Monday 29 June 2020

Prof. Palamagamba Kabudi 'Autaka Ubunge' Kilosa

...
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Prof. Palamagamba Kabudi amesema yupo tayari kuwatumikia wananchi wa jimbo la kilosa iwapo watamhitaji kwenda kufanya hivyo.

Kabudi ameonyesha nia hiyo leo tarehe 29 Juni 2020 wilayani Kilosa, wakati akihutubia katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa mahandaki manne yenye urefu wa kilomita 2.7 ya reli ya kisasa kutoka Morogoro hadi Makutupora.

Licha ya kwamba hakutaja hadharani nia ya kugombea ubunge Kilosa, Profesa Kabudi amesema, kama atapata kibali kutoka kwa Mungu, hatakataa kuwa mtumishi wa wananchi wa Kilosa.

 
“Mimi ni kijana wenu, mzaliwa wa hapa na niwaambie kuwa mkinihitaji kuwatumikia niko tayari” amesema Kabudi.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger