Friday 22 April 2016

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA LINDI ASIMAMISHWA KAZI

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Serikali ya Mkoa wa Lindi imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, Oliver Vavunge na kumwomba Waziri Mkuu amsimamishe kazi Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Kilimo cha Umwagiliaji Maji Taifa kutokana na hasara ya Sh milioni 500 katika mradi wa umwagiliaji maji wa Kiwalala Narunyu, Lindi.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi aliyasema hayo jana wakati alipozungumza na wananchi kwenye Uwanja wa shule ya msingi ya Kiwalala wilayani humo juzi.

Zambi alisema kati ya fedha zilizowekwa kwa ajili ya kutekeleza mradi wa umwagiliaji maji ni Sh milioni 700, kati ya hizo Sh milioni 500 zilishatumika na kubakia Sh milioni 200.

Alisema mradi huo ulioanza mwaka 2011 mpaka mwaka huu haujakamilika na fedha zilishachukuliwa, na kufafanua kuwa mkurugenzi anaingia hatiani kutokana kutokuwa makini juu ya mradi huo katika usimamizi.

Alitoa fedha kwa nyakati tofauti kumlipa mkandarasi wa kwanza na kuvunja mkataba naye Sh milioni 121, wa pili alivunja na alitoa Sh milioni 226 na Sh milioni 116, mwaka jana.

Zambi alisema fedha hizo zilikuwa zinachukuliwa baada ya makandarasi wakidai kwa kazi walizokuwa wakizifanya kwa kuweka miundombinu ya shamba hilo.

Alisema Tume ya Umwagiliaji Maji nayo wataalamu wake hawakuwajibika ipasavyo juu ya usimamizi wa mradi huo kwani wao ndiyo waliotia hasara kwa mamlaka kutokana na barua zao walizokuwa wanaziandika juu ya mradi huo.

Barua ya kutoka Ofisi ya Kanda ya Kusini Tume ya Umwagiliaji Maji iliyoandikwa Septemba mwaka jana ilieleza kuwa mradi huo unatekelezeka kwa kiwango hicho cha fedha, na Novemba 27, mwaka jana, Kaimu Mkurugenzi wa Umwagiliaji Maji alifika na kuandika barua kuwa mradi huo hauwezi kutekelezeka, kinachotakiwa ni kufanya tathmini upya.

Alitoa ushauri kujenga banio dogo. Zambi alisema kwa jumla ushauri wao haukuwa mzuri na kusababisha hasara kwa mamlaka husika
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger