Sunday, 5 April 2020

Trump Awataka Wamarekani kujiandaa kwa idadi ya kutisha sana ya vifo vya Corona

...
Rais wa Marekani Donald Trump amewaonya Wamarekani kujiandaa kwa idadi ya kutisha sana ya vifo kutokana na virusi vya corona katika siku chache zijazo. 

Trump amesema Marekani inaingia katika kipindi ambacho idadi ya vifo itapanda kwa kasi. 

Hata hivyo, Rais huyo amesema Marekani haiwezi kuendelea kusitisha shughuli zake milele akiongeza kuwa itafika wakati ambao maamuzi magumu yatafanywa.

 Wakati visa vya maambukizi ya COVID-19 nchini Marekani vikithibitishwa kupindukia 300,000 kukiwa na zaidi ya vifo 8,300, kuna habari za kutia moyo nchini Italia na Uhispania ambako idadi ya imeanza kupungua. 

Sasa kuna visa milioni 1.17 vya maambukizi vilivyothibitishwa kote duniani na kumekuwa na vifo 63, 437 tangu mlipuko wa virusi hivyo ulipoanza nchini China mwaka jana. 

DW


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger