Wednesday, 10 June 2020

MTOTO WA MIAKA 4 AUAWA KWA KUKATWA PANGA SHINYANGA...MUUAJI NAYE AUAWA

...
Picha haihusiani na habari hapa chini

Na mwandishi wetu- Shinyanga Press Club blog
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la James Mhoja(36)ameuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira kali baada ya kumuua kwa kumkata mapanga mtoto Emmanuel John(4) wakati akicheza na watoto wenzake nyumbani kwao.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga Joseph Paul amesema tukio hilo lilitokea jana Juni 9 majira ya saa 9 alasiri kwenye Mtaa wa Ndala Manispaa ya Shinyanga, wakati mtoto huyo alipokuwa anacheza nje ya nyumba yao ndipo mtu huyo alimvamia na kumshika kisha kuanza kumkata mapanga.

"Mtuhumiwa wa mauaji ya mtoto huyo naye aliuawa na wananchi kwa kumponda mawe na katika uchunguzi wetu wa awali,tumebaini alikuwa anatatizo la ugonjwa wa akili na bado tunaendelea na uchunguzi wa tukio hili"amesema kaimu Kamanda Paul.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger