Thursday 2 January 2020

Polisi adaiwa kukatwa sehemu za siri na mkewe

...
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linamshikilia Flora Adamu (23), mkazi wa Shinyanga Mjini, kwa tuhuma za kumkata mumewe sehemu za siri, ambaye ni askari Polisi mwenye Namba H, 8980 Pc Kazimiri, kwa madai ya kumtuhumu kutokuwa muaminifu katika ndoa.

Imeelezwa kuwa mtuhumiwa huyo alimtuhumu mumewe kuwa ana  nyumba ndogo.

Akizungumza na wanahabari, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, Deborah Magiligimba, alisema tukio hilo limetokea Desemba 28 mwaka jana, majira ya saa 6:30 usiku wakati wanandoa hao wakiwa wamelala.

Alisema wakiwa wamelala, ghafla Flora aliamka na kuanza kumnyatia, huku akiwa ameshika kitu chenye ncha kali kisha kumkata mumewe sehemu za siri na kumjeruhi vibaya.

“Baada ya askari huyu kukatwa uume wake alikimbizwa kwenye Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Shinyanga ili kupatiwa matibabu ya haraka, ambapo alilazwa kwa muda wa siku mbili  kisha kuruhusiwa kurudi nyumbani kuendelea kujiuguza kidonda,” alisema  Kamanda Magiligimba.

“Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi, ambapo mwanamke alikuwa akimtuhumu mume wake kuwa ana nyumba ndogo, ndipo akaamua kuchukua kitu chenye ncha kali kisha kuanza kuukata uume wa mumewe na kumjeruhi vibaya,” aliongeza.

Aidha, kamanda huyo alisema Jeshi la Polisi linamshikilia mwanamke huyo, na kwamba uchunguzi ukikamilika, atafikishwa mahakamani.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger