Tuesday 19 April 2016

TANESCO:HAKUNA MGAO WA UMEME TANZANIA

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeibuka na kukanusha taarifa zinazoenezwa na baadhi ya wananchi juu ya kuwepo kwa mgao wa umeme kutokana na kukatika kwa umeme kunakoendelea hivi sasa.

Katika mahojiano maalum na mtembezi.com Kaimu Afisa Mahusiano wa Tanesco, Leila Muhaji, amesema kukatika kwa umeme kunasababishwa na uboreshaji wa miundombinu chakavu iliyodumu kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20 na ujenzi wa vituo vipya vya umeme vitakavyofanyakazi kwa ufanisi zaidi.

Aidha amewataka wananchi kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki cha maboresho yanayoendelea kufanyika na kuahidi mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo watapata umeme wa uhakika na usiokatika mara kwa mara.

Ametoa wito kwa wananchi kushirikiana kwa karibu na shirika hilo hasa katika kipindi hiki cha mvua ili kuweza kutatua kwa haraka changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger