Tuesday 28 April 2020

Kitwanga Atishia Kuigomea Bajeti Wizara Ya Maji

...
Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga, amesema atapiga kura ya hapana kwenye bajeti kuu na Wizara ya Maji, iwapo hawatafafanua kuhusu mgawanyo wa mradi wa India utakaotekelezwa katika miji 28 wakati ungeweza kutekekezwa katika miji 50.

Amesema kuwa mradi huo hauna thamani ya fedha kwa kuwa kila mmoja unagharimu dola milioni 17 sawa na Shilingi Bilioni 39 wakati kiuhalisia unatakiwa kugharimu Sh.Bilioni 12," amesema.

"Chukua dola Bilioni 50 gawanya kwa miji 28 utapata milioni 17.2 sawa na Bilioni 39 na zaidi, bila kufanya marekebisho sitaunga mkono hoja kwa kuwa najua kinachoendelea na ushahidi nikishauleta...kama mlisema mkataba wa Lugumi ni mbaya sasa hii ni zaidi ya Lugumi na siku nikipewa nafasi nitasema kuhusu Lugumi, "amesema.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger