mh. Jumaa Aweso amewataka wahandisi wasiokuwa na sifa na Vigezo ndani ya wizara hiyo hususani wahandisi wababaishaji, kujitathimini mapema kwani msasa utapita kwa ajili yao. Aweso ametoa tamko hilo akiwa Mkoani Kagera katika ziara Mahususi iliyoanzia katika Ofisi za Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mjini Bukoba (BUWASA), kisha kutembelea kituo cha uzalishaji maji kilichopo Bunena, Bukoba Manispaa na baadae kukagua tanki la Maji lililopo Kashura na lile linalojengwa Ihungo ndani ya Manispaa ya Bukoba. Katika…

Source

Share:

UCHAGUZI WA YANGA WAOTA MBAWA NAMNA HII, TFF YATOA TAMKO

KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetangaza kuusimamisha Uchaguzi Mkuu wa Yanga uliopangwa kufanyika Jumapili hii kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi uliopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Kamati hiyo imefikia hatua hiyo kwa kile kilichoelezwa kuwa baadhi ya wanachama wa Yanga wamefungua kesi mahakamani wakitaka uchaguzi huo usimamishwe.

Akitangaza uamuzi huo, mwenyekiti wa kamati hiyo, Malangwe Mchungahela, amesema: “Leo tulikuwa kwenye vikao vya mwisho kuangalia kama mambo yote yamekaa sawa.

“Tukiwa kwenye vikao hivyo, tukapata taarifa kwamba kuna baadhi ya wanachama wa Yanga wamefungua kesi ya kusimamisha uchaguzi hapa Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Morogoro na sehemu nyinginezo.

“Sasa sisi kama kamati hatutaki kugombana na muhimili wa mahakama na kwa sababu tumesikia sehemu zingine mashauri yameanza kusikilizwa, tumeamua kusimamisha uchaguzi usifanyike Jumapili hii mpaka tupate muongozo wa kilichojiri huko mahakamani.

“Jumatatu tutawapa msimamo wa uchaguzi, lakini kwa sasa kamati ya uchaguzi imesitisha uchaguzi huo kwa muda na wala hatujaufuta. Wale wagombea waliokuwa wakipiga kampeni tumewaambia wasimame kwanza.”

Uchaguzi huo wa Yanga ulikuwa na lengo la kujaza nafasi za uongozi klabuni hapo zilizoachwa wazi ambapo ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti na wajumbe watatu.
Share:

WAFANYABIASHARA WANAOKIMBIA KODI WAPEWA SOMO

Na Allawi Kaboyo-Bukoba Kagera. Mkuu wa mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti amewataka wafanyabiashara mkoani humo kuacha tabia ya kufunga maduka yao palea wanapowaona maafisa wa TRA wakija katika maduka yao na kumuagiza meneja TRA wa mkoa huo kujenga mahusiano mazuri na wafanyabiashara pamoja na kutoa elimu ya kutosha ya umuhimu wa kulipa kodi. Mkuu wa mkoa ametoa agizo hilo katika kikao chake na wadau wa kodi,maafisa wa TRA pamoja na wafanyabiashara kilichofanyika january 11 mwaka huu kwenye ukumbi wa manispaa ya Bukoba kikiwa na lengo la kujua hali ya…

Source

Share:

MAKONDA "MNIOMBEE,NIKIKUA NIWE KAMA RAIS MAGUFULI"


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amewaomba viongozi wa dini wamuombee ili atimize ndoto ya kuwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Muda mfupi uliopita akizungumza katika mapokezi ya ndege aina ya Airbus A220-300 uwanja wa ndege, Makonda amewataka viongozi wa Dini kumuombea juu ya ndoto yake ya kuwa kama Rais Magufuli kwa kuwa ni mtu wa kutekeleza.

"Viongozi wa dini naomba mniombee, nataka nikikua niwe kama Rais Magufuli, haya ni maombi yangu kabisa, kwa sababu ni mtu wa kutekeleza, usiyeyumbishwa,umehakiksha Mungu kwanza na unaipenda Tanzania kuliko hata familia yako"- Paul Makonda.

Makonda ameongeza, "hivi ulivyo Rais wetu angekuwa mwingine Watoto wake tungekuwa tunagombana nao mtaani lakini Wewe umehakikisha hakuna anayeingilia jukumu lako kama Baba wa familia" Makonda

Pamoja na hayo Makonda amemwambia Rais Magufuli, yeye na wakazi wa Dar es salaam wamekwenda kumuunga mkono kwa kuwa alitoa ahadi kutoka kwenye ilani ya CCM na anatekeleza ikiwemo elimu bure

"Nilipotoa tangazo la kuja hapa nilisema waje wale waliowahi kutoa ahadi na wakatekeleza" Makonda.
Share:

ASKOFU KAKOBE AMUONESHEA UBISHI RAIS MAGUFULI..AMUOMBA LEO ALALE


Askofu Zakary Kakobe

Askofu Mkuu wa kanisa la Full Gospel Bible fellowship (FGBF), Zakary Kakobe, ameweka wazi kukoshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli kwa kuweza kuingiza ndege nyingine ya Air Bus 220-300.

Askofu Kakobe ameyasema hayo leo katika mapokezi ya ndege ya sita zilizoingizwa nchini katika awamu ya uongozi wa Rais Magufuli.

Kakobe ametumia nafasi yake ya kuliombea taifa kutoa maneno hayo kwa Rais Magufuli, ambapo amesema kwamba, " Mimi ni mbishi sana. Ukiniona nimekanyaga mahali hapa ujue umenikosha sana".

Askofu Kakobe amemuomba Rais Magufuli atumie siku ya leo kwa kulala ikiwa ni sehemu ya kujipongeza kwa kufanikisha kuingiza ndege nyingine nchini ( kwa kuwa Rais Magufuli aliwahi kutamka hadharani kwamba kitanda chake kimejaa ma-file, kiasi cha kumnyima usingizi).

Mbali na hayo, kiongozi huyo wa dini amemsifu Rais Magufuli kuwa kama Rubani na kwamba Watanzania wanakusanya kodi na yeye amekuwa akizitumia kwa usahihi.
Share:

Picha:MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA AGAWA VITAMBULISHO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO... AWAKUMBUSHA NIDHAMU YA FEDHA

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amewakabidhi wafanyabiashara wadogo Vitambulisho Maalumu vilivyotolewa na Mheshimiwa Rais Dr John Pombe Magufuli huku akiwataka kuwa waaminifu na wazalendo wa taifa lao 
Uzinduzi wa kutolewa vitambulisho hivyo umefanyika Alhamisi Januari 10,2019 katika ukumbi wa mikutano uliopo katika jengo la halmashauri ya wilaya ya Shinyanga . 

Akizindua zoezi hilo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amewataka Wafanyabiashara hao kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha zinazopatikana kutokana na shughuli wanazofanya ili ziweze kuwanufaisha,na kuwaondoa katika hali ya Umasikini. 

“Tuwe na nidhamu ya matumizi ya fedha , umeshalipa kodi yako ya shilingi 20000 kwa mwaka mmoja utapewa kitambulisho na mwaka mwingine unatakiwa ulipe, sasa utakapolipa maana yake fedha utakazokuwa unaendesha biashara zisiingie tumboni tu zikafanye pia maendeleo kwenye familia yako” alisema Mboneko 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi ametahadharisha Wafanyabiashara wakubwa kutojihusisha na udanganyifu kuuza bidhaa zao kwa kuwatumia wafanyabiashara ndogondogo wenye vitambulisho vilivyotolewa na Mheshimiwa Rais kwani kwa kufanya hivyo ni kukwepa ulipaji wa kodi 

“Unakuta mtu anaduka anatoa bidhaa za kwake anawapatia hawa wafanyabiashara ndogondogo ambao hawalipi kodi kwa hiyo anafunga duka lake wakati bidhaa zake zikiendelea kuuzwa mtaani, huyu anakwepa kulipa kodi na tumeshawabaini na tutawachukulia hatua” alisema Mwangulumbi. 

Kwa upande wao Wafanyabiashara ndogo ndogo wameshukuru na kupongeza hatua ya Mheshimiwa Rais Dr John Pombe Magufuli kutoa vitambulisho hivyo ambavyo vitawasaidia kufanya shughuli zao kwa amani na utulivu ikilinganishwa na hapo Mwanzo ambapo walikuwa wakipata usumbufu.

ANGALIA PICHA 

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amewakabidhi wafanyabiashara wadogo Vitambulisho Maalumu vilivyotolewa na Mheshimiwa Rais Dr John Pombe Magufuli huku akiwataka wafanyabishara  kuwa waaminifu na wazalendo wa taifa lao . Picha zote na Steve Kanyefu Malunde1 blog

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akikagua baadhi ya fomu ambazo mfanyabiasha ndogondogo anatakiwa kujaza taarifa zake ili apatiwe kitambulisho 

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko  akiongoza zoezi la kuwapatia vitambulisho baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria katika uzinduzi wa utolewaji wa vitambulisho uliofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo katika jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi akisisitiza jambo ambapo amewataka wafanyabishara kuzingatia usafi katika mazingira ya biashara zao.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko (katikati),kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi na kulia ni Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Shinyanga Jumbe Samson wakisikiliza kwa makini baadhi ya maoni ya Wafanyabishara .

Mkuu wa Wilaya akisisitiza jambo kwa baadhi ya wafanyabishara waliohudhuria katika uzuinduzi wa kugawa vitambulisho kwa wafanyabiashara ndogondogo

Meneja wa TRA Mkoa wa Shinyanga Jumbe Samson akiwasisitiza wafanyabishara kutumia vyema vitambulisho hivyo ili kuepuka usumbufu pindi ukaguzi wa kuwabaini wasio na vitambulisho utakapoanza.
Baadhi ya Wafanyabishara wakiwa ukumbini




Share:

Picha : RAIS MAGUFULI AKUTANA NA SUNIL MITTAL MWENYEKITI WA BHARTI AIRTEL IKULU

Share:

MAANDAMANO YA KUMTAKA RAIS AJIUZULU YAENDELEA SUDAN

Maandamano hayo ni changamoto kubwa kwa Rais Omar Al-Bashir jenerali wa zamani wa jeshi ambaye aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi 1989 na tangu wakati huo anashinda uchaguzi ambao wapinzani wake wanasema sio wa haki na wala huru


Vikosi vya usalama nchini Sudan vilifyatua gesi ya kutoa machozi kuwasambaratisha  waandamanaji katika mji wa Omdurman huko Sudan siku ya Alhamis. 

Shahidi mmoja aliliambia shirika la habari la Reuters katika wiki kadhaa za karibuni za maandamano yanayoipinga serikali yaliyochochewa na malalamiko ya kiuchumi na kisiasa.


Wakati huo huo shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International lilivishutumu vikosi vya usalama katika mji kwa kusababisha majeraha kwa waandamanaji walioko ndani ya hospitali baada ya maandamano ya Jumatano ambapo watu watatu waliuwawa. Baadhi ya watu waliojeruhiwa katika maandamano hayo walipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu.

Vifo vya Jumatano vimejumuisha idadi ya takribani watu 22 waliouwawa huko Sudan tangu maandamano yalipoanza Disemba 19 mwaka jana wakiwemo wafanyakazi wawili wa usalama kwa mujibu wa idadi iliyotolewa na maafisa.


Mamia ya watu pia wamejeruhiwa na mamia wengine wamekamatwa.Siku ya Alhamis huko Omdurman waandamanaji walizuia mtaa wa 40 kwenye mji huo kabla ya vikosi vya polisi kuwashambulia kwa gesi ya kutoa machozi na kulazimisha wengi kutawanyika kuelekea upande wa pili wa barabara. Hakukuwa na ripoti za haraka kuhusiana na vifo vyovyote vilivyotokea hapo.

Chanzo:Voa
Share:

WAZIRI WA MAMBO YA KIGENI POMPEO ASHAMBULIA SERA ZA OBAMA

Ägypten | Mike Pompeo (picture-alliance/dpa/AP Photo/A. Nabil)Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Mike Pompeo aliyasema  hayo katika ukosoaji  mkubwa  wa  sera  za  rais  huyo  wa  zamani  licha  ya hatua  za  mkuu  wa  Pompeo  rais Donald Trump  kuamua kuviondoa  vikosi vya  jeshi  la  Marekani  kutoka  Syria.

"Tunahitaji  kutambua  ukweli  huu kwasababu  iwapo  hatutafanya hivyo, tutafanya  makosa  ya  uchaguzi kwa  hivi  sasa  na  hapo baadaye Na uchaguzi  wetu , kile  tutakachokichagua  leo kina athari kwa  mataifa na  kwa  mamilioni  ya  watu , kwa  usalama  wetu, kwa ufanisi  wa  uchumi wetu, kwa  uhuru  wetu , na  ule  wa  watoto wetu." Alisema Pompeo
Katika  hotuba  ambayo  aliitoa  katika  chuo  kikuu  cha  Marekani mjini  Cairo, Pompeo  alijitenga  na utamaduni  wa  kidiplomasia  wa Marekani  wa  kuepuka kutangaza  hadharani  mizozo  wa  ndani nchini  Marekani  kwa  kumshambulia  Obama  katika  mahali ambapo  mtangulizi  huyo  wa  rais  Trum  alitoa  hotuba  ya kihistoria  yenye  lengo  la  kuimarisha  mahusiano  na  ulimwengu wa  Kiislamu.

 Pompeo ameiwasilisha  Marekani  kuwa  ni  nguvu  ya kufanya  mazuri  katika  mashariki  ya  kati,  na  kudokeza  kwamba Obama  aliiona  Marekani  kama " nguvu  inayoitaabisha  mashariki ya  kati".

Baadhi  ya  maafisa  wa  zamani  wa  Marekani  na  wachambuzi wamemshutumu  mwanadiplomasia  huyo  wa  ngazi  ya  juu  wa Marekani  kwa  kusoma  vibaya  historia  na  kujificha  katika mapenzi  ya  binafsi  ya  Trump  kupunguza  jukumu  lake  katika eneo  hilo.

Chanzo:Dw
Share:

MAHAKAMA YAWAFUTIA KESI KITILYA NA WENZAKE..WARUDISHWA MAHABUHUSU TENA BAADA YA KUACHIWA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewafutia mashtaka aliyekuwa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Harry Kitillya, maofisa wawili wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kueleza mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na shauri lao.

Uamuzi huo umetolewa leo Januari 11, ambapo washtakiwa walikuwa wanakabiliwa na mashtaka nane yakiwemo ya kutakatisha fedha, na kwamba wamefutiwa kesi hiyo chini ya kifungu namba 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai (CPA), sura ya 20, iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Kabla ya kukamatwa tena, Wakili Mkuu wa Serikali, Hashimu Ngole akisaidiana na wenzake Pendo Mangole na Patrick Mwida, amedai kuwa DPP hana nia ya kuendelea na shauri hilo dhidi ya washtakiwa.

"Taarifa hii ya kutokuendelea na shauri hili mbele ya mahakama yako, imeletwa chini kifungu namba 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), sura ya 20, iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002," amesema Ngole. Baada ya maelezo hayo,

Hakimu Ally alisema kutokana na maombi hayo, mahakama hiyo imeifuta kesi hiyo, hata hivyo walikamatwa mara tu baada ya kuachiwa na kupelekwa tena mahabusu.
Share:

CRISTIANO RONALDO KUCHUNGUZWA TUHUMA ZA UBAKAJI POLISI YATOA WARANTI

Polisi mjini Las Vegas wametoa waranti ya kuchunguzwa kwa chembe chembe za vinasaba au DNA ya Cristiano Ronaldo kama sehemu ya uchunguzi wa madai ya ubakaji dhidi ya nyota huyo wa kimataifa wa Ureno anayechezea klabu ya Juventus.

Wakili, Peter S. Christiansen, ameiambia BBC Michezo kuwa ombi hilo ''ni la kawaida''.

Jarida la Wall Street limeripoti kuwa waranti hiyo imewasilishwa hivi karibuni katika mfumo wa mahakama ya Italia.


Ronaldo amekanusha kwamba alimshambulia mwanadada Kathryn Mayorga katika mgahawa mmoja mjini Las Vegas hotel mwaka 2009.

''Bwana Ronaldo amekua akishikilia usemi kuwa yale yaliyotokea Las Vegas mwaka 2009 ni mambo ya watu wawili waliyokubaliana, kwa hiyo bila shaka chembe chembe za DNA zitapatikana, kwa hiyo sioni haja ya polisi kutoa ombi hilo kama sehemu ya uchunguzi wao,"ilisema taarifa ya Christiansen.

Gazeti la Der Spiegel la Ujerumani ambalo lilikuwa la kwanza kuangazia taarifa hiyo mwezi Oktoba, lilisema kuwa Bi Mayorga aliandikisha ripoti katika kituo cha polisi cha Las Vegas muda mfupi baada ya kufanyika kwa tukio linalodaiwa.

Der Spiegel lilisema kuwa mwaka 2010, Mayogra aliafikiana na Ronaldo kutatua suala hilo nje ya mahakama ambapo alilipwa dola 375,000 ilisizungumza hadharani madai hayo.

Chanzo:Bbc
Share:

WATATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI,TUHUMA YA WIZI WA MKOBA ULIOJAA DOLA ZA MUGABE

Watu watatu wamefikishwa mahakamani nchini Zimbabwe, wakishtakiwa kuiba mkoba uliokuwa na $150,000 (£117,600) pesa taslimu mali ya rais wa zamani wa taifa hilo Robert Mugabe.

Washukiwa hao wa wizi wanadaiwa kutumia pesa hizo kununua magari, nyumba na mifugo.

Jamaa wa rais huyo wa zamani, Constantia Mugabe, ni miongoni mwa walioshtakiwa, kwa mujibu wa taarifa katika vyombo vya habari vya serikali.

Mwanamke huyo anadaiwa kuwa na funguo za nyumba ya kijijini ya Bw Mugabe iliyo eneo la Zvimba karibu na mji mkuu wa Harare, na ndiye aliyewasaidia hao wengine kuingia humo na kufika ulikokuwa mkoba huo.

Washukiwa hao wengine walikuwa wameajiriwa kama wafanyakazi wa kufagia na kusafisha nyumbani humo wakati wa kutekelezwa kwa wizi huo siku moja kati ya tarehe 1 Desemba na mapema Januari.

Chanzo:Bbc
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger