Friday 5 June 2020

Tufanye mambo gani ili tuweze kunufaika na maendeleo ya kiteknolojia?

...
Nchini Tanzania, kama ilivyo katika maeneo mengine duniani teknolojia imeleta maendeleo na mabadiliko makubwa kwenye jamii.

Hakuna shaka yoyote kwamba teknolojia imebadili namna na kasi ya mawasiliano yetu ambayo yamepitia hatua mbalimbali kuanzia barua posta, simu za mezani na sasa kidijitali.

Katika miezi ya karibuni gonjwa la korona limewavuta watu wengi zaidi kutumia mbinu za kidijitali si tu kuwasiliana bali hata kwenye kufanya malipo na kupata burudani.

Tukitazama mbele yapo mambo mbalimbali tunayoweza kufanya kuhakikisha kwamba sote tunafaidi matunda ya teknolojia na uchumi wa kidijitali.

Jambo mojawapo ni kuhakikisha huduma ya fedha kidijitali inapatikana kwa watu wengi zaidi.

Huduma ya namna hii ni muhimu katika kukuza uchumi, kupanua wigo wa mfumo rasmi wa fedha na ni njia rahisi kufanya malipo, kutuma na kupokea fedha.

Kampuni za simu nchini Tanzania zimechangia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha tunanufaika na teknolojia. Kampuni kama Tigo Tanzania kupitia huduma yake ya Tigo Pesa ni moja ya wadau wanaohakikisha hilo.

Ubunifu pia ni muhimu kadiri mahitaji na teknolojia inavyobadilika. Ubunifu kama huduma ya Ujanja Ni kutoka Tigo kwa mfano inawapa wateja wake vifurushi vya intaneti na dakika katika bei wanazomudu.

Tuendelee kuwa wabunifu katika zama hizi za teknolojia ili tuzidi kuvuna matunda yake.




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger