Wednesday 3 June 2020

Mtoto Afariki Kwa Kushambuliwa Na Fisi Shinyanga, RPC Atoa Wito Kwa Wazazi

...
SALVATORY NTANDU
Wazazi na Walezi Mkoani Shinyanga wametakiwa kuchukua tahadhari kwa watoto wao dhidi ya  wanyama aina ya Fisi ambao wamekuwa wakionekana katika maeneo mbalimbali  na kusababisha madhara kwao ikiwemo ya vifo.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba June 2 wakati akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na tukio la kushambuliwa  hadi kufariki dunia kwa mtoto wa miaka miwili na nusu  aliyehamika kwa jina la Charles Christian katika kitongoji cha Mwagala kata ya Ibadakuli.

Amesema  tukio hilo limetokea June Mosi mwaka huu majira ya saa moja usiku akiwa anacheza na watoto wenzake nje ya nyumba yao alijeruhiwa kwa kung'atwa na fisi sehemu za usoni na kisha kuburuzwa umbali wa mita 50 ndipo wananchi walipoamua kumfukuza akamuachia na kukimbia baada ya kuzidi kwa kelele za wananchi hao.

“Wanyama hawa wamekuwa wakizurura ovyo hivyo ni Budi kila mzazi /Mlezi kuhakikisha watoto wao wanakuwa salama na kwani matukio ya watu kushambuliwa na fisi ama mifugo yamekuwa ni mengi hivyo chukueni Tahadhari,”alisema Magiligimba.

Amefafanua kuwa  Charles  alifariki dunia akiwa njiani akisafirishwa kwenda katika hospitali ya rufaa ya kanda ya  Bugando jijini Mwanza  kwa matibabu na mwili wake  umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga kwaajili ya kukabidhiwa ndugu zake kwaajili ya Matibabu.

Mwisho.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger