Saturday 27 June 2020

Naibu Waziri Wa Afya Dkt.mollel Atembelea Bohari Ya Dawa (Msd) Jijini Dar Es Salaam

...
Na WAMJW- DSM.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt Godwin Mollel ametembelea Bohari ya Dawa (MSD) Makao Makuu na kuzungumza na watumishi wa taasisi hiyo ili kufahamu namna taasisi hiyo inavotekeleza majukumu yake.

Akizungumza na viongozi wa Bohari ya Dawa Jijini Dar es Salaam Dkt Mollel amesema lengo la kutembelea taasisi hiyo ni kuangalia maboresho katika uagizaji, utunzaji na usambazaji wa dawa vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ili kuboresha huduma ya afya nchini.

Amesema maboresho hayo ni njia ya kuelekea mafanikio ya pamoja katika kutatua changamoto za wananchi hususani katika upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara.

Kwa upande wake mtendaji mkuu wa MSD Maja Jenerali Gabriel Saul Mhidze (Dkt) amesema ujio wa naibu waziri umeongeza chachu katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi kiujumla pamoja na utekelezaji wa maelekezo yanayo tolewa na wizaya ya afya ili kuendana na kasi inayohitajika katika sekta ya afya.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger