Saturday 2 April 2016

Rais Magufuli Amteua Hilda Nkanda Kuwa Kamishna Wa Kazi

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bi. Hilda Nkanda Kabisa kuwa Kamishna wa kazi.

Kabla ya Uteuzi huo, Bi. Hilda Nkanda Kabisa alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Bi. Hilda Nkanda Kabisa, anachukua nafasi iliyoachwa na Bw. Sauli Kinemela ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Siza D. Tumbo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC).

Kabla ya Uteuzi huo, Prof. Siza Tumbo alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) aliyebobea katika masuala ya Uhandisi Mitambo ya Kilimo.

Prof. Siza Tumbo anachukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Evarist Ng'wandu ambaye alistaafu kwa mujibu wa sheria.

Uteuzi huu wa watendaji wakuu wa taasisi za serikali umeanza tarehe 26 Machi, 2016.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Chato

01 April, 2016
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger