Thursday 2 January 2020

Papa Francis aomba radhi kwa kumchapa kibao muumini Aliyemvuta kwa Nguvu

...
Papa Francis ameomba radhi kwa kumpiga kibao mkononi mwanamke mmoja aliyemvuta kwa nguvu wakati akisalimiana na waumini katika mkesha wa mwaka mpya. Papa amesema alikosa uvumilivu na kwamba kitendo kimeweka mfano mbaya.

Papa alikuwa akisalimiana na watoto na mahujaji na wakati akigeuka mwanamke mmoja aliyekuwa kwenye umati wa watu waliokuwa karibu aliuvuta mkono wa Papa kwa nguvu karibu amuangushe.

Hali iliyomfanya Papa kugeuka na kumpiga makofi mawili mkononi mwanamke huyo kwa hasira.


Badaye Papa alikiri kwamba alishindwa kujizuia na yeye pia huwa anakosea kama binadamu wengine.

Hivyo anaomba radhi kwa kitendo hicho kwa muumini huyo na kila mtu.

Kitendo cha Papa cha kumzaba makofi ya mkononi mwanamke huyo, kimezua mjadala kwenye mitandao ya kijamii, hasa Twitter, wengi wakimuunga mkono Papa.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger