Sunday 26 April 2020

Wenye Virusi vya Corona Nchini Kenya Wafika 355....Ni Baada ya Wengine 12 Kuongezeka

...
Watu wengine 12 wamepatikana na virusi vya corona nchini  Kenya ndani ya masaa 24 yaliyopita.

Sasa idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo nchini Kenya imefikia 355 tangu kisa cha kwanza kiripotiwe Machi 13 mwaka huu. 

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumapili, Aprili 26, na katibu msimamizi katika Wizara ya Afya Rashid Aman. 

Aman amesema  kuwa hakuna kifo zaidi kimeripotiwa kutokana na virusi hivyo na idadi ya waliofariki imesalia watu 14.

Watu 8 wamepona virusi hivyo na kufikisha idadi ya waliopona kuwa 106


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger