Friday 5 June 2020

Rais Magufuli aagiza wanaogawa barakoa zisizothibitishwa Washughulikiwe

...
Rais wa Tanzania, Dkt.  John Magufuli amewaagiza viongozi katika maeneo mbalimbali nchini kuwakamata na kuwahoji wale wote wanaogawa barakoa kwa wananchi ili waeleze zimethibitishwa wapi kuwa zinafaa kutumika.

“Ukimuona mtu anagawa barakoa kwa wananchi, ashikwe akaulizwe zimethibitishwa wapi,” amesema Rais Magufuli wakati akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT).

Aidha, amewataka wananchi kuwa makini kwa kutokupokea barakoa ambazo hawajui mgawaji amezitoa wapi kwani vifaa hivyo vinaweza kutumiwa kusambaza virusi vya corona.

“Tusidanganywe kwa kuletewa mabarakoa ambayo hatujui yametoka wapi, tutaeneza corona bila sisi kujua. Anapokuletea mtu barakoa hujui hata ameitoa wapi kataa, mwambie kavae wewe na mke wako na watoto wako nyumbani.”

Amewasihi wananchi wanaotaka kuvaa barakoa washone wenyewe kwani watakuwa na uhakika wa usalama wake.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger