Saturday, 18 April 2020

Idadi ya maambukizo ya Corona Marekani yapindukia laki saba

...
Idadi ya watu waliombukizwa virusi vya Corona nchini Marekani imepindukia laki saba huku idadi ya wanaoaga dunia kwa ugonjwa wa Covid-19 ikiongezeka kwa kasi nchini humo.

Takwimu za hivi punde zinaonyesha kuwa, watu 710,272 wameambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani huku 37,175 wakiaga dunia na kuifanya nchi hiyo kuwa ndio iliyoathiriwa zaidi na virusi hivyo duniani.

Italia inashika nafasi ya pili kwa idadi kubwa ya watu walioaga dunia kwa virusi vya Corona ambapo hadi sasa watu 22,745 wamefariki dunia nchini humo, ingawa kwa upande wa idadi ya maambukizo inashika nafasi ya tatu. 

Uhispania yenye idadi 20,002 ya vifo vya Corona, jumla ya watu 190,839 wameambukizwa virusi vya Corona katika nchi hiyo ya bara la Ulaya.

Nchi zinazofuata ni Ufaransa, Ujerumani na Uingereza na kulifanya bara la Ulaya kwa sasa kuwa kitovu cha virusi vya Corona.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger