Tuesday 19 April 2016

YALIYOJIRI BUNGENI LEO

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
April 19 2016 Mkutano wa tatu wa Bunge la kumi na moja umeanza, na lengo lilikuwa ni  ni kujadili na kupitisha bajeti ya Serikali.
Katika baadhi ya sekta zilizojadiliwa ni pamoja na Wizara ya  Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, na Philipo Gekul ambaye ni Mbunge wa Babati Mjini aliuliza ‘Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ulipaji ushuru wa huduma ambao ni asilimia 0.3 unaotozwa kutoka mitandao ya simu ambao kwa sasa halmashauri zimeshindwa kukusanya ipasavyo
Naibu Waziri Mhandisi Edwin Ngonyani  akajibu >> ‘Suala la ulipaji ushuru wa huduma za mawasiliano ambao ni asilimia 0.3 limekuwa tatizo kwa pande zote mbili, yaani Halmashauti ambazo ndio zinakusanya na kampuni ambazo zinakabiliwa na ugumu wa kuzilipa.’
Kwahiyo Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za mikoa, hivi sasa inafanyia marekebisho sharia ya fedha ya Serikali za mitaa ili kuwezesha kukusanya ushuru wa huduma za mawasiliano mahala pamoja
Baada ya hapo Spika wa Bunge Job Ndugai akaahirisha kikao, na kitaendelea tena April 20 2016 siku ya Jumatano

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger