Monday 27 January 2020

Evariste Ndayishimiye Aidhinishwa Kuwa Mrithi Wa Rais Pierre Nkurunziza

...
Chama tawala cha Burundi CNDD-FDD, kimemteua katibu wake mkuu kuwa mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa Burundi utakaofanyika Mei 2020.

Jenerali Evariste Ndayishimiye ameidhinishwa na chama kama mrithi wa Nkurunziza wa Burundi.

Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye ameteuliwa kama mgomba wa urais katika uchaguzi utakaofanyika Mei 2020 kumrithi Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza.

Jenerali Ndayishimiye ameteuliwa Jumapili kupeperusha bendera ya chama cha CNDD-FDD katika kikao kisicho cha kawaida kilichofanyika Gitega, mji mkuu wa kisiasa baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa saa tatu ya chama tawala cha CNDD-FDD.

Bwana Ndayishimiye ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri katika siasa za Burundi waliokaribu na Pierre Nkurunziza.

Pia ni miongoni mwa waliokuwa waasi wa CNDD-FDD aliyejiunga baada ya kunusurika katika mauaji ya kikabila ya wanafunzi wa Wahutu katika chuo kikuu cha Burundi mwaka 1995.

Jenerali Ndayishimiye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa chama cha CNDD-FDD tangu Agosti 2016.

Kabla ya kuteuliwa kwake, alikuwa Waziri wa mambo ya ndani na ulinzi wa umma.

-BBC


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger