Friday 27 May 2016

Spika Job Ndugai (Mb) Afanya Mabadiliko Mengine ya baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge.

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (Mb) amefanya mabadiliko mengine ya baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge ili kuzingatia maombi ya baadhi ya Wabunge pamoja na mahitaji mapya yaliyojitokeza wakati wa utekelezaji wa shughuli za Kamati za Bunge.

Kwa mujibu wa taarifa yake, mabadiliko hayo yamefanywa kwa mujibu wa Kanuni ya 116(3) na (5) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Aprili 2016 ambapo yamehusisha maeneo manne ikiwemo; Kuhamishwa kwa baadhi ya wajumbe wa Kamati, Kualikwa kwa baadhi ya wajumbe katika Kamati ya Bajeti, Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Haki, Maadili, na Madaraka ya Bunge kuondolewa pamoja na Uteuzi wa wajumbe wapya katika kamati ya Haki, Maadili, na Madaraka ya Bunge.
 
Mabadiliko hayo ya wajumbe kwenye kamati yanaanza mara moja ambapo orodha ya wajumbe waliobadilishwa kamati na nafasi zao ni kama ifuatavyo; Wajumbe wanaohamishwa Kamati ni pamoja na Mhe. Ezekiel Magoyo Maige, (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya Nishati na Madini na kwa sasa anahamia Kamati ya PAC, Mhe. Allan Joseph Kiula (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na kwa sasa anahamia Kamati ya PAC, Mhe. Omary Tebweta Mgumba (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya Sheria Ndigi na kwa sasa anahamia Kamati ya PAC, Mhe. Rhoda Rdward Kunchela (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya Masuala ya UKIMWI na kwa sasa anahamia Kamati ya PAC.

Wengine ni Mhe. Joseph George Kakunda (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya PIC na kwa sasa anahamia Kamati ya PAC, Mhe. Ahmed Ally Salum (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya PAC na kwa sasa anahamia Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Neema William Mgaya (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na kwa sasa anahamia Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii pamoja na Mhe. Salma Mohamed Mwassa (Mb) ambaye alikuwa katika Kamati ya Bajeti na kwa sasa anahamia Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii.

Taarifa inaeleza kuwa, Wajumbe waalikwa katika Kamati ni pamoja na Mhe. Andrew John Chenge (Mb) ambaye yupo katika Kamati ya Sheria Ndogo, Mhe. Joseph Roman Selasini (Mb) ambaye yupo katika Kamati ya LAAC, Mhe. Dkt. Dalali Peter Kafumu (Mb) ambaye yupo katika Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Mhe. Japhet Ngalilonga Hasunga (Mb) ambaye yupo katika Kamati ya PAC, Mhe. Albert Obama Ntabaliba (Mb) ambaye yupo katika Kamati ya PIC pamoja na Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb) ambaye yupo katika Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Aidha, Walioondolewa katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ni pamoja na Mhe. Dkt. Haji Hussein Mponda (Mb) pamoja na Mhe. Najma Murtaza Giga, (Mb).

Wanaoteuliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka Ya Bunge ni pamoja na Mhe. Asha Abdalla Juma (Mb). Mhe. Emmanuel Mwakasaka (Mb) pamoja na Mhe. Augustino Manyanda Masele (Mb).
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger