Friday 5 June 2020

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya 12 na 13

...
Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188


ILIPOISHIA   
RPC akaifunua maiti moja na akamuonyesha Tomas maiti ya Selemani D iliyo chakaa kwa kupigwa risasi.
“Hawa jana tu walikuwa hai, wakisherekea pesa nyingi walizo zivuna kwa kumteka nabii Sanga. Ila sasa hivi wapo hapa hawajitambui. Wewe upo hai ila hii bastola yangu ina weza kukulaza na wewe hapa na ukajumuika na hawa wezako. Niambie ni wapi wezako walipo mpeleka nabii Sanga la sivyo, utaungana nao na wewe utaingizwa kwenye jokofu lile pale ukiwa maiti”


RPC alizungumza huku akimuwekea Tomas bastola ya kichwani na kumfanya Tomas kuanza kutetemeka mwili mzima huku akiona mwisho wa maisha yake sasa umefika, tena ana fia ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti.
   
ENDELEA
Kwa woga ulio mtawala Tomas akashindwa kuizuia haja ndogo na kujikuta akijikojolea. RPC hakulijali hizo zaidi ya kuendelea kuzungumza kwa ukali huku akiwa ameishikilia bastola hiyo.
“Kwa nini ulimteka nabii Sanga, nini alikufanyia ikiwa wewe ni mtu wake wa karibu?”
“Ehee…..!!”
“Nini alikufanyia?”
RPC alizungumza kwa ukali na kumfanya Tomas kuanza kukumbuka jinsi alivyo anza mahusiano na mke wa nabii Sanga. Kukolea kwa mapenzi yao kuliwafanya washiriki katika dhambi ya kumteka nabii Sanga ili wazuie mpango wake wa kumfungulia mgahawa na kumnunulia nyumba Magreth.
“Oya andaa hilo jokofu la hapo kwa ajili ya huyu mjinga, nina muua na siri itabaki kati yako mimi na wewe?”
RPC alizungumza huku akimtazama muhudumu wa Mochwari. RPC akaikoki bastola hiyo na kumfanya Tomas kuzidi kuweweseka. Japo ame fanya makosa, ila hatamani kabisa kufa.
“Nitasema ukweli”
Tomas alijikuta akiropoka na kumfanya RPC atoe simu yake mfukoni. Akaweka upande wa kurekodi sauti na kusubiria ukweli ambao Tomas ata ukiri.
“Zungumza nina subiria.”
“Ahaa miezi kadhaa iliyo pita nabii Sanga na mke wake walinipa jukumu la kuwatafutia eneo kubwa la kujenga mji, kule kigamboni. Jukumu la kusimamia mpango huo, alimkabidhi mke wake. Hivyo nilipata muda mwingi sana wa kuongozana na mke wake kwenda kutembelea maeneo mbali mbali ambayo nilikuwa nimeyapata.”
Tomas alizungumza huku akiendelea kutetemeka. RPC hakuishusha bastola yake, hii ni kuhakikisha kwamba Tomas ana zungumza kila kitu.
“Tulijikuta tukianza mahusiano ya kimapenzi na mwana mama huyo”
RPC akastuka sana ila hakuhitaji kuonyesha mstuko huo kwani ana hitaji kufahamu mambo mengi sana kutoka kwa Tomas.
“Tulifanya kwa siri sana. Kadri siku zilivyo zidi kwenda ndivyo jinsi penzi letu lilivyo zidi kuchanua. Kuna siku nabii Sanga alinipigia simu na kuniambia kwamba ana hitaji nimtafutie sehemu ya kufungua Mgahawa na nyumba ya kupanga maeneo ya Mikocheni. Alikuwa na mpango wa kumpangishia binti mmoja ambaye ni muumini pale kanisani kwake”
“Binti huyo ana itwa nani?”
“Magreth. Swala hilo nabii Sanga aliniomba nisimuambie mke wake kabisa. Ila kwa upande mmoja roho iliniuma kuona binti mdogo ana nunuliwa nyumba ya milioni mia tano. Nilimueleza mke wake na mkewe aka toa wazo la kumteka mume wake, hadi wiki ijayo ndio aachiliwe na watekaji ili aende nchini Nigeria kwenye kikao cha wachungaji na manabii”
RPC akajikuta akishusha pumzi taratibu. Katika miaka yote ya kuifahamu familia ya nabii Sanga, hakutarajia kwamba mke wa nabii huyo ipo siku ata fanya kosa kubwa kama hilo.
“Niliwatafuta vijana na nikawapa kazi hiyo na waliweza kuikamilisha kikamilifu”
Tomas alizungumza huku akiendelea kutetemeka kwa woga.
“Kwa hiyo mzizi wa tukio zima ni mke wa nabii SANGA?”
“Ndio”
Taratibu nabii RPC akashusha bastola yake na kuirudisha kiunoni mwake. Aka yahifadhi mazungumzo hayo ya Tomas kwenye simu yake na kuiweka mfukoni.
“Zirudishe hizo maiti”   
Nabii Sanga alimueleza mtu huyo anaye hudumia Mochwari kisha wakatoka katika chumba hicho. Akamuingiza Tomas kwenye gari lake, kabla ya yeye kuingia, akatafuta namba ya kijana wake mmoja na kumpigia.
“Ndio mkuu”
“Upo wapi?”
“Bado nipo nyumbani kwa nabii Sanga.”
“Hakikisha huyo mke wake hatoki kwenda eneo lolote”
“Kwa nini mkuu?”
“Hupaswi kunihoji kwa nini, fwata amri yangu”
“Samahani sana mkuu.”
RPC akakata simu na kuingia ndani ya gari.
“Huyo Magreth ana ishi wapi?”
“Ahaa sifahamu, ila wale vijana mulio waua ndio walimfwatilia msichana huyo na kufahamu ni wapi ana fikishwa na nabii Sanga. Ila kwa mimi sijui”
RPC akamtazama Tomas machoni mwake kwa sekunde kadhaa na kuamini kwamba anacho kizungumza ni kitu cha ukweli. Nabii Sanga akawasha gari hilo na kurudi makao makuu ya polisi. Akakabidhi Tomas kwa vijana wake na akarudishwa mahabusu. RPC moja kwa moja akapitiliza hadi ofisini kwake, akajifungia na kuisikiliza sauti ya Tomas jinsi inavyo toa maelezo hayo.
“Haki ya Mungu hawa wanawake hawaaminiki”
RPC alifikiria huku akitafakari ni jinsi gani anavyo weza kuvumbua mbele ya jamii kesi hiyo ambayo kwa namna moja ama nyingine ina weza kwenda kuligawanya kanisa la nabii Sanga huku naye akiwa ni miongoni mwa waumini wa kanisa hilo.
                                ***
    Magreth akabaki kama alivyo zaliwa huku akimtazama nabii Sanga anaye malizia kuivua suruali yake. Akatembea taratibu hadi kitandani. Akamlaza nabii Sanga chali,huku taratibu akimtazama.. Aibu aliyo kuwa nayo awali, yote ime muondoka. 


Magreth kwa jinsi alivyo pagawishwa na kiasi cha pesa alicho pewa na nabii Sanga, hakuona haja kumbania mzee huyo, huku moyoni mwake akiamini kwamba swala zima la kumpenda Evans litakuja hapo baade akiwa amesha weka kila kitu sawa. Mtanange wa wakati huu hakuwa wa kinyonge,  Nabii Sanga alizidi kuchanganyikiwa na kupagawa na penzi bichi kabisa la Magreth.
“Nitakupa kila utakacho kitaka Mage”
Nabii Sanga
“Kweli?”
“Haki ya Mungu vile, sijawahi kupata penzi tamu kama lako.”
“Uta nilinda dhidi ya mke wako?”
“Ndio baby, hawezi kukugusa”
“Niahidi”
“Nakuahidi, haki ya Mungu vile”
Magreth alifanya mahojiano hayo huku akijituma vzr. Kuokoka kwake hakukumfanya ashindwe kumpagawisha nabii Sanga. Hadi mzunguko una kwisha kila mmoja akajikuta akiwa ameridhika

“Niambie nini una hitaji nikufanyie?”
“Aahaa…kuna yule mgonjwa wangu kule hospitalini. Nilikuwa nina ombi moja”
“Ombi gani baby”
“Nimezungumza naye na amenieleza shida alizo pitia. Siku ile aliyo niokoa aliweza kuibiwa vyeti vyake vya kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu na siku ile aliondoka kwa rafiki yake na hakuwa na pakuishi. Nina omba nitakaopo hamia kwenye ile nyumba kigamboni, niweze kuishi naye”
Magreth alizungumza huku akiwa amejilaza kifuani mwa nabii Sanga
“Ahaha. Una muamini?”
“Kama aliweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yangu. Nina muamini kwa maana wale Panya road siku zile wange nibaka na sijui ningekuwa kwenye maisha gani. Inawezekana ningekuwa nimesha kufa sasa”
“Nimekuelewa mke wangu. Basi akitoka hospitalini, utaishi naye. Ila hakikisha kwamba huni saliti”
“Kwa nini nikusaliti mpenzi wangu, ikiwa usichana wangu wewe ndio ume bahatika kuutoa. Au huniamini?
“Nakuamini tena sana kwa maana nime jionea jinsi gani ulivyo ”
“Nashukuru mume wangu”
“Leo usiku nitarudi kwangu, ila hakikisha kesho una kwenda kununua asset zote za ndani kisha zinapelekwa kwenye hiyo nyumba mpya.”
“Sawa mpenzi”
“Kuna rafiki yangu mmoja ana kampuni ya magari. Nitamuambia kesho akutafutie gari zuri na lenye hadthi na wewe”
“Asante sana mpenzi wangu, ila mimi siwezi kuendesha gari?”
“Ohoo usijali katika siku hizi ambazo nita kuwa hapa Tanzania, nitakufundisha gari, hadi nina ondoka nina imani utakuwa umesha mudu kuendesha”
“Sawa sawa mume wangu”


                                **********
‘Kama porini hakuweza kuonekana na majambazi tumewakuta wao wenyewe, je watakuwa wamemuaa? Hapana hajauwawa au wamemuachia?’
RPC aliwaza kichwani mwake huku akijaribu kujiongeza kutokana na mazungumzo ya Tomas.
‘Kama wamemuachia ata kuwa amekwenda wapi? Au ame fahamu kwamba mke wake ndio msaliti?’
‘Ila kama aliamua kumnunulia mwanamke nyumba ya milioni mia tano na kuhitaji kumfungulia mgahawa, nina imani kwamba atakuwa ana muamini sana huyo mwanamke na kumpenda’
‘Magreth…..Yaa Magreth anaweza kufahamu ni wapi alipo nabii Sanga. Ni lazima tumpate huyu msichna’
RPC baada ya kupata mwanga katika swala la kuto kumpata nabii Sanga, akanyanyuka kwa haraka na kuelekea mahabusu alipo fungiwa Tomas.
“Nileteeni mtu wa kuchora”
RPC alimuagiza bodyguard wake huku akimtazama Tomas ambaye amejikunyata kwenye kona ya chumba hicho.
“Nahitaji utuelezee sifa za Magreth. Si una mkumbuka kwa sura?”
“Ndio nina mkumbuka”
Polisi mwenye taaluma ya kuchora akafika eneo hilo. Tomas akaanza kuelezea muonekano wa Magreth.
“Ana sura nyembaba kiasi iliyo chongoka kwenye kidevu chake. Ana macho yaliyo kaa muundo kama wa yai, ila si makubwa. Ana pua ndogo ndogo kiasi na lipsi zake pia ni ndogo kiasi. Ni mrefu kama futi sita kasoro kidogo. Ana rangi ya chocolate fulani hivi.”
Kila alicho kieleza Tomas ndicho anacho kifanya mchoraji. Baada ya muda mfupi sura halisi ya Magreth ikapatikana kwenye karatasi ya mchoraji.
“Imekamilika?”
“Ndio mkuu”
RPC akaitazama picha hiyo ya Magreth, kweli ni mwanamke mzuri sana na anaye vutia. RPC akamgeuzia Tomas picha hiyo.
“Ndio huyu?”
“Ndio ndio huyo huyo wala hujakosea”
Tomas alizungumza wa kubabaika.
“Vijana wako hawakukuambia ni wapi walipeleleza hadi wakatambua anapo ishi?”
“Hapana hawakunijulisha kwani lengo lao kubwa ilikuwa ni nabii Sanga na waliweza kumfwatilia nabii Sanga alipo kuwa ana rudi kwake ndio waka mvamia na kumteka.”
RPC akaikunja vizuri karatasi hiyo yenye picha ya Magreth. Akaeleka kwenye kitengo cha askari wanao dili namitandano.
“Scan hii picha na unitafutie huyu binti”
“Sawa mkuu”
Kijana huyo aka iscan picha hiyo na kuiingiza kwenye computer yake na kuanza kutafuta picha hiyo ya Magreth kwenye mtandao. Haikuchukua muda maelezo yote kuhusiana na Magreth yakatokea katika computer hiyo. Imekuwa ni rahisi sana kwa askari hao kuipata kwani Magreth ni miongoni mwa  walio jisajili kwenye kitambulisho cha taifa hivyo taarifa zote zinazo muhusu yeye zipo hapo.
“Magreth Jonas Asinga”
RPC alisoma maelezo yanayo onekana kuhusiana na Magreth.
“Hembu tuma maelezo hayo kwenye mitando ya simu watupatie information za binti huyo. Nina imani mtandoa mmoja wapo utakuwa na information zake za mawasiliano.”
“Sawa mkuu”
Kijana huyo akaandika email kwa mitandoa mikubwa mmine ya mawasiliano , huku email hiyo ikwia huku ikiwa na wito wa kuomba data za mteja Magreth Jonas Asnga, ikiwemo namba yake ya simu. Baada ya dakika tano kijana hiyo akajibiwa email yake na mtandao wa simu ambao Magreth ana utumia.
“Waombe simu zote zilizo pigwa jana na leo watutumie”
Maombi hayo hayakuweza kukataliwa kwa maana yana tokea makao makuu ya polisi. Wakaanza kuorozesha audio za mazungumzo yote aliyo yafanya Magreth kwa siku ya jana na leo. Wakaanza kusikiliza mazungumzo hayo ambayo yanamuhusisha Magreth na nabii Sanga ambaye alimpa maelekezo ya kwenda kuchukua pesa ofisini kwake. Wakazidi kuendelea kusikiliza mazungumzo hayo hadi jinsi MagreLth aivyo wasiliana na majambazi hao na kuwajulisha amefika Mkinga.
    Mazungumzo ya siku ya leo kati ya nabii Sanga na muhasibu wake akimuomba amfwate sehemu alipo, ikampa picha RPC ya kuweza kufahamu kwamba nabii Sanga yupo sehemu gani na yupo sehemu salama. Ila kutokana ni ahadi ambayo alitoa kwa wananchi kwamba jeshi la polisi lita hakikisha kwamba lina mrudisha nabii Sanga salama salmini mikononi mwa familia yake. Ikamlazimu RPC kuandaa kikosi cha vijana wake wanne na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwa Magreth, huku zoezi hilo likifanyika kwa siri sana pasipo askari wengine kuweza kufahamu ni kipi RPC wao ame kigundua.


 ==>>SIN -Sehemu ya 13  
“Huu ndio mtaa anao ishia huyo binti?”
RPC aliwaambia vijana wake huku wakitazama mtaa huu wa uswahilini wenye mchanaganyiko wa watu wa kila aina.
“Msichana mwenyewe anafanania hivi?”
RPC alizungumza huku akiwaonyesha picha ya Magreth iliyo chorwa kwenye karatasi hiyo.
“Huyu ame fanya kosa gani mkuu?”
“Ina sadikika huyu ndio yupo na babii Sanga?”
“Mkuu unataka kuniambia kwamba huyu binti ndio alite mteka nabii Sanga?”
“Hapana, hapa inaonekana nabii Sanga alisha achiwa na watekaji, ila akaamua kuelekea kwa kimada wake kujificha”
“Mmm!! Sasa kwa nini asiende kwake au kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi?”
“Hilo ni swali ambalo tutalipata mara baada ya kuwapata wote wawili. Hembu waulize hao watoto juu ya picha hiyo”
“Sawa”
Askari mmoja aliye valia nguo za kirai. Akashuka kwenye gari hilo na kuwasogelea watoto wanao cheza pembezoni mwa barabara hiyo ya vumbi.
“Mambo”
“Poa shikamoo”
“Marahaba. Nina swali nahitaji kuwaliza”
“Uliza tu?
“Muma mfahamu dada huyu?”
Askari huyo aliwaonyesha watoto hao picha ya Magreth, wenye miaka kati ya sita hadi kumi.
“Ndio tuna mfahamu ana itwa dada Mage”
“Ana ishi wapi?”
Watoto hawa wakatazamana, kisha mmoja wao akaonyesha ishara ya kuhitaji kupewa pesa. Askari huyu akatoa noti ya shilingi elfu tano mfukoni mwake na kuwakabidhi. Mtoto huyo mwenye kimo kirefu kuliko wezake wote, akaipokea pesa hiyo.
“Ana kaa pale kwa bi Ngedere. Ile nyumba yenye kibaraza mbele na ngazi?”
“Ile nyumba yenye matairi mbele na wale wamama walio kaa??”
“Ndio”
“Sawa asanteni”
Askari huyo akarudi kwenye gari.
“Daa kweli kazi ipo bosi, yaani hadi watoto wameanichomoa pesa ya kuelekezwa tu”
“Hahaahaa, ni wapi alipo sema?”
Askari huyo akawaonyesha wezake nyumba hiyo. Taratibu wakaegesha gari hilo kwenye hiyo nyumba na wakashuka askari wawili ambao wote wamevalia nguo za kiraia. Gari hilo iana ya Toyota VX V8 likawastua sana wapangaji wa nyumba hiyo walio kuwa wamekaa kibarazani.
“Habari zenu?”
“Salama”
“Tume mkuta Magreth?”
Wapangaji hawa wkatazamana, katika siku mbili tatu hizi Magreth amekuwa akiletwa na magari ya kifahari jambo ambalo lime zua maswali mengi kwa wamama hao wanne.
“Ndio yupo”
“Ahaa muna weza kutusaidia kutuonyesha chumba chake?”
“Mmm shosti yetu amekuja kufumaniwa nini?”
Mama Boka aliwanong’oneza kwa sauti ndogo wezake hao kwa maana wana sikia sauti ya mwanaume katika chumba cha Magreth ila hawajamuona mwanaume ambaye yupo ndani humo.
“Ahaa ingieni humo ndani, chumba cha pili, mkono wa kulia ndio chumba chake”
“Tuna shukuru”
“Ila nyinyi ni kina nani?”
“Ni watu wema kabisa musiwe na mashaka”
“Mmmm haya”
Askari hao wakaingia ndani humo, wakasimama kwenye mlango wa Magreth na kusikilizia miguno ya kimahaba inayo tokea ndani humo.
“Gonga mbona una shangaa?”
“Wapo kwenye starehe zao bwana”
“Sisi tupo kazini. Ngoja nigonge”
Askari huyo akaanza kugonga kwa nguvu hadi Magreth na nabii Sanga ambao wapo katikati ya mapenzi mazito wakastuka.
“Nani huyo?”
Nabii Sanga aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka.
“Atakuwa ni mama mwenye nyumba. Kwani sauti yangu ina sikika hadi huko nje?”
“Sijajua, ila mbona naona ina sikika hapa hapa”
“Ngoja”
Magreth akajichomoa ,. Akashuka kitandani, akajifunga tenge na kufungua mlango huo huku akiwa na jazba kubwa, na amepania kama ni mama mwenye nyumba basi ata mpatia jibu litakalo mtingisha mwana mama huyo mwenye maneno mengi. Magreth akastuka sana mara baada ya kukutana na sura za wanaume ambao haja wahi kuwaona hata siku moja.
“Wewe ndio Magreth?”
“Ndio ni mimi. Ny….i….nyi ni kina nani?”
Magreth aliuliza huku woga ukiwa umemtawala. Mahojiano hayo yakamfanya nabii Sanga kutafuta suruali yake nakuivaa kwa haraka huku kichwani mwake akihisi kwamba watu hao ni majambazi.
“Tume mkuta nabii Sanga?”
Swali hilo lika wachanganya kabisa, nabii Sanga na Magreth kwani watu hao hawajajitambulisha hadi sasa hivi.
“Ahaa nyingi ni kina nani?”
Ikamlazimu Magreth kuuliza swali hilo kabla ya kujibu swali alilo ulizwa.
“Sisi ni maofisa wa polisi kutoka kituo cha kati”
“Waache waingie”
Nabii Sanga alimuambia Magreth na kumfanya ageuke na wakatazamaana huku Magreth akiwa na mshangao mkubwa sana.
“Waache wapite”
“Karibuni”
Askari hao wakaingia na kumkuta nabii Sanga akiwa ana vaa shati lake
“Habari yako mzee”
“Salama. Tumekuja kukuchukua na kukuweka mikono salama”
“Hapa pia ni mikono salama. Ila nina elewa nini munataka kufanya. Sasa hivi ni saa kumi na mbili, acheni kigiza kiweze kuingia nami nitatoka ndani humu”
“Ila muheshimiwa, tupo hapa na mkuu wetu na ametoa agizo la sisi kukuchukua na kukupeleka kwenye gari lake lipo hapo nje”
“Nendeni mukamuite mkuu wenu”
“Ahaa kwa nini?”
“Nyinyi nendeni mukamuite yeye, ndio nahitaji kuzungumza naye”
Askari mmoja akatoka ndani humo na kurudi kwenye gari. Akamueleza RPC nini anacho hitaji nabii Sanga.
“Waondoeni hao wamama hapo barazani, sihitaji wafahamu juu ya uwepo wangu mtaani hapa?”
“Sasa tuta fanya nini mkuu”
“Fanyeni chochote.  Nyinyi ni askari hakikisheni kwamba wana ondoka eneo hilo”
Askari hao watatu wakajishauri na kushuka kwenye gari hilo. Wakawasogelea wana mama hao wanao endelea kutazama kila kinacho endelea na kila mmoja ana hamu ya kufahamu ni nini kinacho endelea kwa mpangaji mwenzao.
“Sisi ni maofisa polisi. Muna ishi humu ndani?”
Wamama hao wakastuka kidogo huku wakiwatazama askari hao.
“Ndio”
“Basi kila mmoja aingie chumbani kwake na asidhubutu mtu kuchungulia”
“Kwani kuna nini?”
“Mama hatuna muda wa kutangaza au kukueleza kuna nini. Ingieni ndani”
Askari mmojaa alizungumza kwa ukali sana na kuwafanya mama Boka na wezake wanyanyuke huku wakikunja mkeka walio kuwa wameukalia. Wakaingia ndani huku wakiwa na hofu kubwa. Askari walipo hakikisha kwamba hali imekuwa shwari, bodyguard wake akamfungulia mlango na akashuka kwenye gari hilo na kuingia ndani. Nabii Sanga aka simama na kuepeana mkono na RPC kwani ni watu wanao fahamiana kwa muda mrefu na pia wana heshimiana.
“Naomba mutupishe”
RPC alizungumza na vijana wake wakatoka na kusimama kwenye kordo hiyo kuimarisha ulinzi.
“Huyu ni Mage, binti ambaye aliweza kujitolea kunipa msaada wa kipesa kipindi nilipo kuwa nimewekwa kizuizini na majambazi”
“Ahaa sawa mzee. Nina litambua hilo kwa maana tume fwatilia mazungumzo ya simu ya binti. Hayo mazungumzo ndio yameweza kutusaidia sisi kuweza kufika hapa”
“Sawa sawa”
“Tumekuja kwa jambo moja tu. Tunahitaji tukupeleke nyumbani kwako kwa maana sehemu hii sio salama kabisa.”
“Sawa hilo halina shaka. Ila nahitaji huyu msichana asi sumbuliwe kwa chochote na wala asiweze kuitwa kituoni kwa mahojiano”
“Sawa sawa”
“Mage kuwa na amani na kesho hakikisha kwamba una fanya ule utaratibu nilio kuagiza uweze kuufanya”
“Sawa baba”
“Kwa heri”
Nabii Sanga na RPC pamoja na vijana wake wakatoka ndani hapo na moja kwa moja wakaeleka katika gari na kuondoka. Magreth akashusha pumzi na kujitupa kitandani, kwani uwepo wa maaskari hao umemfanya awe katika wakati wa mashaka. Ila alipo kumbuka kwamba ana kiasi kikubwa cha pesa benki, basi mawazo na matatizo hayo ya polisi yakamuondoka kabisa kichwani mwake.
“Sasa mimi ni tajiri”
Magreth alizungumza kwa furaha. Mlango wake ukagongwa na akasikia sauti ya mama Boka ikimuita.
“Nakuja”
Magreth alizungumza huku akishuka kitandani. Akajifunga tenge lake vizuri na kufungua mlango.
“Ehee upo salama wewe?”
“Ndio kwa nini?”
“Hawa polisi wamekuja kufanya nini hapa?”
“Hahaa mbona muna mashaka hivyo au mume hisi nime tekwa na watu ?”
“Weee!! Mwanzo tulihisi kwamba ume kuja kufumaniwa. Ila walipo tuambia tuingia ndani na kujifungia, hapo ndipo matumbo yalipo tupata moto”
“Kweli shosti yetu tulijawa na wasiwasi mwingi sana. Haya tuambie ni nini kinacho endelea?”
Mama Amina naye aliuliza.
“Ngoja kwanza niwashukuru majirani zangu kwa kuishi nami kwa amani japo tulikwaruzana katika maswala ya zamu za usafi na ununuzi wa luku, ila yote katika yote. Mungu yeye pekee ndio anaye fahamu nini tunacho pitia kwenye haya maisha”
“Mbona una ongea hivyo?”
Mama mwenye nyumba aliuliza huku akitokea mlango wa uwani na kuwafanya wapangaji hao walio simama kwenye mlango wa Magreth kumshangaa.
“Kesho nina hamia Kigamboni. Kuna nyumba yangu nimenunua kule”
Magreth aliwadanganya wezake hao katika swala zimala kununua nyumba.
“Mage ume nunua nyumba!!?”
“Ndio mbona muna shangaa au sina hadhi ya kununua nyumba?”
“Mmmm kwa kazi gani ulio kuwa nayo? Hembu acha kuwaongopea wezako na wewe”
Mama mwenye nyumba alizungumza kwa kejeli.
“Hahaa, wewe baki hapo hapo kwenye hili banda lako la kuku”
“Hahaaa!! Banda la kuku, ulitumwa kujakukaa hapa kupanga?”
Bi Ngedere alizungumza kwa hasira kwani hakupenda nyumba yake iweze kudharauliwa namna hiyo.
“Mage hembu achana naye. Tupe siri ya mafanikio yako kwa maana siku mbili hizi tumekuona una shushwa kwenye magari ya kifahari na wala hatukuoni jikoni ukijumuika nasi katika swala zima la kuchoma maandazi”
“Ni kweli jamani, kesho mimi nina hama. Haya yaliyo tokea humu ndani kwangu sinto weza kuwaambia. Leo mumesha pika?”
Magreth alibadili mada kwa kuwaliza maswali.
“Mimi nimepika toka mchana”
“Mimi nasubiri saa mbili mbili nisonge ugali nile na wanangu”
“Mimi nita nunua maandazi tu ninywe na chai.”
“Mimi bado sijapika”
“Bi Ngedere na wewe?”
“Na mimi nini, una pesa ya kunipa nikanunue chakula?”
“Ahaa…maneno yote ya nini mama angu. Hivi wewe mama una shindwa kuwa na kinywa kizuri cha kuzungumza?”
“Babuu weweee nikiwa na kinywa kizuri nita faidika na nini?”
“Haya nisamehe mimi. Jamani nisubirini”
Magreth akaingia ndani na kuchukua laki moja na nusu na kutoka nayo nje. Akawapa wapangaji wezake wanne kila mmoja elfu thelethini.
“Jamani hizo mutanunua mukipendacho usiku huu”
Wapangaji hao wakajawa na furaha sana, huku wengine wakimuona Magreth ndio mkombozi wao kwani baadhi yao tayari wamesha anaza kuwakimbia vijumbe wa michezo yao wanayo cheza kila siku kwa kukosa pesa za kutoa.
“Wewe mama utakula jeuri yako. Hata mia sikupi na kesho nitakagwa vitu vyangu vyote vya ndani na hata kijiko sikupi. Muangalie ndio maana Mungu alikunyima kimo kirefu ndio maana akili zako zipo kama kimo chako”
Maneno ya Magreth yakawafanya wapangaji wezake hao kucheka kwa dharau huku wakigongeana mikono na kumfanya mama mwenye nyumba ajisikie vibaya sana.
                                ***
“Kile mulicho kiona pale nyumbani kwa yule binti musi mueleze mtu yoyote”
Nabii Sanga alizungumza huku gari hilo la RPC likizidi kuchanja bunga kueleka nyumbani kwake.
“Hatuto mueleza mtu”
RPC alijibu huku akiwa amekaa siti ya mbele, pembeni kabisa ya dereva.
“Nashukuru kusikia hivyo.”
“Upo salama lakini?”
“Ndio nipo salama”
Wakafika nyumbani kwa nabii Sanga. Wakaelekea moja kwa moja sebleni na kumfanya mtoto wa nabii Sanga kumkimbilia baba yake na kumkumbatia kwa nguvu. Mfanyakazi wake wa ndani naye akafanya hivyo alivyo fanya binti huyo. Kelele za furaha zinazo sikika sebleni zikamfaya mrs Sanga kukurupuka ndani kwake na kukimbilia sebeeni. Mapigo ya moyo yakamstuka mara baada ya kukutanisha macho yake uso kwa uso na mume wake ambaye hajaonyesha sura yoyote ya kumchangamkia. RCP akaingiza mkono wake mfukoni na kutoa pingu huku akimtazama mrs Sanga anaye shuka kwenye ngazi huku akilazimisha tabasamu la kinafki kwani shida zote zilizo tokea katika siku mbili hizi yeye ndio chanzo.
                                                                                                ITAENDELEA
Haya sasa, Nabii Sanga amesha rudi nyumbani kwake, moyoni mwake ana ufahamu ukweli kwamba mke wake ndio adui namba moja. RPC ana toa pingua mfukoni je ata mfunga mrs Sanga na kuondoka naye kama mtuhumiwa? Endelea kufwatilia kisa hichi cha kusisimua, usikose sehemu ya 14.

 


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger