Wednesday, 10 June 2020

TAKUKURU Makao Makuu Kuwahoji Wabunge 69 wa CHADEMA Kuhusu Matumizi Ya Fedha Za chama

...
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, inatarajia kuwahoji wabunge 69 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuhusu tuhuma za matumizi mabaya ya fedha, 
 
Taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 10 Juni 2020 na Doreen Kapwani, Afisa Uhusiano wa Takukuru imesema mahojiano hayo yatafanyikia Makao Makuu ya taasisi hiyo Dodoma na yatakamilika wiki ijayo.

“Ni kweli kuwa Takukuru imewaita waheshimiwa wabaunge wa Chadema na waliowahi kuwa wabunge wa chama hicho kwa ajili ya mahojiano.”

“Hatua hii ni muendelezo wa uchunguzi wa malalamiko dhidi ya matumizi mabaya ya fedha nza Chadema unaoendeshwa na Takukuru ambapo hatua iliyopo sasa ni kuwahoji wabunge 69,” amesema Doreen


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger