Saturday 27 June 2020

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya 17,18 na 19

...
Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188

ILIPOISHIA
“Baby vipi?”
Magreth aliuliza huku akimsangaa nabii Sanga akishuka kitandani. Nabii Sanga siku zote ana mfahamu mke wake, ni mtu ambaye ana simamia misimamo yake pale anapo amua jambo fulani kulifanya, tena awe ameliamua kihasira. Woga wa siri zake kuwa hadharani ukamfanya, ajikute akitengua mamauzi ya kuuwawa kwa Tomasa. Akaitafuta namba ya RPC na kumpigia, ili kumpa agizo la kusitisha zoezi hilo. Mapigo ya moyo yakazidi kumdunda nabii Sanga huku jasho likimwagika, mara baada ya kukuta namba ya RPC haipatikani hewani huku akitambua kwamba muda huu ndio wakati wa Tomasa kuuwawa kisiri.


ENDELEA
 “Ohoo Mungu wangu”
Nabii Sanga alihaha, huku akijaribu kuipiga tena simu ya RPC ila majibu aliyo kutana nayo hapo awali ndio hayo hayo anayo kutana nayo kwa muda huu. 
“Baby niambie ni kuna tatizo gani?”
Magreth alizungumza huku akishuka kitandani na kumdadisi nabii Sanga.
“Kuna mambo ya kifamilia tafadhali naomba uniache kidogo”
Nabii Sanga alizungumza huku jasho likiendelea kumtiririka mwili mzima. Japo kuna air condition, ila haikuzuia jasho kuto mwagika kwa kiasi hicho.
“Nani nani nani?”
Nabii Sanga alizungumza huku akijaribu kutafakari ni nani ambaye ana weza kuzungumza naye kwa haraka ili kumfikia RPC. Nabii Sanga akamkumbuka mke wa RPC ambaye pia ni miongoni mwa viongozi wa kanisa lake. Akampigia na kwa bahati nzuri simu hiyo ikapokelewa.
“Habari za muda huu mama Karata”
“Salama tu baba mchungaji habari ya muda huu?”
“Salama, samahani sana kwa kukusumbua usiku”
“Hakuna taba baba yangu. Kwanza pole kwa kilicho tokea, yaani nilishindwa kufika kanisani leo kwa maana nipo safarini kwa sasa”
“Ahaa upo wapi kwa sasa?”
“Nipo Mwanza huku, nimekuja kumuuguza uguza mama mkwe, kidogo magonjwa ya uzeeni yana msumbua”
“Ahaa poleni sana”
“Tunashukuru kwa kweli, nina imani bwana Mungu ata kwenda kunyoosha mkono wake juu yetu”
“Hakika yeye ni mwema. Sasa nilikuwa nina hitaji kupata namba ya Mr Karata kwa maana nina mpigia kwenye ile namba yake iliyo ishia mwisho nane nane, ila simpati hewani kabisa”
“Ahaaa niliongea naye kama lisaa lililo pita. Akaniambia kwamba yupo njiani ana elekea poroni kwenye oparesheni ya kusaka majambazi hivyo akanitaarifu kwamba ata zima simu yake. Ila kuna namba yake nyingine ambayo ni private ya familia labda nikupatie hiyo baba”
“Nitashukuru sana mama Karata”
“Sawa, kata simu nikutumie.”
Nabii Sanga akakata simu huku jasho likimvuja sana mwilini mwake. Hakuna kitu anacho kiogopa kwa mke wake kama kutoboa siri zake za ndani, ndio maana hata mke wake afanye kosa la aina gani basi yupo radhi kumsamehe na kuto muhukumu kwa chochote. Ujumbe mfupi wa meseji ukaingia, kwa haraka akaufungua na kukuta namba hiyo ya simu. Hakuhitaji hata kujibu ujumbe huo, akaipiga namba hiyo na kwa bahati nzuri ikaanza kuita.
                                ***
RPC akapunguza mwendo wa gari lake huku akiwaza ni nani anaye mpigia kwenye simu yake ya siri sana ambayo ni yeye na wana familia wake ndio wana fahamu namba hiyo. Taratibu akaitoa simu hiyo ndogo aina ya Bontel na kuitazama namba hiyo vizuri na kuifahamu kwa haraka.
‘Ameitoa wapi namba yangu?’
RPC alizungumza kimoyo moyo huku akiitzama namba hiyo ya nabii Sanga inayo mpigia. Akasimamisha gari pambezoni mwa barabra, kisha akafungua mlango na kutoka nje ili Tomas asiweze kufahamu ni mtu gani ambaye amemteka kwa maana kama ni sauti ya RPC ni maarufu sana karibu kwa Watu wote kwani mara kwa mara huonekana kwenye vyombo vya habari akizungumza na waandishi wa habari.
“Ndio mzee”
RPC Karata alizungumza huku akitazama usalama wa eneo hilo.
“Upo wapi asiee?”
“Naelekea Kibiti. Namba hii sikumbuki kama nilisha wahi kukupatia mzee”
“Ni kweli, amenipatia mama muda huu. Nilikuwa naomba uweze kusitisha zoezi tulilo panga ulifanye”
“Kwa nini!!?”
RPC Karata alizungumza huku akiwa ameshikwa na mshangao mkubwa.
“Kuna mambo ambayo hayato kwenda sawa. Ninacho kuomba ni kumuachia huru na pesa niliyo kupatia wewe iwe ni zawadi yako”
RPC Karata akakaa kimya huku akitafakari ni nini cha kufanya. Kama ni kumuachia huru Tomas ni lazima polisi wata mtafuta wakiamini kwamba ata kuwa ametoroka gerezani. Pia akimua askari vile vile wata mtafuta kwa kigezo hicho hicho cha kutoroka gerezani.
“Kipi bora sasa?”
RPC Karata alijikuta akijiuliza huku simu ikiwa sikioni mwake.
“Bora kivipi?”
“Ahaa samahani sio swali lako. Okay nimekuelewa, ila kwa sharti moja”
“Sharti gani?”
“Ufunge kinywa chako, usimuambie hata mke wako juu ya hili swala letu. Nina familia ina nitegemea nyuma yangu hivyo sihitaji matatizo yasiyo ya lazima kwenye maisha yangu.”
“Hilo sinto weza kulizungumza”
“Na jambo jengine ina bidi aondoke nchini Tanzania na akatafute nchi ya kwenda la sivyo. Mkono wa sheria ni mkubwa sana na utamsaka ndani ya nchii hii na endapo ata kamatwa, aisee hapo mimi sinto ingilia kati kwani jambo hilo litakuwa nje ya uwezo wangu”
“Nimekuelewa”
“Sawa mzee nashukuru kwa kunielewa”
RPC Karata akakata simu huku akiachia msunyo mzito, kwani kwenye maisha yake huwa hapendi kuianza kazi na kuiachia njiani.  Akamtazama Tomas aliye muweka siti ya nyuma, akafungua mlango huo na kumtoa Tomas. Akamfungua mnyororo wa miguuni pamoja na pingu za mikononi. Akamuwekea bastola ya kichwa na kumfanya Tomas kujawa na woga.
“Leo hii Mungu wako amekusaidia na umepona kuhusiana na swala kutembea na mke wa mtu. Kesho rudia tena roho yako ita kwenda ahera madukani bila ya wewe kupenda. Potea ndani ya nchi hii kabla jeshi la polisi halijakukamata”
RPC Karata alizungumza kwa sauti nzito ambayo sio rahisi kujulikana. Akampiga Tomas kichwani kwa kutumia kitako cha bastola hiyo na kumpelekea kupoteza fahamu. Akamsukumia pembezoni mwa mtaro huku macho yake yakiwa yame fungwa na kitambaa cheusi. Kisha akarudi ndani ya gari lake na kuondoka eneo hilo na kurudi zake jijini Dar es Salaam huku akimtumia meseji nabii Sanga kwamba ame muachia huru Tomas.
                                    ***
‘TAYARI TOMAS AMEACHIWA HURU MKE WANGU. USIFUNGUE KINYWA CHAKO’
Mrs Sanga mara baada ya kuisoma meseji hiyo kutoka kwa mume wake, akatabasamu huku akiwa amejawa na furaha sana, kwani mpango wake umekwenda sawia kama vile alivyo kuwa ame panga.
‘Hawezi kukurupuka kwangu huyu fala’
Mrs Sanga alizungumza huku akishushia kipande cha nyama anacho kitafununa kwa fumba zito la wyne. Ujumbe mfupi ukaingia whatsapp, akaufungua na kukuta video kutoka kwa mume wake. Akaifungua video hiyo. Macho yakamtoka, mapigo ya moyo yakaanza kumuenda kasi sana. Pombe iliyo kuwa imesha anza kukitawala kichwa chake, yote ikakata. Video ya ngono, inayo muonyesha yeye na Tomas wakifanya mapenzi ofisini kwa mume wake, ndio hiyo aliyo tumiwa na mume wake. Ukaingia ujumbe mwengine wa meseji kutoka kwa mume wake kupitia whatsapp.
‘ENDAPO UTARUDIA KUTEMBEA NA HUYO PAKA WAKO. NITAISAMBAZA HII VIDEO NA TUONE MIMI NA WEWE NANI NI ZAIDI YAKO.’
Mrs Sanga mikono yote ikazidi kumtetemeka kwa woga. Hakuna kitu kibaya kwa watu wanao jiheshimu na kujulikana kama matendo yao ya ajabu ambayo watu wa kawaida hawawezi kuyajua, pale yanapo kuwa wazi hadharani na kujulikana na kila mtu.
Mume wangu’
Mrs Sanga akatuma ujumbe huo wa meseji huku akijifuta jasho. Tiki mbili za blue zikamdhibitishia kwamba huo ujumbe umesha somwa na mume wake. Nabii Sanga akajibu ujumbe huo kwa vikatuni viwili vilivyo tumbua macho.
‘Kumbuka wewe ni Mume wangu. Nime pata wivu mara baada ya kusikia una tembea na Magreth na tena umemunulia nyumba na kumfungulia mgahawa. Shetani alinipitia na nikapanga kukuteka ili usimnunulie nyumba binti huyo. Kumbuka ni wapi tulipo toka mume wangu. Pesa hizi ambazo leo tuna zichezea, kumbuka ni mambo mangapi ambayo tumeyafanya ili kuzipata. Hembu acha kuzitawanya ki hivyo.’
Mrs Sanga aliandika ujumbe huo huku machozi yakimlenge lenga usoni mwake. Ujanja wake wote wa kutunisha msuli mbele ya mume wake ume kwisha.
‘Kumbuka tuna watoto. JONSON, JACKSON na JULIETHI. Wote hao wanatarajia urithi bora kutoka kwa sisi wazazi wao. Tusigawe mali zetu mume wangu’
Mrs Sanga alizidi kutuma ujumbe wa meseji kwa mume wake huku akiwa mpole ili kuzuia maamuzi ya mume wake juu ya kuisambaza video hiyo. Kwani video hiyo ina muonyesha jinsi anavyo liwa  na Tomas.
‘Leo ndio una kumbuka una watoto wanao kutegemea eheee?’
‘Hapana nina wakumbuka kila siku mume wangu.’
‘Sasa mimi nimekuambia. Wewe fungua bakuli lako uone kama hizi video kama hazito wafikia hadi wanao. Siku zote kumbe una toa m** kwa wanaume wa nje, mimi mumeo hata  sijawahi khaaaa!! Inatia kinyaa kwa kweli’
Meseji hiyo ya nabii Sanga ikamfanya Mrs Sanga kushusha pumzi huku akitafakari nini cha kumjibu mume wake huyo.
‘Ila baba Jonson kumbuka hata wewe uli mf* yule kijana wa Nigeria. Mbona nilikusamehe na kukuahidi kukutunzia siri?’
‘Nimefanya yote yale ili kudumisha huduma yangu. Unahisii bila kufanya hivyo leo tungekuwa na makanisa Tanzania nzima?’
‘Sawa mume wangu. Niambie upo wapi nije tuyazungumze haya?’
Mrs Sanga alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Kiburi na jeuri yote ime potea.
‘Rudisha kwato zako nyumbani uta nikuta’
‘Sawa mume wangu nakuja’
Mrs Sanga, akafungua pochi yake na kuweka kiasi cha pesa anacho daiwa kwa huduma ya chakula na vinywaji aliyo patiwa. Akaayanyuka kwa haraka na kurudi chumbani kwake. Akabadilisha nguo na kuvua baibui hilo kisha,  akakushanya kila kilicho cha kwake na kuianza safari ya kurudi jijini Dar salaam huku akiwazia endapo video hiyo aliyo nayo mume wake, ikisambaa duniani kote, sura yake ata iweka wapi kama mke wa nabii Mkubwa sana kutoka nchini Tanzania.
                                ***
“Baby mbona nakuuliza swali, hunijibu mume wangu. Niambie ni nini kinacho endelea?”
Magreth alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama nabii Sanga aliye kaa kwenye sofa ndani ya chumba hicho.
“Simu yako ipo wapi?”
“Ahaa ipo pale”
“Naiomba”
Magreth akaichukua simu yake na kumkabidhi nabii Sanga.
“Ile video umeiweka wapi?”
“Eneo la kamera”
Nabii Sanga akatafuta video hiyo kisha akaifuta na kumrudishia Magreth simu yake.
“Sihitaji hiyo video iendelee kudumu kwenye simu yako”
“Sawa mume wangu, nimekuelewa”
“Niandalie suruali yangu nahitaji kwenda nyumbani sasa”
“Kwenda nyumbani!!? Kwa nini ikiwa uliniahidi kwamba tuta lala pamoja hadi asubuhi”
“Magreth fanya nilivyo kuambia nahitaji kwenda nyumba sasa hivi. Akili yangu haipo sawa”
Magreth hakuwa na ujanja zaidi ya kukubaliana na nabii Sanga. Akamuandalia nguo zake huku nabii Sanga akimpigia dereva wa kanisa lake na kumuhitaji amfwate eneo hilo la Kigamboni. Nabii Sanga akaingia bafuni na kuanza kuoga na kumuacha Magreth akiwa na maswali mengi sana. Magreth akaitazama simu ya nabii Sanga kwa sekunde kadhaa. Wivu wa mapenzi, ukamfanya aichukue simu hiyo na kuanza kupitia meseji moja baada ya nyingine ambazo amekuta akichati na mke wake. Meseji hizo zikamugopesha sana Magreth mara baada ya kusoma meseji ya mrs Sanga, anayo lalama kuhusiana na siri ya nabii Sanga ya kutoka na  kijana wa Nigeria huku nabii Sanga akisisitiza kwamba amefanya hivyo ili kuisimamisha huduma yao.
‘Huduma gani? Au kanisa?”
Magreth alizungumza huku akiirudisha simu hiyo sehemu alipo itoa huku mapigo yake moyo yakimdunda kwa woga.
‘Kumbe huyu ana tumia njia ambazo si za Mungu kuvuta waumini eheeee? Hapana bwana ana upako haya mambo yatakuwa ni ya kwao wenyewe”
Magreth alizungumza mwenyewe huku akijitahidi kuyazuia mapigo yake ya mbio yasiende spidi kwa kuhisi vitu ambavyo hana uhakika navyo. Nabii Sanga akatoka chumbani, akajifuta maji mwili mzima kisha akavaa nguo zake huku akimpigia tena dereva na kumuomba aharakishe kuja kumchukua, pasipo kujua kwamba Magreth amesoma meseji zote katika simu yake.
                                    ***
    Baada ya dakika arobaini na tano. Tomas akazinduka, kutoka kwenye hali ya kupoteza fahamu. Hii yote ni kutokana na hali ya mvua iliyo anza kunyesha maeneo hayo kwa kasi sana. Akajifungua kitambaa usoni mwake na kutazama eneo hilo. Kutokana na giza na mvua inayo endelea kunyesha hakuweza kuligundua eneo hili kwa haraka sana. Akatoka kwenye mtaro huo huku akiendelea kuvuta kumbukumbu zake ni wapi alipo. Mwanga mkali wa gari linalo kuja kwa kasi barabarani, likamfanya Tomas, apunge mkono ili kuomba msaada hata wa kuuliza kwamba hapo alipo achwa ni wapi. Ila gari hiyo ndogo ikapita kwa spidi na kutokomea kwenye upeo wa macho wa Tomasa.  Tomas akaanza kuifwata barabara hiyo ya lami huku akikisia kwamba anapo elekea itakuwa ni jijini Dar es Salaam. Akasikia mlio wa gari unao kuja nyuma yake. Akageuka na kupunga mkono na gari hilo likaanza kupungumza mwendo na kadri jinsi linavyo zidi kumsogelea ndivyo jinsi aliyo fahamu kwani namba za usajili za gari hilo ni mali ya Mrs Sanga, mwana mama aliye muharibia maisha yake matamu ya uhuru na kumfanya sasa aanze kuishi kwenye maisha mabaya ya kupoteza uhuru ndani ya nchi yake. Huku onyo na agizo la kuondoka nchini Tanzania kabla ya kukamatwa na polisi likijirudia kichwani mwake.

==> SIN -Sehemu ya 18
Gari hilo likasimama mbele yake kidogo na kumfanya Tomas kusimama huku akiwa na mashaka kiasi moyoni mwake, kwani hisia za kumuona nabii Sanga akiwa na mke wake zime mtawala kichwani mwake. Mlango wa gari hilo ukafunguliwa, Tomas hakuamini alipo muona Mrs Sanga akaishuka kwenye gari hilo. Hakujali mvua inayo nyesha ila Mrs Sanga akamkimbilia Tomas na kumkumbatia kwa nguvu huku akimpiga mabusu mfululizo ya usoni mwake.
“Jamani pole mpenzi wangu, mbona ume chafuka hivi?”
Mrs Sanga alizungumza huku akiwa amesahau kwamba hadi hapo alipo, yupo kwenye kikaangio cha mume wake na ameahidiwa na mume wake akianzisha tena mahusiano na Tomas basi video yake ya ngono ina kwenda kuwekwa mtandaoni.
“Upo na nani kwenye gari?”
“Peke yangu hembu tuondoke eneo hili mume wangu”
“Una taka twende wapi?”
“Nikupeleke sehemu yoyote ambayo uta ihitaji”
“Nahitaji kuondoka nchini Tanzania usiku huu huu. Nataka kwenda Aftika kusini kwa mke wangu”
Tomas alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama Mrs Sanga usoni mwake.
“Afrika kusini kwa mke wako.Tomas mbona hukuwahi kuniambia kwamba una mke Afrika kusini”
“Vitu vingine sio muhimu kwa wewe kuweza kufahamu. Ila kumbuka kwamba nina ondoka kwa ajili ya wewe. Nimepewa nafasi moja ya kuishi hapa duniani ni kuondoka. Sitaki tena mahusiano na wewe. Kama utaweza kunisaidia basi nisaidie ila kama huto weza kunisaidia sawa usinisaidie, ila nitajua nini cha kufanya”
Tomas alizungumza kwa msisitizo na kumfanya Mrs Sanga kukaa kimya huku akiitafakari hali hiyo ya Tomas.
“Sawa ingia kwenye gari”
Mrs Sanga alizungumza na Tomas akafungua mlango wa siti za nyuma na kuingia.
“Kaa huku mbele”
“Mama sihitaji mapenzi na wewe. Nina mtoto mdogo na mke wangu wana nitegemea. Siwezi kufa kwa ajili yako. Kama una weza nisaidie kuondoka nchini ila kama huwezi, usinisaidie”
“Ila Tomas kukuambia kwamba ukae mbele si kwamba nina lengo baya”
“Lengo liwe zuri au baya ila nakuomba tafadhali tuondoke. Nipelekea nyumbani kwangu, nikachukue vilivyo muhimu niondoke”
“Sawa”
Mrs Sanga akawasha gari na kuianza safari ya kwenda nyumbani kwa Tomas. Ukimya wa dakika kadhaa ukatawala ndani ya gari huku Tomas maombi yake yote kwa Mungu ni kufanikiwa kuondoka Tnazania kabla ya kukamatwa tena na polisi.
“Tomas”
“Naam”
“Kwa hiyo ndio mimi na wewe basi?”
“Tena sio basi ya herufi ndogo ni BASI ya herufi kubwa mama. Sihitaji kabisa kufa. Leo bado nusu nife na keshi keshi nilizo pitia…..Ahahh hapana kwa kweli, siwezi kuwa mjinga tena”
“Ila Tomas hiyo uliyo pitia ni mikwara tu”
“acha using** wewe mama. Nimepigwa shoti za umeme, nimewekewa bastola kichwani mwangu mara kadhaa. Nimeshuhudia rafiki zangu wakiuwawa kwa kupigwa risasi tena kikatili, sasa hivi una niambia mikwara. Acha ujinga bwana”
Tomas alizungumza kwa hasira huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Mrs Sanga akakosa cha kuzungumza zaidi ya kuendelea kuvumilia maumivu ya kuachwa na mwanaume anaye mpenda. Wakafika nyumbani kwa Tomas.
“Baki hapa”
Tomas alizungumza huku akifungua mlango wa gari hilo.
“Kwa nini jamani. Au uniruhusu kuingia ndani?”
“Kama vipi wewe ondoka”
“Tomas, acha kuwa na hasira. Kumbuka kwamba haya tuliyo yafanya yote ni kutokana na upendo wetu”
“Nisikilize wewe mwanamke mpnede mume wako. Nakama hujui, mumeo ana video ya ngono niliyo kuwa nina ku** mule ofisini kwake. Sasa wewe shangaa shangaa macho tu. Atakuua na wewe. Kwanza washa gari  lako usepe una niwekea kiwingu”
Tomas akashuka na kuubamiza mlango wa gari la Mrs Sanga. Mrs Sanga hakuridhila kuachwa kwa namna hiyo na Tomas, akaingia kwenye geti la nyuma anayo ishi Tomas na kuanza kumuita. Tomas akatoa fungua kwenye maua yaliyo katika chungu maalumu, kilichopo hapo mlangoni mwake. Akafungua mlango wake huku akiwa hamsikilizi chochote mrs Sanga.
“Tomas kumbuka kwamba nina kupenda. Kumbuka kwamba nina kuhitaji sana kwneye maisha yangu. Sihitaji kukuacha, wewe ndio kila kitu kwenye maisha yangu. Una nikuna kila sehemu ya mwili wangu, una nikata kiu yangu ya mapenzi. Kwanini nikuache’
Mrs Sanga alizungumza huku akiwa ana angua kilio kizito sana.
“Hivi wewe mwanamke ume rogwa ehee?”
“Ndio Tomas, umeniroga na penzi lako. Umeniroga baba, sisikii wala sisemi chochote. Ume niroga baba”
Mrs Sanga alizungumza huku akiishika miguu ya Tomas aliye simama huku  akimtazama kwa macho ya hasira. Tomas ana tamani hata achukue kiti kizito na kumponda mwanamke huyo kichwani mwake.
“Tomas, nipe, nipe vya mwisho mwisho. Nitakupa chochote utakacho taka. Tafadhali Tomas”
Tomas akashusha pumzi nzito, kwani hakuwahi kutegemea kwamba ipo siku mwana mama huyo ata kuwa ni king’ang’anizi namna hiyo.
                                ***
“Baby ni lini uta kuja tena?”
Magreth alimuuliza nabii Sanga kwa sauti ya upole huku akimtazama usoni mwake. Nabii Sanga hakujibu chochote zaidi ya kuendelea kuminya minya simu yake.
“Sanga si nimekuuliza jamani”
“Mage sijui lini nitakuja. Kichwa changu hakipo sawa. Tafadhali nina kuomba uniache kwa muda”
“Nikuache kwa muda, au kwa sababu una kwenda kukutana na mke wako si ndio. Umeniacha na ny**ge kitandani kisa mke wako si ndio. Nini maana ya upendo wako ulio kuwa una niahidi au ulitaka kunivunja tu usichana wangu ili unichezee si ndio?”
Magreth alizungumza kwa hasira iliyo chananyikana na wivu.
“Usifike huko Magreth tambua kwamba nakupenda ndio maana nimefanya kila kitu kwa ajili yako”
“Kila kitu kwa ajili yangu. Okay rudi kitandani tuendelee
“Mage kuna maswala yametokea ya kifamilia nina takiwa kuyaweka sawa. Ninakuomba unielewe basi mke wangu”
“Ahaa….una hofia mke wako kukutolea siri za kumf** sijui huyo kijana wa kinigeria?”
Nabii Sanga moyo ukamstuka sana. Hakuamini kama Magreth ana weza kugundua swala hilo. Kabla nabii Sanga hajazungumza kitu chochote, simu yake ikaita, akaitazama na kukuta ni dereva wake. Akaipokea na kuiweka sikioni mwake.
“Ndio”
“Nimefika hapa nje”
Nabii Sanga akakata simu na kuuzungusha mkono wake mmoja akiunoni mwa Magreth.
“Nisikilize Mage. Haya aaliyo yazungumza huyu mwanamke hayana ukweli wowote ndani yake. Usimsikilize kwa maana ame changanyikiwa”
“Kwa hiyo una niachaje mimi?”
“Kivipi?”
“Mimi nina bado naham”
“Mage nakuahidi kesho asubuhi nitakuja kabla hata sijafanya jambo lolote”
“Una nidanyanya”
“Kweli nina kuja”
“Poa”
Magreth alijibu kishingo upande, taratibu nabii Sanga akambusu Magreth mdomoni kisha akatoka ndani humo. Akatoka kabisa getini na kuingia kwenye gari la kanisa.
“Shikamo mzee”
“Marahaba. Ngoja kwanza”
Nabii Sanga alizungumza huku akiendelea kuitafuta simu ya mke wake kwa kutumia GPRS. Haikuchukua muda mrefu sana akafanikiwa kuiona ni sehemu gani simu ya mke wake inapo patikana. Jambo lililo mstusha sana ni kwamba eneo hilo alipo mke wake kwa sasa ndio maeneo ya mtaa anao ishi Tomas. Nabii Sanga hakuhitaji kupoteza muda zaidi ya kumueleza dereva wake waelekee nyumbani kwa Tomas.
    Magreth mara baada ya kumshuhudia nabii Sanga akiondoka, akaingia bafuni na kuoga kwa haraka huku saa yake ya ukutani ikionyesha majira hayo ni saa sita usiku.
‘Wata kubali tu’
Magreth alizungumza huku akimalizia kuoga. Akarudi chumbani kwake na kuvaa nguo aliyo iona ina mpendeza. Akampigia Sheby simu na kumuomba aweze kufika nyumbani kwake hapo haraka iwezekanavyo.
‘Pesa itasaidia kufanikisha ninalo kwenda kulifanya’
Magreth alizungumza huku akichukua kiasi cha pesa na kuingiza kwenye wallet yake ya kike. Sheby akafika nyumbani hapo na Magreth akaingia kwenye gari na kuondoka eneo hilo.
“Usiku huu kweli pale Mwanyamala wana weza kuturuhusu kuingia?”
“Ndio”
“Kwani kuna madokta ambao una fahamiana naye?”
“Hapana ila twende”
Baada ya nusu saa akafika katika hospitali ya Mwanayamala. Kitu alicho kifanya Magreth ni kutoa kiasi cha pesa kila sehemu ambayo walipewa kizuizi cha kuingia.
“Sheby nisubiri hapa ndani ya gari.”
“Sawa”
Magreth akashuka ndani ya gari hilo na moja kwa moja akaelekea katika chumba alicho lazwa Evans Shika. Kwabahati nzuri akamkuta akiwa bado hajalala.
“Mage mbona usiku sana vipi?”
“Nimekuja kukuona, nimeshindwa kulala Evans”
Magreth alizungumza huku akiufunga mlango wa chumba hicho kwa ndani. Kwa jinsi n** zilivyo utawala mwili wake, Magreth alishindwa kabisa kujizuia. Akamsogelea Evans kitandani alipo lala.
“Evans nina kupenda. Nimeshindwa kuvumilia, nimeshindwa kabisa kulala kwa ajili yako. Nakupenda sana”
Magreth alizungumza huku akivua gauni lake hilo alilo livaa. Akabakiwa na ch*pi pekee huku kifuani mwake, maziwa yake yaliyo kaa vizuri yakimtamanisha Evans ambaye kwenye kipindi chote cha maisha yake hakuwahi kukutana na mwanamke kimwili.
                                ***
“Toms tafadhali mume wangu, naomba tafadhali”
Mrs Sanga alizungumza huku akimshika Tomas eneo lake nyeti. Hisia kali alizo nazo Tomas kwa mrs Sanga, zikaifanya hasira yake kuanza kumyeyuka tartaibu. Mrs Sanga akafungua zipu ya suruali ya Tomas na kumtoa jo**wa Tomas
Mrs Sanga akavua nguo zake huku Tomas akikamilisha kumvua Mrs Sanga


“Hembu simama hapa”
Nabii Sanga alimuambia dereva wake mara baada ya kuona gari la mke wake nje ya geti la nyumba ya Tomas. Hasira ikaanza kumtafuna nabii Sanga, huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana.
“Usishuke kwenye gari na zima taa za gari”
“Sawa mzee”
Nabii Sanga akashuka kwenye gari huku akianza kutembea kwa hatua za tahadhari hadi sehemu lilipo gari la mke wake. Akachungulia katka kioo cha nyuma na hakuweza kumuona mtu yoyote. Akajaribu kufungua mlango wa dereva na akaukuta wazi. Akafungua na kutazama ndani na kukuta funguo ya gari ikiwa ina ning’inia eneo hilo. Nabii Sanga akaachia msunyo mzito huku akichomoa funguo hiyo, akafunga mlango wa gari hilo huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.
Akalitazama geti dogo la nyumba ya Tomas, kisha akaanza kutembea kuelekea kwenye geti hilo. Akajaribu kulisukuma kwa ndani na kwa bahati nzuri likafanikiwa kufunguka. Akatazama nyumba hiyo na kukuta taa zote zikiwa zime zimwa. Akaanza kutembea kwa hatua za kunyata kuelekea katika mlango wa kuingilia ndani kabisa ya nyumba hiyo. Vilio na miguno ya kimahaba, vikamafanya nabii Sanga kujawa na hasira kwani ana vitambua vilio vya mke wake. Mlango wa kuingilia sebleni hapo, upo wazi kidogo, hivyo ikamuwia uraisi kwa nabii Sanga kuingia pasipo Tomas na mrs Sanga kuweza kujua chochote. Nabii Sanga akahisi moyo wake ukilipuka kwa mapigo ya moyo yatokanayo na hasira. Hakuamini kabisa kumuona mke wake akiwa amekunjwa vibaya kwenye sofa moja la sebleni hapo, huku Tomas akizungusha kiuno chake kwa kasi sana. Nabii Sanga akaupeleka mkono wake ukutani na kuminya swichi ya taa za sebleni hapo na zote zikawaka na kuwafanya Tomas na Mrs Sanga kustuka sana huku wakitazamana na nabii Sanga aliye simama mlangoni hapo huku akiwa amefura kwa hasira kiasi cha kushindwa hata ajue awafanye nini wasaliti wake hao.



==>>SIN 19
Mrs Sanga na Tomas wakajikuta wakikaa kwenye sofa hilo miili yao ikizidi kutetemeka kwa woga. Nabii Sanga, akaangaza macho yake sebleni hapo, ili aweze kupata kitu cha kuwaadhibu Tomas na mke wake ila akakosa kitu cha maana. Nabii Sanga akafunga mlango wa kutokea ndani humo huku akikunja mikono ya shati lake ambayo ni mirefu. Hapakuwa na hata mmoja wao aliye weza kusimama ili kukimbia.
“Endeleeni”   
Nabii Sanga alizungumza huku akiwakazia macho. Akaitazama meza ya chakula iliyopo karibu na sebleni hapo, kwa bahati nzuri akaona kisu. Akakifwata na kukichukua huku macho yake yakiwa makini sana kwa Tomas na mke wake.
“Endeleeni”
Nabii Sanga alizungumza huku akikaa akiwasogelea karibu. Tomas hakika hakuweza hata kusimamisha jog** wake, kwani hali ya hofu ime mtawala sana mwilini mwake.
“Nimesema endeleeni muna nitumbuliaa nini macho”
Nabii Sanga alifoka, huku akimpiga Tomas mgongoni mwake kwa kutumia ubapa wa kisu hicho kikubwa kiasi. Nabii Sanga akatoa simu yake mfukoni na kuweka sehemu ya video na kuanza kurekodi kitu kinacho endelea eneo hilo.
“MnyonyE denda huyo”
Nabii Sanga alizungumza huku akikisukumiza kichwa cha Tomas karibu na kichwa cha mke wake.
“Mu…m….mmu…m….”
Mrs Sanga alitamani kuzungumza jambo, ila maneno yakashindwa kumtoka kabisa kinywani mwake. Nabii Sanga akamtandika Tomas kofi zito la mgongo na kumfanya Tomas aweweseke na kuanza kumnyonya mrs Sanga lipsi zeke huku wote wawili wakiendelea kutetemeka kwa woga.
“Mnyonye vizuri, una tetemeka nini?”
Nabii Sanga alifoka huku akimpiga tena Tomas ngumi ya mgongo.
“Na wewe malaya mzee changamka”
Nabii Sanga alimuambia mke wake ambaye amelegea kabisa kwa woga.

Nabii Sanga alizungumza huku jasho likimvuja mwili mzima. Tomas, kila alivyo jaribu kuvuta hisia zake ili jog** wake aweze kusimama ila ina shindikana jambo lililo na maumbile.


Nabii Sanga hakika hakuwa na masiraha hata kidogo. Mrs toka aolewe hakuwahi kumuona mume wake akiwa ame kasirika kwa kiasi hicho, kwani hadi mcho yake ambayo siku zote yametawalia na weupe, ila leo yamekuwa mekundu mithili ya mvuta bangi aliye bobea katika kilevi hicho.

Kila kinacho endelea nabii Sanga ana kirekodi vizuri sana. Hadi dakika tano zina malizika hapakuwa na majibu mazuri kwa Tomas.
Nabii Sanga alipo ona hakuna chochote kinacho endelea kwa Tomas, akaihifadhi video hiyo anayo irekodi katika simu yake, kisha akairudisha simu yake mfukoni. Akachukua shati la Tomas na kumfunga kikono yake kwa nyuma, huku mrs Sanga muda wote huo amejibanza kwenye sofa huku akilia kwa woga sana.


“Nyinyi huwa muna wafanya watu wanao mtumikia Mungu ni malaika wasio na hasira. Hata mimi nina unyama ndani yangu. Sasa acha leo nikuonyeshe mbwa wewe”


Nabii Sanga alizungumza huku akimtandika mangumi ya mbavu Tomas ambaye muda wote anatetemeka. Tomas ubavu wa kujinasua mikononi mwa nabii Sanga kama mwanaume, wote umemuishia. 


“Nilikupa onyo la kuondoka nchini Tanzania, ila hujalitii sasa, ikifika alfajiri na nikakuona hapa Tanzania nina kuua”


“Wewe malaya vaa nguo tuondoke. Utakwenda kunijubu vizuri nyumbani”
Mrs Sanga akakosa hata nguvu za kusimama. Nabii Sanga akamsogelea mke wake, akamzaba makofi mawili ya mashavuni na kumfanya mwana mama huyo kusimama huku akitetemeka. Mrs Sanga akaanza kuvaa nguo zake taratibu. Alipo maliza, kwa ishara nabii Sanga akamuamrisha mke wake kumfungua Tomas shati hilo alilo mfunga mikono kwa nyuma.
“Ni onyo la mwisho. Endapo nitakuona hapa Tanzania kwa mara nyingie nitakuua”


Nabii Sanga alizungumza huku akimnyooshea Tomas alicho kishika mkononi mwake. Mara baada ya kuzungumza hivyo akamshika mkono mke wake. Akafungua mlango na kutoka nje. Dereva alipo muona nabii Sanga na mke wake wanatoka getini akawasha gari na kuwafwata walipo.


“July wewe nenda nyumbani. Nitaondoka na gari la mama hapa”
Nabii Sanga alizungumza huku uso wake ukiwa umejaa tabasamu pana sana ili kumfanya dereva wake asielewe ni nini kinacho endelea.
“Sawa baba nikutakie usiku mwema”
“Na wewe pia”


July akawasha gari na kuondoka eneo hilo. Nabii Sanga akamfungulia mke wake mlango na kumuingiza ndani, kisha na yeye akazunguka upande wa dereva na kuingia. Akawasha gari na kuondoka eneo hilo kwa mwendo wa kasi sana.


Tomas kwa unyonge akanyanyuka kwenye sofa hilo huku maeneo aliyo ingiliwa yakiwa yamejawa na maumivu makali sana. Akaelekea moja kwa moja bafuni kwake, akaanza kujisafisha huku akiwa katika hali ya wasiwasi na maumivu ya moyo. Chuki dhidi ya Mrs Sanga na nabii Sanga ikaanza kuutawala moyo wake, akatamani kujiua ila moyoni mwake, kila anapo kumbuka familia yake akajikuta aki airisha mawazo hayo mabaya.
‘Lazima nilipe kwa hili. Nitahakikisha nina lipa’
Tomas aliapa kimoyo moyo huku akiweka nguo zake katika begi la mgongoni kwa ajili ya safari ya kuelekea Afrika kusini.
                                ***


“Ohoo…iaa…aiiia…..Mage……”
Evans alitoa miguno ya kimahaba, huku akisikilizia ulimi wa Magreth


“Taratibu utani…tonesh….a kidonda”
Evans alizungumza huku akimtazama Magreth aliye pagawa “Haya”
Magreth alizungumza huku akikizungusha kiuno chake

“Ohoo asante sana Evans. Wewe ndio mwanaume wa maisha yangu”
Magreth alizungumza 

 “Kwa nini ime kuwa hivi?”
Evans aliuliza huku akimtazama Magreth usoni mwake.
“Eehee!!”
“Kwa nini umeamua kunipa kitu ambacho sijawahi kupewa na mwanamke wa aina yoyote katika maisha yangu?”
“Kweli hujawahi kupewa penzi na mwanamke yoyote?”
“Ndio, wewe ndio mwanamke wa kwanza kunipa penzi. “Jamani, usijali nitakuwa nina kupa kila mara utakapo hitaji”
“Mage”
“Bee”
“Una nipenda?”
“Ndio, nina kupenda sana Evans. Kwenye maisha yangu sijawhai kumpenda mwanaume wa ina yoyote zaidi yako wewe”
“Kweli?”
“Ndio, nina kupenda. Natambua ni jambo gumu sana kwa mwanamke kumuambia mwanaume kwamba ana mpenda ikiwa ndio mara yao ya kwanza. Ila nimejizuia nimeshindwa Evans nakuomba uweze kunielewa katika hio”
“Magreth nimekuelewa na hata mimi nina kupenda. Nitahakikisha kwamba nina kulinda maisha yangu yote na nitakutunza. Hii elimu ya biashara niliyo isomea, hakika ita tusaidia kukuza biashara ya maandazi uliyo nayo”
Magreth akajikuta akimkumbatia kwa nguvu Evans hadi kwa bahati mbaya aka muumiza eneo la jeraha.
“Ohoo pole mpenzi wangu”
“Nimepoa nakupenda sana Magreth”
“Nina kupenda pia Evans wangu”

                                ***
Nabii Sanga na mke wake wakafika nyumbani kwao. Mara baada ya nabii Sanga kusimamisha gari hilo, akashuka na kumfungulia mke wake mlango.
“Shuka”
Nabii Sanga alizungumza kwa sauti nzito iliyo jaa hasira na uchungu mkali sana. Mrs Sanga kwa woga akashuka huku akiuatazama macho hayo ya mumewe yanayo dhihirisha kwamba leo hali sio nzuri. Nabii Sanga kwa upendo wa kuwadanganya walinzi wake. Akamshika mkono mke wake na wakaingia ndani na hapakuwa na mlinzi wa aina yoyote ambaye aliweza kutambua kwamba watu hao wapo katika uhasama mkali sana. Nabii Sanga na mke wake wakaingia chumbani, kitendo cha nabii Sanga kufunga mlango wa chumba hicho, akachomoa mkanda wa suruali yake na kuanza kumcharaza mke wake mikanda mfululizo huku kwa mara kadhaa akimziba mdomo wake ili asitoe kelele yoyote ya kuomba msaada.
“Nina kupa kila kitu, ila una kwenda kufanya ujinga kwa yule kijana sasa leo utanitambua”
Nabi Sanga alizungumza huku akiendelea kupiga mke wake, kipigo ambacho toka waowane hakuwahi kumpiga mke wake. Nabii Sanga ili kelele zisitoke, chumbani humo, akamburuta mke wake hadi katika bafu lililopo chumbani kwao. Akaziba eneo linalo tolea maji katika sinki lao la kuogea. Akafungulia bomba na maji yakaanza kujaa katika sinki hilo.
“Leo utanijua mimi ni nani. Malaya mkubwa wewe”
“Mume wangu nakuomba unisamehee….Sinto rudia tena mimi”
Mrs Sanga alilia kwa uchungu sana, hakuwahi kupigwa hata kofi na mume wake huyo toka walipo fahamiana, ila leo ana chezea kipigo kikali sana. Nabii Sanga, akamshika mke wake kichwa chake na kumvuta karibu na sinki hilo lililo jaa maji. Akakidumbukiza kichwa cha mke wake na kumfanya aanze kutapatapa kwa kukosa pumzi.
“Leo nina kubatiza kwa jina la SANGA malaya wewe”
Nabii Sanga alizungumza huku akimchomoa mke wake na kumfanya akohoe sana kwa kupaliwa na maji.
“Utanisaliti eheee?”
“Hapana mume wangu, sinto rudia tena. Sinto kusaliti tena”
Nabii Sanga akaona maelezo hayo ya mke wake hayamtoshelezi. Akakidumbukiza tena kichwa hicho na kumfanya mrs Sanga azidi kutapatapa. Akakitoa kichwa cha mke wake na kumtazama tena.
“Uta nisaliti?”
Nabii Sanga aliuliza huku meno yake akiwa ameyang’ata kwa hasira hadi yakaanza kutoa mlio wa kusagana.
“Haki ya Mungu vile mume wangu. Sinto kusaliti. Nitakupenda hadi kufa kwangu, nisamehee, nisamehe mume wangu”
“Yaani ungekuwa si mama wawanangu leo hii ninge kuuaa mbwa wewe”
Nabii Sanga alizungumza huku akiiachia shingo ya mke wake kwani kwa kupigo hicho na kitendo alicho mfanyia Tomas, sidhani kama mrs Sanga ana weza kurudia usaliti wa ndoa yake iliyo unganishwa kanisani miaka mingi sana ya nyuma.
                                ***
    Askari anaye pitia kukagua wahalifu katika mahabusu za kituo hicho cha polisi, akagundua kutoweka kwa Tomas katika sero aliyo kuwa amefungiwa peke yake. Kwa haraka akaanza kutoa taarifa kwa wezake walipo kituoni hapo na wao wakafika eneo hilo na kweli wakashuhudia kwamba Tomas hayupo.
“Eeeheee Mungu watu, hii imekula kwetu”
Askari mmoja alizungumza huku akijawa na wasiwasi kwani, kupotea kwa kijana huyo itakuwa ni shida kwa askari wote waliopo zamu. Wakawasiliana na RPC pamoja na IGP na kutoa taarifa hiyo ya kupotea kwa Tomas. Agizo la IGP kwa vijana wake walipo chini yake akiwemo RPC Karata ni kuhakikisha kwamba wana toa taarifa kwenye vituo vya usafiri vyote Tanzania ikiwemo Bandari zote, Airport zote, Vituo vyote vya mabasi, dalalada na mipaka yote ya jiji la Dar es Salaam inayo ruhusu mtu kutoka nje ya Dar es Salaam kufungwa. Huku mipaka yote ya Tanzania kufungwa na ulinzi mkali sana ukazidi kuimarishwa katika maeneo hayo. Picha ya Tomas, ikaanza kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii pamoja na vituo vya televishion huku vituo vya redio vikipewa sifa za Tomas na kuzitangaza usiku huo huo, ili hata ikitokea mtu kumuona jambazi huyo aweze kutoa taarifa kwa askari. Zawadi ya milioni kumi ikatengwa na jeshi la polisi na kwa yoyote atakaye fanikisha kukamatwa kwake basi ata pewa zawadi hiyo.
                                                                                                ITAENDELEA   
Haya sasa, Tomas amesha gundulika kwamba hayupo katika mahabusu za makao makuu ya polisi. Picha yake na habari ya kutafutwa kwake kwa sasa imeenea Tanzania nzima. Je atafanikiwa kutoroka nchini Tanzania pasipo kukamatwa? Endelea kufatilia kisa hikii cha kusisimua, usikose sehemu ya 20.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger