Wednesday 29 January 2020

Umeme Ukerewe Bei Juu, Unit Moja Inauzwa Tshs 2500 Badala Ya Tshs 100

...
Waziri wa Nishati nchini Tanzania, Dk Medard Kalemani ametoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella kuhakikisha anafuatilia gharama za umeme zinazotozwa kwa wananchi wa kisiwa cha Ukerewe mkoani humo.

Imeelezwa leo bungeni kuwa Watumiaji wa umeme katika Wilaya ya Ukerewe Mkoa wa Mwanza wanatumia nishati hiyo kwa gharama ya Sh2,500  kwa uniti moja badala ya Sh100 inayotozwa kwa maeneo mengine.

Hayo yamesemwa bungeni jijini Dodoma leo  na Mbunge wa Ukerewe (CCM), Joseph Mkundi wakati akiuliza swali la nyongeza akiitaka Serikali  kuchukua hatua.

Akijibu swali la nyongeza la mbunge huyo, Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema jambo hilo halikubariki.

Dk Kalemani amesema Mtanzania yeyote anayetumia umeme usiozidi uniti 70 kwa mwezi, anapaswa kulipia kiwango cha Sh100 kwa uniti siyo gharama ya huko.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger